Skip to main content

SASA ARDHI YA ZANZIBAR KUSAJILIWA KWENYE MFUMO MAALUM

 


 

Na Mwandishi wetu, Zanzibar

Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi (WAMM) jana imesaini Hati ya Makubaliano na Kampuni ya Kitaifa ya Kijiografia na Misitu (IGN FI) ya Ufaransa kuhusu Mradi wa Taarifa za Usimamizi na Usaji wa Ardhi Zanzibar.

Akizungumza mara baada ya hafla ya utiaji saini waziri dhamana wa wizara hiyo  Mhe. Rahma Kassim Ali amesema kufanya kazi kwa mfumo wa taarifa za Usimamizi na Usajili wa Ardhi utasaidia kwa kiasi kuondosha migogoro ya ardhi iliyokuwepo Zanzibar.

Waziri Rahma aliyasema hayo baada ya kushuhudia hafla ya utiaji saini ambapo ilifanyika Wizara Ardhi na Maendeleo ya Makaazi, Maisara Unguja. Alisema hatua hiyo ya utiaji saini ina manufaa makubwa hasa katika kuondoa migogoro ya ardhi ambayo inaonekana kujitokeza kila siku.

 “Tunaamini mfumo huo utasaidia sana kwani taarifa zitakuwa kwenye mfumo na mmiliki husika hasa wa ardhi atajulikana kwani taarifa za ardhi  zipo kwenye karatasi lakini mfumo sio rahisi kupoteza taarifa.” Alisema waziri huyo.

Waziri Rahma alisema hivi sasa wizara yake inaendelea na zoezi la utambuzi wa ardhi ambapo pia taarifa zake zitaingizwa katika mfumo na tayari wamefanya zoezi la utambuzi katika shehia 50 zimeshafanyiwa kazi na mategemeo ya Serikali ni kuitambua ardhi yote katika shehia 388 za Unguja na Pemba.

“Mfumo huu tuna matumaini makubwa kwamba migogoro ya ardhi mingi itaondoka na itakayokuwepo ni ile ya kawaida lile tatizo kubwa ambalo linatukumba wizara litaondoka kwa asilimia 95 na itakuwa manufaa makubwa ambayo Serikali ya awamu ya nane imepiga hatua kubwa.” Alifafanua Waziri Rahma.    



Hivyo alisema anaamini ndani ya mwezi mmoja upembuzi yakinifu wa mfumo huo utakuwa umeshakamilika na kwenda kwenye mfumo wenyewe hivyo ni matumaini yake ndani ya mwaka huu kabla ya 2024 mfumo huo utakamilika na kuanza kutumiwa rasmi.

Kwa upande wake  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mhandisi Dk. Mngereza Mzee Miraji, alisema mfumo huo utakapoanza kazi utakuwa na faida kubwa ikiwemo ya kuongeza usalama wa umiliki wa ardhi kwa wawekezaji na wananchi, kupunguza urasimu na kutoa huduma rahisi ya kuaminika na salama kwa wateja kwani wananchi na wawekezaji wamekuwa wakitoa malalamiko katika jambo hilo. 

Alisema pia utapunguza muda wa kukagua, kusahihisha na kubadilisha ama kuhamisha umiliki wa ardhi kwa wananchi wawekezaji na miradi yote inayofanyika Zanzibar, kupunguza uvamizi wa ardhi, misitu, hifadhi za barabara na sehemu za wazi, uhifadhi wa ardhi na maliasili na kupunguza rushwa na viashiria vyote vya rushwa hasa ya ufatiliaji, usajili na uhamisho wa hatimiliki.

Mhandisi Dkt. Mngereza alibainisha kuwa utiaji saini huo ni mwanzo mpya ya kimapinduzi katika sekta ya ardhi nchini ambalo ndio lengo la Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi kuondoa urasimu na kuondoa migogoro ya ardhi hapa Zanzibar hivyo matumizi ya teknologia mpya ni njia moja ya kutatua changamoto zilizokuwepo katika suala la ardhi Zanzibar.

Mapema Mrajis wa Ardhi Dkt. Abdul-Nasser Hikmany alisema mfumo huo utasaidia kiutendaji pamoja na kutoa huduma bora kwa jamii kupitia Kamisheni ya Ardhi Zanzibar ambapo taasisi hiyo iko chini ya Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar.

Dkt Hikmany alisema malengo ya taasisi hiyo  kuwa taarifa zote ambazo zitahusu ardhi zitaingizwa katika mfumo huo ikiwemo utambuzi, mipango miji, usajili na mambo mengine ikiwemo maombi ya umiliki wa ardhi.

Alielezea kwamba mfumo huo sio mpya duniani  kwani umeshatumika katika nchi nyengine ikiwemo Uganda, Seralione na hata Tanzania bara ambao ufanya kazi kwa muda wa miaka mitano.




“Leo tumetia saini Hati ya Makubaliano kwa ajili ya kutekeleza upembuzi yakinifu ambayo itatuonesha gharama ya mfumo huu na utatengenezwa kwa jinsi ya mazingira ya Zanzibar yalivyo.” Alisema Dkt. Hikmany.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kitaifa ya Kijografia na Misitu (IGN FI) ya Ufaransa Christopher Dekeyne, alipongeza Serikali kufanya kazi pamoja na Taasisi yake kwani na wana uzoefu mkubwa katika mabara mengi hasa ya Afrika  wamefanikiwa na mradi huo na umeleta manufaa. Hivyo anaamini kwamba mfumo huo utaleta tija Zanzibar.

Alisema kazi hiyo itaanza kwa kufanya upembuzi yakinifu kujua mazingira ya Zanzibar na vitu vitakavyohitajika ili kuwa na mradi utakaokidhi haja na mahitaji ya Zanzibar na kuwezesha kutengeneza mfumo ambao utaanza kutekelezwa mwishoni mwa mwaka huu kwa ajili ya kuinua uchumi wa Zanzibar.

Aidha alisema ni matumaini yake kwamba watapata ushirikiano wa kutosha ili kuweza kufanikisha mradi huo na kufanya kazi kwa viwango vinavyotakiwa.

Mwisho.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch