Skip to main content

MTAMBWE KUSINI MAJI 'BWERERE', ZAWA YASEMA JAMBO

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI wa shehia ya Mtambwe kusini wilaya ya Wete Pemba, wamesema kwa sasa huduma ya maji safi na salama katika vijij vyao, inapatikana kwa urahisi, tofauti na hapo zamani.

Walisema, kwa sasa wamekuwa na wakati mzuri wa kujipangia shughuli zao mbali mbali za kimaisha, na wala upatikanaji wa huduma hiyo, sio changamoto inayowatengulia rataiba zao za kimaisha.

Wakizungumza na waandishi wa habari waliofika kijijini hapo, walisema kwa sasa huduma hiyo, iko karibu vijiji vyote, tena bila ya mgao, jambo ambalo limechangia kufikia malengo yao.

Walieleza kuwa, upatikanaji wa huduma hiyo kwa miaka minne mfululizo sasa, unawapa uhakika wa maisha yao, hasa kwa vile kila mmoja, anaendesha shughuli zake kwa urahisi.

Salma Hamad mkaazi wa kijiji cha Kivumoni, alisema kwa sasa huduma hiyo iko vyema na haina shida kwao, ikilinganisha na miaka 20 iliyopita.

‘’Awali sisi wananchi wa kikijiji cha Kivumoni shehia ya Mtambwe kusini, tukifuata maji masafa ya mbali, ingawa kwa sasa tunaishukuru serikali,’’alieleza.

Nao mwananchi Mafunda Abdalla Omar na Neema Abdalla Omar wakaazi wa kijiji cha Mkanjuni shehiani humo, walisema kilichobakia kwao, ni kuyatunza miundombini ya maji safi salama iliyopo.

Mwananchi Jabiri Saleh Jabir (65) alisema awali aliwahi kutoka nywele kichwani, kutokana na ubebaji wa maji wa masafa marefu, ingawa kwa sasa, huduma hiyo imewafuata kwenye makaazi yao.

‘’Zamani ilikuwa ni kazi kubwa kupata huduma ya maji safi na salama, inabidi uende mabondeni kufuata huduma hiyo, tena maji hayakuwa safi na salama kama haya ya sasa,’’anaelezea.

Sheha wa shehia ya Mtambwe kusini Othman Ali Khamis, aliwataka wananchi, kuhakikisha wanaendelea kuchangia huduma ya maji safi na salama, ili huduma hiyo iwe endelevu.

Alieleza kuwa, ndani ya shehia hiyo ipo mifereji 42 ya nje, ambayo wananchi wanaweza kupata huduma saa 24, na wakati wowote.

‘’Wapo wananchi walioamua kuvuta huduma hiyo ndani, lakini kwa wasiokuwa na uwezo, serikali imeamua kuweka mifereji nje, ili iwarahisishie kupata huduma hiyo,’’alieleza.

Sheha huyo alisema, kwa sasa huduma hiyo, inapatikana saa 24, na ikitokezea kukosekana, iwe hakuna hduma ya umeme, au kuharibika mashine.



Aidha sheha huyo amewakumbusha wananchi kuendelea kutunza mazingira, na hasa kuacha ukataji wa miti ovyo, karibu na vyanzio vya maji.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Maji Zanzibar ‘ZAWA’ Ofisi ya Pemba, Suleiman Anas Massoud, alisema huduma kwenye shehia hiyo imeimarika, baada ya kushirikiana kwa karibu na tasisi ya Zanzibar Milele Foundention na mfuko wa Mwakilishi wa Jimbo la Mtambwe.

Alisema, kisima kilichopo Daya Mtambwe, kinauwezo wa kuzalisha kati ya lita 55,000 hadi 60,000 kwa saa, ambapo yanakwenda samba mba mahitaji na matumizi.

Hata hivyo amewakumbusha wananchi wa shehia hiyo, kuendelea kuchangia huduma ya maji safi na salama, ili iwe rahisi inapotokezea hitilafu.

‘’shehia za Mtambwe kusini na Kaskazini kuna mradi maalum na sasa wanakusanya takwimu ili kuimarishiwa hudum na hasa kwa vile sasa idadi ya watu imeongezeka,’’aliongeza.

Wananchi 4,733 wakiwemo wanawake 2,323 na wanaume 4,210 wa vijiji vya Makoongweni, Kivumoni, Mkanjuni, Kinazini, Kokota shehia ya Mtambwe kusini wilaya ya Wete, wanavitegemea visima viwili vilivyopo Daya, Mkanjuni na kile cha Kinazini kikiwa kimeharibika mashine yake.

                   Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch