Skip to main content

DK: MNGEREZA AWAAINISHA WADAU WALIOFANIKISHA MPANGO UWEKEZAJI MAJI ZANZIBAR


 




Na Muandishi wetu Zanzibar@@@@

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi (WAMM) Mhandisi Dkt

Mngereza Mzee Miraji amesema Mpango wa Uwekezaji katika Sekta ya Maji Zanzibar

2022-2027 wenye lengo la kuimarisha sekta ya maji na kumaliza tatizo la maji safi na

salama Zanzibar alianzisha kwa kushirikiana na Wadau wa Maendeleo mbali mbali.

Mhandisi Dkt Mngereza aliyasema hayo jana katika hafla iliyoandaliwa ya

kumkabidhiwa Tuzo ya Kifahari ya VIP Global Water Change Maker, Mhe Rais wa

Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Husseini Mwinyi iliyofanyika jana

Ikulu Zanzibar.

Alisema katika kipindi ulichoteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Nishati na

Madini alichukuwa juhudi mbali mbali za kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya

maji safi na salama, kwa kukutana na Mashirika ya Kimataifa ya Misaada ikiwemo

JICA, USAID, BPI, Banks ikiwemo AFDB, wawakilishi wa balozi mbalimbali ikiwemo

UK, EU, JAPAN n.k.

Alielezea kwamba hivyo Wizara ya Maji, Nishati na Madini (WMNM) na Taasisi ya

Ushirika wa Wadau wa Maji (GWP ) walishirikiana kuandaa mpango huo uliojumuisha

wataalam wa fani mbalimbali kutoka Zanzibar, Serikali ya Jamhuri ya Tanzania (SMT),

South Afrika na Ethiopia chini ya ufadhili wa GWP ambapo mshauri elekezi wa kikosi

alikuwa Dkt Victor Kongo.



Aliesema kuzinduliwa kwa Mpango huo pamoja na kuutangaza kwa kufanya

Makongamano na Warsha mbali mbali kulipelekea Washirika wa Maendeleo kujitokeza

na kuonesha nia ya kuunga mkono Serikali Zanzibar katika kutatua changamoto ya

upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama.

Mhandishi Dkt Mngereza alisema Miongoni mwa Washirika wa Maendeleo walijitokeza

ni pamoja na KFW na GIZ za Ujerumani, Ruden Institute ya Norway, UNESCO-IHI Delft

ya Uholanzi, JICA ya Japani na Benki ya EXIM India.

Aidha alimshukuru Rais Mstaafu Jakaya Mrisho, kupitia GWP kwa juhudi zake za

kubeba jambo hili kwa hatua zote,alipokuwa Dakar,nchini Senegal aliagiza utekelezaji

wa hilo na baada ya muda mfupi alipatikana na kuanza kazi, May-Nov 2022.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Ushirika wa Wadau wa Maji (GWP ) Dkt Victor

Kongo alisema zoezi la Mpango Mkuu wa maji lilikua gumu kidogo kwani ilibidi watafute

nyaraka na ripoti mbali mbali kuanzia miaka ya 60 iliyopita hadi sasa ili kutambua

miundo, mifumo na mipangilio iliyopo ya usimamizi wa sekta ya maji Zanzibar na



changamoto zake. Pia, walifanya tathmini kutambua wingi na ubora wa rasilimali maji

Zanzibar na changamoto za usimamizi wake.

Alisema kupitia mashirikiano mazuri na taasisi ya Global Water Partnership, Dkt.

Mngereza aliweza kuhudhuria kikao cha dunia cha World Water Forum kule Dakar

Senegal ambapo alikutana na wadau wa kimataifa katika sekta ya maji.

Alifahamisha kwamba wadau hao ni pamoja na mkuu wa chuo cha kimataifa cha IHE-

Delft kilichoko Uholanzi ambacho ni hodari katika utafiti na taaluma katika sekta ya maji.

Alisema Pia kupitia chuo hicho pamoja na taasisi ya SADC Groundwater Monitoring

Institute, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Wizara ya Maji nishati na Madini

walianzisha kongamano la kila mwaka la kisayansi kuhusu maji Zanzibar ambalo

lilifanyika kwa mara ya kwanza tarehe 14-15 Septemba mwaka 2022 na litakuwa

likifanyika kila mwaka.

Alifahamisha tathmini waliyoifanya ilibainisha mambo makuu saba kati ya mambo hayo

ikiwemo athari za mabadiliko ya tabia nchi katika sekta ya maji Zanzibar, Kwa muda

mrefu, hakujakuwa na mpangilio maalum au Programme ambayo ina ratibu mwenendo

wa utekelezaji wa miradi katika sekta ya maji. Hali ambayo ilisababisha kutokuwa na

muelekeo maalum wenye malengo katika sekta ya maji.

Vile vile alisema Sera ya maji ya 2004 ina mapungufu kadhaa ambayo inatakiwa

kushughulikiwa kwa kufanya mapitio ya hiyo sera. Pia Kunahitajika hatua madhubuti za

kuboresha miundo mbinu iliyopo na pia kuongeza miundo mbinu mipya ya kusambaza

maji.

Sambamba na hayo hatua madhubuti zinahitajika kujenga mashirikiano na taasisi za

kikanda na kimataifa katika sekta ya maji ili kupanua wigo wa mashirikiano ya kitaluma

na utafiti.



Aidha Dkt Mngereza na Dr Victor wamempongeza Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali

Mwinyi kuwa Mpokeaji wa Kwanza wa Tuzo ya Kifahari ya VIP Global Water Change

Maker, pamoja kuwa pongeza viongozi wa Wizara ya Maji, Nishati na Madini kwa

Kuendeleza utekelezaji wa Mpangu Mkuu wa Maji Zanzibar.


Mwisho.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch