Skip to main content

WANAOTUMIA MLANGO WA NYUMA KUPITA, KUWAPITIA WENZAO WOTE HATARINI KIAFYA

 


 HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@

ZANZIBAR nayo, imebarikiwa kuwa na utamaduni wake unaofuatwa. 

Inajumuisha imani ya dini ya kiislamu, mila, desturi na maadili mema, yatokanayo na asili na watu wa ukanda wa pwani.

 Kuna mambo ambayo hujitokeza ikiwemo wigo na kusababisha kupotea kwa utamaduni husika, hatimae kuleta mabadiliko kwa vizazi.  

Utandawazi ni miongoni mwa mambo yanayosababisha kupotea kwa utamaduni huo, na kupelekea mmong'onyoko wa maadili na kuzaliwa chungu ya majanga.

 Miongoni mwa wigo huo ni suala la kufanya tendo la kuingiliwa kinyume na maumbile, ambalo huathiri afya ya uzazi kwa jamii.

 

Ingawa baadhi ya wanajamii, huona ni jambo la kawaida bila kuzingatia athari, huku wakiyatupilia mbali makatazo ya imani ya dini na hata sheria za nchi.

 

"Wake zenu ni mashamba yenu, basi waendeeni mashambani kwenu mnavyopenda'' surat  Al- Baqara (2:223) aya hii inawaruhusu wanaume kuwaendea wake zao kwa namna wanavyopenda.

 Ingawa ndani ya mipaka ya mashamba yao yaani sehemu ya mbele ya mwanamke, amabayo ni ya uzazi na sio nyuma kama wingine wanavyotafsiri.

 Kipengele cha 154 cha 'penal code Cap. 16 (2022) "unnatural offences" cha sheria ya Tanzania Bara kinafafanua kuwa, yeyote anaefanya tendo la kinyume na maumbile, akitiwa hatiani adhabu ya juu ya kifungo cha maisha au angalau miezi 30 ya kifungo.

 Kwa Zanzibar kipengele cha 150 inaeleza kuwa tendo la ngono, kinyume na maumbile (anal intercourse) ni kosa na linaadhibiwa hadi miaka 14 ya kifungo.

 

Utafiti uliofanywa na Nyblade et al (2017) nchini Tanzania unaonesha kuwa, tendo hilo hufanywa na watu wa rika tofauti, ambapo mwanamke mmoja kati ya wanne, wanashiriki tendo la kinyume na maumbile.

 Mratibu wa Tume ya Ukimwi Pemba Ali Mbarouk Omar anasema, kibaolojia maumbile ya njia ya haja kubwa haijaumbwa kufanya tendo la kujamiana.

 

 Ndio maana, kunatokezea madhara ikiwemo michubuko na kusababisha hatari ya kupata maambukizi ya virusi vya UKIMWI na magonjwa mengine ya kujamiana.

 

"Njia ya haja kubwa (rectum), zimeumbwa kutoa kinyesi na sio kuingiza jambo lolote, kama wanavyofanya baadhi ya watu kuingiza uume, hali ambayo ni kuharibu afya ya uzazi," anasema.

 

Katika ufafanuzi wake anasema, mbegu za mwanaume zinapoingia kwenye njia ya haja kubwa, husabisha muingiliano  wa homoni  ambazo mara nyingi, hupelekea ulegevu wa viungo,

 

Jingine ni kuwa na sauti nyembama na tabia ambazo zinazopelekea kuwa na muonekano tofauti, hivyo ikiwa ni mwanamme huwa na tabia za kike.

 

Kwa kawaida njia ya tendo la kujamiana ambayo anakuwa nayo mwanamke, hutoa utelelezi au maji ya matayarisho ya tendo la kujamiana.

 

Ingawa kwa njia ya haja kubwa haifanyi hivyo, kwani ina ukavu wakati wa jimai na kuleta michubuko ya lazima.

 

Anasema njia ya haja kubwa ya mwanaume, hutoka kinyesi  ambacho  kina vimelea vya hatari, vinavyoweza kusababisha uambukizi njia ya mkojo, kwa anaefanya au kusabisha bawasili, kwa anaefanyiwa. 

Kumbe kunaweza kusababisha saratani ya njia ya haja kubwa au matatizo ya muda mrefu ya kutokuwa na uwezo wa kuzuia haja kubwa, inapotokea

 Madhara mingine hasa kwa wanawake ni shida ya kujifungua, kwani pumzi (nguvu) za kusukuma mtoto zinakosekana.

 "Uimara wa njia ya haja kubwa, husaidia kuzuia pumzi ya uchungu na kusaidia njia ya uzazi ya kawaida, kufanya kazi yake ya kusukuma mtoto kwa urahisi,"anafafanua.

 

Mkuu wa vituo vinavyotoa huduma na tiba kwa watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI, kanda ya Pemba dokta Rahila Salim Omar, anasema kisayansi tendo la ndoa lina sehemu yake sahihi.

 Kuingiliwa kinyume na maumbile, mtu hubadilika uhalisia wake  na kupelekea kupoteza uimara na misuli kulegea, hatimae kuharibu sehemu za uzazi.

 

Fatma Said Mohamed ni daktari kutoka kitengo cha elimu ya uzazi hospitali ya Abdalla Mzee, anasema kitendo hicho kinasababisha njia ya haja kubwa kulegea.

Anaenda mbali zaidi kuwa, kila umri unaposonga, haja kubwa hutoka bila kizuizi, humsababishia aibu na kumshushia hadhi yake mbele ya jamii.

 

Afisa ustawi hospitali ya Abdalla Mzee Nasir Faki Juma, anatilia mkazo kuwa eneo linalofanyiwa tendo hilo asili yake haliruhusiki, kuingia kitu kutoka nje kwenda ndani.

  MTAZAMO WA JAMII UKOJE

Asha Bakar Juma wa Mkoani anasema, tabia hiyo iwe kwa mwanamke ama mwanamme haikubaliki katika jamii na huonekana hana utamaduni.

 

Siti Ali Hamad na Kombo Juma Ali wanasema, jamii humuangalia vibaya na kumuondolea hadhi mtu mwenye tabia ya kufanya tendo hilo kinyume na maumbile.

 

Asma Juma Hamad (sio  jina lake halisi) anasema baadhi ya wasichana hutumia njia hii ya kujamiana kama ni njia ya kulinda usichana  wao (bikira) au hata kukwepa ujauzito.

 

 "Kwa sasa jamii imeona tendo la kujamiana kinyume na maumbile ni jambo la kawaida, kwani  wapo  wanandoa wengi hufanya  tendo hili kwa  kuridhishana, hata kama wanajua ni kosa,''anasema. 

 SABABU YA MATENDO HAYO NI IPI?

 Ali Mbarouk Mratibu wa Tume ya UKIMWI Pemba anasema  zipo sababu za kimaumbile, kibaologia na za kishetani zinazosababisha  matendo ya kujamiana kinyume na maumbile.

 

Anasema sababu za kibaologia kwenye nasaba au maumbile ya kibauologia  na mchanganyiko  wa homoni na vinasaba, inawezekana kusababisha mtu kuwa na hisia au maumbile tofauti kidogo na jinsia yake.

 

Ingawa mienendo ya tabia za jimai inaeleza kwamba, hii haishawishi mtu kufanya tendo la kujamiana kinyume na maumbile.

 

Kwa sababu za mabadiliko ama  mchanganyiko wa chembe nasaba ( DNA na vichocheo vya homoni.

 

Aidha mwanamme anaweza kuwa na tabia za kike sauti, mwendo, ishara, tabia, hulka na hata maono ama mwanamke anaweza kuwa na mabadiliko, muonekano, sauti, tabia, ndevu, hulka na silka za kiume.

