Skip to main content

TAMWA-ZANZIBAR: ''WANAWAKE JITOKEZENI 2025 MSIJALI VITISHO''

 

 

 

NA MARYAM NASSOR, ZANZIBAR @@@@

MKURUGENZI wa Chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, amewataka wanawake kujitokeza kwa wingi  kugombea nafasi mbali mbali za uongozi majimboni,  ili kuongeza ushiriki wao bila ya kuogopa vitisho.

Dk. Mzuri ameyasema hayo leo Oktoba 1, 2024 ukumbi wa mikutano wa chama hicho Tunguu Unguja, katika kikao cha kueleza namna gani  wanawake  watapata ulinzi dhidi ya ukatili wa kijinsia  mitandaoni, kupitia mradi wa wakuwawezesha waandishi wa habari vijana.

 

Amesema kuwa, hamu yao ni kuona wanawake wengi  wanaingia majimboni kugombea nafasi mbali mbali, lakini suala la udhalilishaji mitandaoni, linawarudisha nyuma.

“Jamii inaamii mtu akitaka kugombea nafasi ya uongozi ni lazima awe msafi kwa asilimia 100, lakini mwanamke ni binadamu na  hakosi mapungufu,’’alisema.

Amesema kuwa, moja kati ya kikwazo kikubwa kwa wanawake katika kugombea ni vitisho kutoka wagombea wanaume.



‘’Wanawake musiogope kujitokeza kugombea, kwani wamekuwa kidogo katika kugombea nafasi za uongozi, wakisumbuliwa na ukatili wa  wa kijinsia mitandaoni lakini musivunjike moyo,’’alifafanua.

Afisa kutoka Mamlaka ya kuzuia rushwa na uhuhumu wa uchumi Zanzibar ‘ZAECA’ Yussuf Juma Suleiman, amesema moja kati ya vikwanzo  vinavyowarudisha nyuma  wanawake katika kugombea nafasi za uongozi ni rushwa ya ngono.



Amesema kuwa, kabla wanawake hawajaingia katika kugombea nafasi za uongozi, ni vizuri kupewa elimu ya uraia, ili kujua miiko na misingi ya uongozi, ili wasiwe na mwanya wa kutoa rushwa.

Aidha amesema kuwa, serikali ya Mapinduzi Zanzibar imepitisha sheria mpya ya kuzuia rushwa na uhujumu wa uchumi, sheria namba 5 ya mwaka 2023, kifungu cha 53.

Amesema, kifungu hicho kimeharamisha rushwa ya ngono, kwa kukataza mtu yoyote kushawishi, kuahidi kufanya ngono na adhabu yake ni kifungo kisichopungua miaka saba na kisichozidi miaka 10.

“Rushwa ya ngono ni uhalifu kama ulivyo mwingine, na serikali imeazisha sheria ili kukabiliana nayo, lakini wandishi wa habari toeni elimu ili wanawake wanaotia nia wasiwe ni mwanya wa kutokea rushwa,’’ alisema.

Nae Afisa sheria Mwandamizi kutoka ofisi ya msajili wa vyama vya siasa, Abdul-razak Said Ali amesema   serikali imekuwa ikichukua jitihada mbali mbali, katika kumuwezesha mwanamke kugombania nafasi za uongozi ili kuongeza ushiriki wao.



Alisema kuwa, moja ya hatua iliyochukuliwa na serikali ni kuongeza kifungu katika sheria ya vyama vya siasa nambari 1 ya mwaka 2024, kifungu namba 10 (c) ndani ya marekebisho, kinatoa masharti yanayohusiana na uanzishwaji wa dawati la kijinsia na ushirikishwaji wa jinsia na jamii.

Na washiriki wa mkutano huo Mwalim Mwatima Issa, Rashid alisema wandishi wa habari wanatakiwa kujipa kipaumbele katika kufanya kazi zao.

Nae mshiriki Nusra Shabani aliuliza kwanini vyama vidogo vya siasa, havipewi ruzuku ili kuviwezesha vishiriki kikamilifu katika uchaguzi.

                Mwisho 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan