Skip to main content

WAANDISHI WA HABARI PEMBA WAPEWA ONYO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

 


NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@ 

 WAANDISHI wa habari kisiwani Pemba, wametakiwa kutojihusisha na ishara zozote zinazopelekea uvunjifu wa amani, iwe ni kabla, wakati baada ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu.

 

Wito huo ulitolewa August 28, 2025 na Mkurugenzi wa Baraza la Mji la Manispaa ya Chake  Chake, Shida Kombo Hamad, kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Chake Chake, wakati akifungua mafunzo ya siku moja kwa wanahabari hao, juu ya kuripoti habari za uchaguzi, katika ukumbi wa Shirika la Utangazaji Zanzibar ‘ZBC’ Pemba.

 

Alisema kuwa vyombo vya habari ni taasisi muhimu kwa jamii nchini, vinavyotoa huduma ya kuhabarisha, ambayo ni haki ya msingi raia kama inavyotamkwa kwenye katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu cha 18.

 

Alieleza kuwa, dhima ya sekta ya habari ni kuelimisha na kuburudisha jamii, ambapo kwa upande wa utangazaji, sekta ya habari inahudumiwa na vyombo vya habari ambavyo ni redio, television na mitandao ya kijamii, na sio kuwa sehemu ya uchafuzi wa amani.

 

"Hivyo ni wajibu wetu na ni jukumu la kila mmoja, kuhakikisha tunazingatia maadili ya habari, wakati wa kutekeleza shughuli zetu za utangazaji," alisema.

 

Akizungumzia sula la utolewaji wa leseni kwa vyombo vya habari, alisema kuwa Tume ya Utangazaji Zanzibar ‘TUZ’ ndio yenye dhamana hiyo, pamoja na kupanga na kusimamia masafa ya utangazaji, kudhibiti shughuli za watangazaji na maadili yao,’’alifafanua.

 

"Ni kawaida kwa vyama vya siasa kutumia vyombo vya habari katika kueleza sera, ilani na ahadi za zao, ili kufahamika na wananchi, hata hivyo vyombo vya habari havipaswi kusahau majukumu yao ya msingi,’’alifafanua Mkurugenzi huyo.

 

Hivyo aliwataka waandishi wa habari kuacha propaganda za chuki, na badala yake kuripoti taarifa kwa usahihi, na kuepuka kuingiza nchi kwenye vurugu.

 

Mapema Mrajisi Tume ya Utangazaji Zanzibar Ali Ayoub, wakati akimkaribisha mgeni huyo rasmi, alisema kuwa waandishi wa habari ni wadau wakubwa, katika kuripoti taarifa za uchaguzi, ndio maana Tume ya Utangazaji, imeona ipo haja kutoa taaluma kwao.

 


Afisa Sheria kutoka Tume ya Utangazaji Zanzibar, Khadija Mabrouk Hassan, akiwasilisha mada kuhusu kanuni za huduma za utangazaji wakati wa uchaguzi, alifahamisha kuwa mtoaji wa huduma ya maudhui ya utangazaji, ahakikishe kuwa taarifa zote zinaripotiwa kwa usahihi na bila upendeleo.

 

Aliwatakata waandishi wa habari, kutoripoti taarifa kwa mtazamo binafsi, ili kupendelea upande wowote wa kisiasa katika vipindi vyake, ili kuepusha uvunjivu wa amani.

 


Nae Meneja wa Huduma za Utangazaji kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ‘TCRA’ Andrew Kisaka, akiwasilisha mada muongozo wa utangazaji kuhusu machafuko na majanga, alieleza kuwa zaidi ya watu1,000 walipoteza uhai na wengine 600,000 kupoteza makazi nchini Kenya mwaka 2007.

 

Aidha mwaka 2011 nchini Nigeria, zaidi ya watu 800 walipoteza uhai katika machafuko yaliyotokea katika kipindi cha uchaguzi.

 

Hivyo ni muhimu kwa mwandishi wa habari kuepuka kusambaza taarifa za uongo, kuchochea migogoro au kutoa mahukwaa kwa wale wanaochochea migogoro au vurugu.

 

MWISHO.

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...