 

Hoja hizi zinapingwa ama kuungwa mkono na wanatabia (behaviorists) kwa kusema, tabia ya kufanya au kufanywa tendo la jimai kinyume na maumbile, ni tabia ya  mtu.

 

Na aidha ikiwezekana kuchochewa na homoni ama kuchochewa na tabia za kibinadamu za tamaa, ushawishi, wigo au hisia za kimwili.

 

 DINI INASEMAJE

Sheikh Said Abdalla Nassor kutoka Ofisi ya Mufti Pemba anasema suala la kufanya tendo kinyume na maumbile, kwa dini ya kiislamu halikubaliki.

 

Anafahamisha, kutokana na kukatazwa katika dini tendo hilo linachangia madhara makubwa, ikiwemo  kupata adhabu ya  Allah, kukosa barka, kuondoshewa nuru katika maisha ya duniani na ya akhera.

 

"Mtume Muhammad, amabe ni kiongozi wetu anasema analaaniwa anaemuendea mwanammke kinyume na maumbile na siku zake za afya,''anasema.

 

Mchungaji wa kanisa la 'TAG' Makangale na mwangalizi  kwa upande wa Pemba Samwel Elias Maganga, anasema kufanya tendo la kinyume na maumbile, halikubaliki.

 

Anaelezea bibilia kitabu cha walawi mlango wa 18 mstari wa 22 hadi 23 inasema 'usilale na mwanamme mfano wa kulala na mwanamke ni machukizo wala usilale na mnyama yoyote ili kujitia najisi kwake, wala mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kulala nae ni uchafu'.

 

Nyaraka na ripoti mbalimbali zenye uzito wa sharia na kidini ikiwemo ile ya Islam Q &A ,Islam web  zimeelezea wazi kwamba tendo la jimai kinyume na maumbile kuwa ni haramu.

 

Akitowa ushuhuda Fatma Kombo Juma (jina sio sahihi) baada ya mume kumuingilia kinyume na maumbile na hatimae kupata athari athari wakati wa kujifungua.

 

Mwingine ambae alikataa jina lakw kupishwa, aliyeolewa na kuishi na mume wake Dar-es Salaam amepoteza watoto wawili, kwa kukosa pumzi za kusukuma wakati wa kujifungua.

 

Mwenyekiti wa jumuiya ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi VVU ZAPHA+ Wilaya ya  Chakechake Maryam Said Abdalla  anasema, sio busara jamii kuendelea kufanya jambo linalowaletea madhara .

 


Anaitaka jamii kuacha tabia hiyo, kwani inawapa hitilafu katika mfumo mzima wa uzazi, huku akiwaambia wale ambao wameshakomaa na jambo hilo, wanaweza kupata ushauri wa taalamu na kucha kabisa.

 

Wanaharakati wa haki za binadamu, pamoja na  mashirika kama Human Rights Watch , Amnesty International , Human Dignity Trust  na LGBT Voice of Tanzania wanakataa kabisa  matumizi ya jimai isiyo ya kawaida.

Chama cha waaandishi wa habari Tanzania Zanzibar imekuwa mstari wa mbele  katika kutowa elimu  juu ya unyanyasaji  wa kijinsia, uzazi, mimba na matumizi ya vyombo vya habari kufikisha  ujumbe kwa umma.



Mkurugenzi wao dk. Mzuri Issa anasema chama hicho kimekuwa na ushawishi mkubwa katika  mawasiliano  ya kijamii  kuhusu afya , haki za wanawake  na ukatili wa kijinsia.

 

Mkakati wa wizara ya Afya ni pamoja na kutoa huduma  bora , salama na za heshima kwa watu wote  huku ikihakikisha  kuondoa ubaguzi, unyanyasaji  na ukandamizaji.

 

Huku malengo yakiwa ni kuboresha  upatikanaji  wa huduma za afya za uzazi ,akili kwa jamii ya LGBTQ kukuza elimu  na uelewa  wa haki za binadamu  miongoni mwa wafanayakazi  wa afya  na jamii .

 Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...