Skip to main content

WANANCHI WATAKIWA KUJIANDIKISHA DAFTARI LA WAPIGA KURA

 



IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA 

JAJI wa Rufaa mstaafu Mbarouk Salim Mbarouk amewataka wadau wa uchaguzi kuwahamasisha wananchi kujiandikisha kwa wingi kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ili wapate haki yao ya msingi ya kupiga kura ifikapo Oktoba mwaka 2025.

 

Akizungumza na wadau hao katika mkutano wa uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura lililofanyika katika Ukumbi wa Kiwanda cha Mafuta ya Makonyo Wawi Chake Chake, Jaji huyo alisema, kila mmoja alifikia vigezo ana haki ya kushiriki zoezi hilo.

 

Alisema kuwa, ipo haja kwa wadau hao kila mmoja kwa nafasi yake ahakikishe anawahamasisha wananchi waliokaribu yake kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura, ili kumuwezesha kupiga kura katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.

 

"Tume inathamini sana mchango wenu na ndio maana imewaita hapa kushirikiana na nyinyi, kujadili namna ya kuifikia jamii kwenda kuwaelimisha na kuwahamasisha ili wasikose haki yao ya kujiandikisha katika daftari hili la wapiga kura," alisema Jaji huyo mstaafu.

 


Aidha alieleza kuwa, nchi ipo katika maandalizi ya uchaguzi na imetoa mamlaka kwa Tume ya uchaguzi kutekeleza majukumu ya kusimamia na kuratibu shughuli mbali mbali kwa mujibu wa Sheria ya uchaguzi ilivyoelekeza na ndio maana imeanza na zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura.

 

Akiwasilisha mada ya Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC Giveness Awile alisema, viongozi wa vyama vya siasa hawapaswi kuingilia utekelezezaji wa majukumu ya watendaji wa vituo wakati wote wa uandikishaji wa daftari la wapiga kura vituoni.

 

Aidha alisema kuwa, wanatoa mafunzo ya kuwajengea uwezo watendaji wote watakaoboresha zoezi hilo la uandikishaji, ili wafanye kazi kwa ufanisi na utaalamu zaidi.

 

"Tunatarajia kuwa na wapiga kura 5,586,433 sawa na asilimia 18 ya wapiga kura 29,754,699 waliopo kwenye daftari kwa sasa, mwaka 2019/2020, ambapo kwa sasa Pemba tuna vituo vya kupiga kura 140 kati ya 135 vya zamani," alieleza Kaimu huyo.

 


Alisema kuwa, Tume ya Uchaguzi imeongeza upeo mpana kwa kumeongeza vituo vya kupiga kura kwa wananchi walipo kwenye vyuo vya mafunzo, ili na wao wapate haki yao kupiga kura kwa kila aliekidhi vigezo vinavyokubalika kisheria.

 

Nae mwasilishaji Martine Mnyenyelwa alisema kuwa, vifaa mbali mbali vitakavyotumika katika zoezi hilo vitaboreshwa kwa ajili ya ufanisi zaidi katika kazi.

 

Akifunga mkutano huo Balozi Omar Ramadhan Mapuri aliwasisitiza wadau hao kuwa, kila mmoja atumie nafasi yake kuelimisha ili wananchi washiriki kikamilifu katika zoezi hilo.

 


Balozi huyo pia aliwataka wadau wa Uchaguzi kuzingatia katiba, Sheria na kanuni katika zoezi hilo.

 

                          MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan