Skip to main content

WANANCHI MSUKA PEMBA UZALENDO UMEWASHINDA, WATAKA UJENZI WA BARABARA YAO KWA KIWANGO CHA LAMI

 

     



HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@

“HATUWEZI kwenda na kasi ya maendeleo, kwetu kutokana na uchakabu wa barabara,’’wanasema wananchi na watumiaji wa barabara ya Konde- Msuka.

Wakaongeza kuwa, hata gari ya abiria hawana, shida kubwa hasa wanapotaka kwenda mjini kwa ajili ya kufuata matibabu.

Wakizungumza na mwandishi wa makala haya, wananchi wa kijiji cha Msuka wilaya ya Micheweni mkoa wa kaskazini Pemba, wanasema hawajui ni lini watajengewa barabara hiyo.

Kwa kuwa barabara huchangia pato kubwa katika maendeleo ya mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla, ndio maana wananchi hawa sasa wanataka kujengwa barabara ya kudumu.

Kuna shughuli nyingi ambazo bila ya kuwepo miundombinu ya barabara haziwezi kufanyika ama kufanyika kwa wakati wake.

Ingawa umuhimu wa barabara hauonekani kwa ghafla mpaka pale panapotokezea tatizo, ikiwemo wafanyabiashara, wanapotaka kuingiza ama kutoa bidhaa zao mbalimbali.

Akina mama wanapotaka kufuatia huduma za afya katika hospitali kubwa ama za rufaa hakuna mafanikio bila ya kuwepo kwa barabara.

WANANCHI WANASEMAJE

Halima Khamis Abdalla (50) anasema tokea azaliwe, barabara yao hiyo imekuwa ikipokea ahadi, na hadi sasa haijajengwa na wanaendelea kupata usumbufu.

‘’Kwa ahadi za kujengwa kwa barabara yetu hii, zimeshatolewa zaidi ya 20, lakini mimi sasa natimizi miaka 50, bado huna utekelezaji,’’anasema.

Anasema barabara hiyo yenye mashimo makubwa na mchanga mwingi kwa baadhi ya maeneo hata wakiwaita wenye gari wanapofikwa na tatizo kama la kuhitaji kufika hospitali au safari ya haraka hawataki.

Wengi wa wenye agari huhofia kupata hasara badala ya faida, kutokana na uchakavu wa miundombini ya bara bara hiyo, kw amuda mrefu sasa.

“kila siku tunaambiwa barabara iko kwenye bajeti, lakini hatuoni maendeleo yoyote nasi tunatamani kuwa nayo kama wenzetu wa maeneo mengine”, anasema.

Rufea Mohamed Seif anasema wenye kupata tabu zaidi ni wanawake hasa pale wanapofuatia huduma mbalimbali za kijamii huko mtaa wa Konde na Micheweni.

Anaona sio ajabu kwa akinamama wa Msuka kujifungulia njiani wakiwa ndani ya magari ya Ng’ombe, kwani hawana gari kutokana na uchakavu wa barabara yao.

Akitowa ushuhuda wa mtoto wake baada ya kujifunguwa njiani Maryam Adam Juma, anasema baada ya kukosa usafiri wa gari ilibidi mwanawe aingizwe kwenye gari ya Ng’ombe na hatimae kujifungua kabla ya kufika hospitali.

Kwake hali hiyo hujitokeza pale wenye gari zao kukataa kuwapeleka huku wakidai kuwa, mara wanaporudi hulazimika kwenda kwa mafundi kutengeneza.

"Kwa kusema kweli ni mateso makubwa, maana sisi huku ni watu tunaishi tu ila kwa upande wa barabara, hatujanufaika nayo", anaeleza.

Hapa akasema, lazima mamleka zijue kuwa, inapokosekana barabara ya kisasa katika kijiji, waathirika wakubwa ni wanawake na watoto na sio wengine woowte.

‘’Mwanamke ndio mzazi, ndio mlezi, ndio anayefuatilia huduma za kijamii kutoka kijijini hadi mjini, sasa barabara ikiwa chakavu waathirika ni sisi,’’anasema.




 Ali Juma Mohamed anasema wamechoka kupigwa dana dana kila siku huambiwa barabara hiyo iko katika mpango wa  kutatengenezewa, lakini hawauoni.

Anasema huwa na woga sana wake zao wanapotaka kujifunguwa, kwani hulazimika kuwaingiza kwenye gari za Ng’ombe kuburuzana na wakati mwengine huzaa njiani.

“Tunaiomba serikali nasi ituone, kwa uhakika tunateseka wananchi wa Msuka hasa ukizingatia barabara, ndio kila kitu katika kujiendeleza kiuchumi”, anasema.

Akasema huduma za kijamii, haziwezi kutimia vyema kama miundombinu ya barabara iko chakavu, kwani ndio kichecheo kikubwa cha kusukuma mbele maisha.

Bimkubwa Salim Fadhil anasema roho ina choyo na wao hadi sasa wanapoona maeneo ya wenzao wamefikiwa na huduma ya barabara hutamani nao siku na moja waweze kupata huduma hiyo.

“Yote hayo nasi kama wananchi tunaopata shida hiyo ya barabara lazima tuone wivu na tutamani siku moja tuone tunapita katika barabara safi kabisa. 

WAFANYABIASHARA WANASEMAJE

Salim Makame mfanyabiashara ya samaki kutoka Chake chake anasema tatizo kubwa linalowarejesha nyuma, ni uchakavu wa miundombinu ya barabara, kwani huwawia vigumu kutoka Konde hadi bandari ya Msuka na kurudi.

 Kwa sababu ya ubovu wa barabara hiyo yenye mashimo na mchanga mwingi, kwa muda mwingi hughairi kwenda kununuwa samaki, katika badari hiyo kwani vyombo vyao vya usafiri wanaporudi huharibika.

“Mimi naamini wafanyabiashara tunapokuja kwa wingi katika badari ya Msuka na tukanunuwa bidhaa maendeleo zaidi wanayapata wananchi wenyewe,’’anafafanua.





Juma Ali Kombo mfanyabiashara wa vyakula, anasema itakapotengenezwa barabara ya Konde -Msuka wataweza kufanya biashara zao bila ya shida.

Kwa sasa wanalazimika kupata hasara, kwani hiyo gari inayowapelekea bidhaa zao, lazima wapandishe bei kutokana na uchakavu wa barabara.

VIONGOZI WA SERIKALI

Sheha wa shehia ya Msuka Magharibi Amina Khatib Ali, anasema miongoni mwa hatuwa, waliyoichukuwa ni kupeleka taarifa hizo katika Ofisini ya mkuu wa wilaya kwa hatuwa za mbele.

"Kwa kweli barabara yetu ya Konde- Msuka ni mbovu na hakuna linaloendelea la kimaendeleo bila ya barabara,’’ alisema.

Mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya, anasema barabara hiyo imo kwenye mpango wa barabara za wilaya zitakazojengwa.

Anasema anafahamu kuwa wananchi wa Msuka, wana kiu ya maendeleo lakini wavute subra, hadi pale muda utakapofika wa utengenezaji wa barabara katika wilaya yao.

“Naelewa wananchi wanakiu ya maendeleo, lakini nawaomba muwe wastahamilivu bara bara yenu, imo katika mpango wa kutengenezwa, ili na nyinyi muweze kufaidika “, alisema.

Afisa Mdhamini wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Pemba Ibrahim Saleh Juma anasema kwa upande wa Pemba barabara za ndani ambazo ziko katika mpango wa ujenzi ni kilomita 134.95 ikiwemo ya Msuka yenye kilomita 4.1.

Ambapo kwa ujumla katika  wilaya ya Micheweni zipo jumla ya barabara sita zinazojumuisha kilomita 47.4 na zimo katika mpango wa ujenzi kwa kiwango cha lami kwa mwaka huu.

Kwa upande wa wilaya ya Mkoani zipo barabara sita zinazojumuisha kilomita 24.1 ikiwemo ya Mbuguwani tironi yenye kilomita 3, Kengeja- Shamiani– Kiimbini yenye kilomita 4.4.

Mdhamini anabainisha kuwa hata wilaya ya Chake chake kuna jumla ya kilomita saba za barabara za ndani ikiwemo ya Wesha Mkumbuu yenye urefu wa kilomita 10 pamoja na Chanjamjawiri –Pujini yenye urefu wa kilomita 4.3. zinazojumuisha kilomita 29.5.

“Wizara pia ina dhamiria ya kuzijenga barabara 11 zenye urefu wa kilomita 33.95 kwa wilaya ya Wete ikiwemo ya Kiungoni – Tovuni yenye urefu wa kilomita 1.5, Mkarafuu mmoja –jumapili kilomita 5.15, Bagamoyo –Kele kilomita 6.5.

Akisoma bajeti kuu ya wizara hiyo ya mwaka wa fedha 2022/2023 waziri wa wizara hiyo Dk. Khalid Salum Mohamed amesema wizara imepanga kujenga barabara za ndani zenye urefu wa kilomita 275.9 Unguja na Pemba, ili kuwaondoshea wananchi changamoto ya usafiri iliyopo hivi sasa katika maeneo mbalimbali ya mjini na vijijini.

Mradi huo unatekelezwa na Kampuni ya ASER na IRIS kutoka nchini Uturuki na tayari wizara imekamilisha maandalizi ya ujenzi wa barabara hizo na kazi inayoendelea ni kuzifanyia usanifu wa michoro barabara zilizopendekezwa katika mradi huo.

Kwa mujibu wa waziri huyo kazi ya usanifu wa michoro imekamilika kwa barabara ya Kibonde Mzungu– 18 Mwera kilomita 6.1, Dimani Sokoni – Dimani Beach kilomita 1.5, Kombeni – Nyamanzi kilomita 1, Jumbi – Chuo cha Utumishi (IPA) – Tunguu (Ringroad) kilomita 5, Kidimni – Ubago kilomita 4.3, Jumbi Sokoni – Kibondeni Skuli - Hospitali kilomita 4.4, Mgeni Haji – Kwambani kilomita 2.4 pamoja na barabara ya Cheju – Kibele kilomita 4.1.

 Aidha, Barabara ya majaribio kutoka Kibonde Mzungu hadi Mwera yenye urefu wa kilomita 6.1 tayari ujenzi wake umeanza, hadi kufikia Machi, 2022 jumla ya shilingi 18,536,160,000 zimepatikana ikiwa ni malipo ya awali Advance payment ya Mkandarasi kwa mujibu wa mkataba.

                             Mwisho.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch