Skip to main content

WAZIRI RAHMA APONGEZA UZALENDO WA KIVITENDO GANDO

 



WAZIRI wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar, Rahma Kassim Ali amewashukuru wananchi wa Kijiji cha Gando Pemba kwa uzalendo wao wa kutoa eneo la ardhi kwa kikosi cha KMKM kwa ajili ya ujenzi wa  kituo cha Afya.

Kauli hiyo ameitowa wakati alipoweka jiwe la msingi katika eneo hilo ikiwa ni shamra shamra za maadhimisho ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar kutimiza miaka 59 tangu yalipotokea mwaka 1964.

Alisema wananchi wa Kijiji cha Gando wameonesha  moyo wa uzalendo na kueka kando itikadi za kisiasa kwa kutoa eneo lao kuwapa Kikosi cha KMKM kujenga Kituo cha Afya. hivyo ni jambo  jema na la kuwashukuru.

“Hakika nyinyi ni wana mapinduzi halisi na mmeonesha kwa vitendo jinsi mnavyoshirikiana na Serikali kuleta maendeleo katika eneo lenu. Nasaha zangu kwa wananchi wengine Unguja na Pemba kuiga  mfano wenu hasa ikizingatiwa kuwa maendeleo hayana chama, nakushukuruni kwa dhati kwa kutoa eneo lenu kwajili ya kituo cha afya,”alisema.

Pia aliwashukuru mafundi na vibarua wa KMKM, kwa hatua waliyofikia katika mradi wa ujenzi kituo hicho kwa kwenda muda na kwa gharama ndogo kwani  bila ya hivyo gharama zingelikuwa kubwa zaidi kwa Serikali katika kutekeleza mradi huo.

Hivyo waziri Rahma alimuagiza Komodoo wa KMKM Azana Hassan Msingiri kuwatizama kwa jicho la huruma mafundi na vibarua waliyofanikisha ujenzi huo ili kuthamini jasho na uzalendo wao.

Alieleza kwamba anaamini mradi huo wa kituo cha afya utakapo kamilika huduma bora zitapatikana kwa askari pamoja na wananchi kama vile ambavyo zinaonekana kwenye Hospital ya KMKM Kibweni Unguja.

Aidha alisisitiza umuhimu wa kuwepo vifaa, madaktari, manesi na maodali wa kutosha kwa mujibu wa mwongozo wa vituo vya afya uliotayarishwa na Wizara ya Afya Zanzibar katika kituo hicho kitakapoanza kutoa huduma.

 Vile vile aliwakumbusha wafikirie umuhimu wa  kutoa huduma za mama na mtoto ili wananchi  wa Gando pamoja na vitongoji vyake wasipate tabu na usumbufu wa kwenda kujifungulia maeneo ya mbali jambo ambalo litakuwa sio sahihi.



Aidha alisema hatua ya wananchi kutoa eneo lao inaonesha taswira kwamba wananchi hao wako tayari kushirikiana na KMKM kutoa taarifa za watu wanaotaka kusafirisha magendo ya karafuu na magendo mengine ikiwemo uvuvi haramu na uchafuzi wa bahari hali ambayo itasaidia kuimarika kwa kambi ya KMKM Gando.

“ Kuimarika kwa kambi hiyo kusaidia Serikali na jamii juu ya uvuvi haramu na uhifadhi wa bahari yetu. Hivyo basi, ushauri wangu kwenu wanaKMKM mzidishe mashirikiano na wananchi wa Kijiji cha Gando na vijiji jirani kwani kufanya hivyo kutasaidia sana ufanisi wa kazi zenu nzito ambapo huwa mnakabiliana na watu ambao hamuwaoni lakini kwa msaada wa wananchi basi mtawaona”Alisema waziri huyo.

Sambamba na hayo Waziri Rahama alimuagiza Katibu Mtendaji wa kamisheni ya ardhi Zanzibar kuwapatia  hatimiliki ya eneo hilo ambapo ombi  hilo liliwasilishwa kwa waziri wa ardhi kupitia  risala iliyosomwa awali.

                               Mwisho

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch