Skip to main content

SKULI YA SEKONDARI CONECTING CONTINENT, ZAO LA MWEKEZAJI LINALOWANYIWA NA WAZALENDO

 

     



NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@

SKULI ya sekondari ya Connecting Continent iliyopo nje kidogo ya mji wa Chake chake, ni miongoni mwa skuli 10 binfsi zilizopo kisiwani Pemba.

Skuli hiyo ipo nje kidogo ya mji wa Chake Chake, imekuwa ikiwavutia zaidi na wanafunzi wasichana kutokana na upasishaji wake mzuri wa kila mwaka.

Conecting ni miongoni mwa skuli 10 binafsi kisiwani Pemba, zilizobahatika kuruhusiwa kuwekeza katika elimu kwa ngazi ya sekondari.

Skuli hiyo ilianzishwa mwaka 2006 ikimilikiwa na wawekezaji wajerumani, ikiendeshwa na michango midogo midogo ya wafadhili wenyewe na ada nyepesi zinatolewa na wazazi na walezi.

 


 

Skuli hiyo ilianza kufanya mitihani ya taifa mwaka 2008, na kufika mwaka 2022, wanafunzi 671 walihitimu.  

Kati ya wanafunzi hao wanawake walikuwa 332 na wanaume walikuwa 339 kwa wakati huo, wakitokea skuli mbali mbali za msingi kisiwani Pemba.

Mwandishi wa makala hii hakutaka hadithi za mdomo alitaka kujua kinaga ubaga historia japo fupi ya skuli hio hadi ilipofika.

Mwalimu mkuu skulini hapo mwana mama Mwache Juma Abdalla, anasema kuwa mwaka 2020 wanafunzi 58 walifanya mtihani wa taifa kidato cha nne, 24 wanawake na 34 wanaume,mwaka 2021, 43 wanaume 17 wanawake 26, mwaka 2022, 83 wanaume 28 na wanawake 55.

Mwaache anaeleza kutokana na ufaulu kupanda mwaka hadi mwaka ni uthibitisho tosha kuwa, skuli hiyo, jambo ambalo litaweza kufikia malengo waliyojipangia.

Anaeleza kuwa, idadi kubwa ya wanafunzi wanaofaulu ni wanawake, na ndio maana kila mwaka wanapokea zaidi wanafunzi wa jinsi hiyo.

Anaona Serikali ya Mapinduzi inafanya jitihada mbali mbali kuhakikisha kila mtoto, anapata haki ya msingi ikiwemo elimu.

Kutokana na umuhimu huo, ndipo Serikali ikaruhusu mashirika na taasisi mbali mbali hata kutoka nje kuwekeza tasnia hiyo nchini, kwa maendeleo zaidi.

Hatuwa hiyo ni pamoja na kuanzisha skuli za maadalizi, msingi na Sekondari kwa kufuata misingi na kanuni zilizowekwa.



LENGO LA WAMILIKI KUANZISHA SKULI HIYO

Moja ni kuwasaidia wananachi wa Zanzibar, kupata skuli bora itakayoinua maisha yao kwa maendeleo, na kupata elimu yenye kiwango.

Anafahamisha kuwa, skuli hiyo inachukuwa wanafunzi wa kawaida na wenye mahitaji maalum, ili makusudi lengo liweze kufikiwa.

Lengo ni kuona kila mmoja, anapata haki hiyo ya elimu sawa kama wanavyopata wengine katika jamii mbali mbali.

Akielezea suala la kupokea wananfunzi kwanza zipo taratibu mbali mbali hufanyika ikiwemo usaili utakaoleta majibu mazuri.

‘’Tunafanya mitihani mara mbili kwa kipimo zaidi na ili mwanafunzi turidhike nae na kuendelea na darasa la tisa nilazima afikie daraja C, bila hapo skuli haichukui kwani itakua ni mzigo bila matunda,’’anasema Mwalimu huyo Mkuu.

Akigusia mafanikio, anasema ni mengi na makubwa, ikiwemo kupasisha wanafunzi katika kiwango cha juu kila mwaka, kuengezeka kwa madarasa kutoa vyumba vinne (4) na kufikia 10, maabara tatu (3) na maktaba.

WANAFUNZI WA SASA

Fatma Mohamed Bakar anaesoma kidato cha tatu mwenye ulemavu wa viungo, anaeleza sababu zilizomfanya kujiunga skulini hapo, ni pamoja na kiwango kizuri cha ufaulu hasa wanawake.

‘’Waalimu wa skuli hii wanakua na juhudi binafsi katika ufundishi, ambao unatufanya kila mmoja kufahamu na kisha kufaulu,’’anasema.

Husna Mohamed Haji anaeleza amejiunga katika kituo hicho mwaka 2021, akiwa darasa la tisa baada ya kupasi michepuo katika skuli ya Pindua.

Anaeleza kuwa licha ya kuwa na upungufu wa usikivu haikuwa changamoto kwake, kutoendelea na masomo katika skuli hiyo kubwa.

“Nashukuru kwa kuwapa moyo wa imani wazazi, walimu wangu pamoja na wanafunzi wenzangu na jamii iliyonizunguka hadi nilipofika,’’anasema.    

 ‘’Walimu wanaposomesha hutoa sauti ili niweze kusikia na kufahamu vizuri kinachosomeshwa na kisha hufanya vizuri kuanzia mitihani ya ndani hadi taifa,” anaeleza.

Kwa upande wa malengo yake ya baadae Husna anasema ni mengi moja ni kuhakikisha anasoma kwa bidi hasa masomo ya sayansi ili kufikia ndoto zake yakuwa ijinia.

‘’Lengo langu nikuhakikisha najikita zaidi kusoma masomo  ya sayansi ikiwemo physics,Chemistry na hesabati,(PCM)ili niwe injinia,” alieleza.  

KWA UPANDE WA MATOKEO KWA MWAKA

Mwaka 2022 katika ufaulu wa wananfuzni walipata daraja la tatu, nne, lakini miaka ya karibuni kiwango cha ufaulu kilipanda.

Mwalimu huyo anaeleza kuwa, hiyo ni kutokana na ushirikiano kati ya walimu, wazazi na wanafunzi wenyewe, kuhakikisha wanatoka walipokuwa na kufika pale wanapotaka kimaendeleo.

Anaeleza kuwa mashirikiano hayo ndio njia pekee iliyopelekea kuondosha daraja la nne na zero, na kupata daraja la kwanza, la pili na tatu tu.  

Ambapo kwa mwaka 2022 skuli ilifanikiwa kupasisha kwa kiwango cha daraja kwanza wanafunzi 4, daraja la pili wanafunzi 43, la tatu wanafunzi 30, na daraja la nne walikuwa wanafunzi wawili (2).

Hivyo matokeo hayo ni ushahidi tosha kwamba skuli hiyo inatoa matokeo mazuri zaidi kuliko skuli nyengine za binfsi zilizopo Kisiwani humu, ni takribani miaka 8 sasa hakuna zero.

MASHIRIKIANO NA SERIKALI.

Mwalimu huyo anasema mashirikiano baina yao na Wizara ya elimu ni mazuri, na ndio maana wakaweza kufikia hapo walipo sasa.

‘’Bila mashirikiano na Wizara tusingalifika hapa tulipofika kimaendeleo, kwani kila jambo linahitaji mashirikiano.

                 CHANGAMOTO

Alisema kuwa nikukosa dahalia la uhakika kwa watoto wanafunzi, kwani sehemu wanalala ni nyumba za watu binafsi.

‘’Zipo yumba za watu binafsi wazazi ndio wanatoa fedha zao kwa ajili yakulipia kodi na chakula, jambo ambalo linawapa mashaka, kwa kuwepo uangalizi mdogo hasa kwa wanaume.

Akizungumzia suala la kodi kwa Mamlaka ya Mapato Zanzibar ZRA, ameomba wafanyiwe msamaha kwani kituo hicho hakipo kibiashara kipo kusaidia jamii zaidi kupata elimu.

‘’Kwa mfano hapa wapo wanafunzi 300, lakini wapo waliofiliwa na mzazi, wenye mazingira magumu na wenye kipato duni hawalipi ada,’’anasema.

Hivyo mamlaka hiyo ni vyema kumuunga mkono mfadhili  huyo, kwani lengo ni kusaidia watoto hasa mayatima na wenye hali ngumu na sio kibiashara.



     WALIOWAHI KUSOMA

Juma Kitwana Bilali anaeleza kuwa, Connecting ni miongoni mwa skuli binafsi yenye kiwango kizuri cha kupasisha hasa watoto wa kike.

‘’Mimi nimesoma connecting na kwa sasa nasomesha wenzagu katika kituo hichi,” anaeleza.

Hivyo kuwataka wazazi na walezi kuendeleza mashirikiano kwa walimu, ili wapate kuboresha taaluma hiyo kimaendeleo.

Mwanafunzi Omar Ali Juma, anasema ameshawahi kuwa baharia katika meli za nje, baada ya kumaliza elimu yake ya sekondari skuli hapo.

MALENGO YA SKULI BAADAE

Mwalimu huyo anasema ni kufika mbali zaidi kielimu, kutoka walipo kimatokeo, na pia kuwa na wanafunzi hadi wa kidato cha sita.  

Akizungumzia suala la upasishaji anasema kuwa wanaka kuwa na kiwango cha daraja daraja la kwanza, na pili tu sio tatu, nne wala zero.

Skuli ya Conecting Continent Organization iliyopo Mgogoni Wilaya ya Chake Chake imeanzishwa mwaka 2006, ikiwa na wanafunzi 18 tu wa darasa wa tisa.

Ambapo kwa sasa wapo na wanafunzi wakidato cha nne 58, wakiwemo wakike 29 na wakiume 29, wanaotarajiwa kufanya mitihani yao ya taifa kwa mwaka 2023.

Mwenyekiti wa bodi ya wazazi skulini hapo Said Mohamed Ali anasema kuwa skuli ipo vizuri kiutendaji kwani kimatokeo takribani miaka 8 sasa hawajawahi kufelisha.

Anachojivunia Mwenyekiti huyo ni umoja, mshikamano uliopo baina ya waalimu, wazazi na Bodi ya wazazi skuli hapo.

 

Afisa Mkurugenzi wa mamlaka ya mapato ZRA Pemba Jamal Hassan Jamal, amewataka watendaji wa skuli hiyo kujisajili na kulipa kodi ili kuondosha changamoto zisizokuwa za lazima.

Anaeleza kuwa Serikali haina nia ya kumkwaza mtu bali ipo kusaidia wananchi wake, hivyo kuwataka kujisajili mamlaka kwa mujibu wa kipato chao.

“Ipo sheria namba 7 ya mwaka 2009 inasema yoyote anayeanzisha biashara kwa ajili yakujipatia kipato, lazima kuomba usajili mamlaka ya mapato Zanzibar.

Aidha kuwataka kufuata sheria kuomba usajili ZRA, ili kuepusha kwa ujenzi wa taifa.

                        MWISHO.    

 

 

 

 

 

 

 

                                                            

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch