Skip to main content

MAPINDUZI YA MWAKA 1964 MKOMBOZI WA MAWASILIANO MTANDAO ZANZIBAR, MIAKA 59 SASA DUNIA WA KIGANJA

 





NA ZUHURA JUMA, PEMBA:::

MAPINDUZI ya 1964 chini ya jemedari wake marehemu Abeid Amani Karume, yamekuja kutatua changamoto za wananchi pamoja na kuimarisha sekta mbali mbali ya kimaendeleo, hapa nchini.


Miongoni mwa hayo ni kuimarisha huduma za mawasiliano ya kimtandao, kila kona ya Zanzibar, ili kuhakikisha kwamba wananchi wanafanya kazi zao vizuri kupitia mawasiliano.


Mawasiliano ya kimtandao ni muhimu, katika maisha ya kila siku ya mwanadamu, kutokana na kurahisisha kila kitu katika ulimwengu huu wa sasa kidijitali.


Wanajamii wana msemo wao usemao… ‘dunia kiganjani’ hii inaonesha dhahiri kwamba mawasiliano ya kimtandao, yamerahisisha kila kitu katika ulimwengu huu na sasa kuwa kiganja.


Njia mbali mbali zinatumika kuwasiliana kwa sasa, ukilinganisha na zamani kabla ya Mapinduzi yam waka 1964 ambayo sasa tunasherehekea miaka 59, ambapo watu walilazimika, kupeleka barua kufikisha ujumbe ambapo ulikuwa ukichukua muda mrefu.


Lakini kwa miaka hii 59 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar, unaweza kufikisha taarifa nchi yeyote kwa sekunde tu na kupata mrejesho papo hapo (feedback).

Hiyo ni faraja kubwa kwa wananchi wa Zanzibar, wanaotembea kifua mbele sasa ndani ya miaka hii 59 ya mapinduzi Zanzibar, kwani mawasiliano ya kimtandao yamekuja kuwarahisishia maisha yao.

Ibrahim Saleh Juma ambae ni Afisa Mdhamini Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Pemba anasema, kutokana na uharaka wa mawasiliano ya kimtandao, wananchi wanapata kufanya biashara zao mtandaoni, pamoja na mawasiliano ya moja kwa moja.

Kuna mitandao mbali mbali ambayo hutumiwa kwa mawasliano, ikiwemo kupiga simu, ambazo kampuni zake zimeekeza kisiwani hapa, kwa lengo la kuwafanya wananchi kupata mawasiliano popote walipo.

Kuna kampuni kama vile Zantel, Tigo, TTCL, Vodacom, Halotel na Airtel ambazo mitandao yake ipo vizuri kisiwani hapa na wananchi wanaedelea kuitumia kila siku.

Kwake anaona miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar, imefanikiwa kuimarisha huduma ya kiinteneti maeneo yote ya mjini na vijijini, kutokana na kampuni hizo, kujenga minara ambayo inawezesha huduma hiyo kuingia kila pembe ya kisiwa hiki.

‘’Kabla ya mapinduzi haya, wazanzibari wenye taifa lao hili hawakuwa na uhuru wa kuwasiliana, kupata habari, kufikishiana taarifa kwa wakati kama ilivyo sasa, maana hayo yalikuwa kwa wale watawala,’’anasema.

Mdhamini huyo anaeleza kuwa, mitandao kama kijamii ya whatsApp, Twitter, facebook na Instagram imekuwa ikiwarahisishia wananchi kutumiana ujumbe na kufika kwa muda mfupi, jambo ambalo kabla ya Mpinduzi ya Zanzibar halikuwepo.

“Tuna kila sababu ya kujivunia matunda ya Mapinduzi yetu ya miaka 59, kwa sababu zamani watu walikuwa wanafikisha taarifa kwa kutumia barua na walikuwa wakisukuma baiskeli kutwa nzima, lakini kwa sasa tuna simu, za haraka za kufikisha ujumbe”, anasema.

Wakati huo hata gari hazikuwepo nyingi, hivyo inapotokea dharura kama vile kifo, basi jamaa wa mbali, wanaweza kupata taarifa kuanzia siku ya tatu na kuendelea.

“Kwa kweli kabla ya Mapinduzi ya mwaka 1964, hali ilikuwa ni tete ya kimawasiliano, wananchi walikuwa wakihangaika kwa kila jambo, kwa sababu huduma nyingi, zilikosekana wakati huo”, anafahamisha.



Katika ziara iliyofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, aliibua changamoto za mawasiliano na baada ya hapo, ilipata kujengwa minara 13 mipya.

“Kipindi cha katikati kuna watu kwenyebaadhi ya vijiji, walikuwa wanapanda hata kwenye miti kutafuta mawasiliano na wengine walikuwa hata hawajui mawasiliano ni kitu gani”, anahadithia.

Lakini kwa sasa kufikia miaka 59 ya Mapinduzi Zanzibar, Serikali imeimarisha eneo hilo la mawasiliano ya kimtandao, hasa kupitia simu za mkononi na internet.

Anafafanua kuwa, kila kwenye mnara mawasiliano, yanavuta kutoka kilomita moja hadi kilomita nne masafa yake yanavyokamata, hivyo inawezekana mtu yupo karibu sana ya mnara na mawasiliano, yakawa ya shida kidogo.

Kuna baadhi ya wananchi wamekuwa wakilalamika kwamba wapo masafa ya karibu lakini hawapati mawasiliano vizuri, anasema Mdhamini huyo kuwa, ni kweli kwa sababu minara hiyo kuanza kukamata zaidi masafa ya mbali kuliko karibu kwani inavuta juu.

Hivyo, inawezekana wapo watu wachache wanaoweza kupata shida ya mawasiliano, lakini hayo yanaendelea kerekebishwa na mnara katika eneo jengine ambao utawanufaisha wao.

“Pia kuna mawasiliano ambayo tunayatumia ya ujazo wa 2G, 3G na 4G lakini kwa sasa tunakwenda kuimarisha kwenye eneo la ujazo wa 5G, hii ni kuhakikisha kwamba Serikali, ipo mstari wa mbele kuwaimarishia wananchi wake miundombinu ya mawasiliano”, anaeleza.

Taarifa za kitaalamu zinaonesha kwamba ujazo wa 2G inakamata watu 200 hadi 300 kwa sekunde, 3G inaunganisha watu kati ya 300 hadi 350 kwa sekunde na 4G inaunganisha watu kati ya 400 hadi 500 kwa sekunde.

Anasema, katika kisiwa cha Pemba maeneo mengi tayari yana mawasiliano kwa kiwango kikubwa, ambacho sasa hakimuachi mtu nyuma.

‘’Kama ukitaja matunda ya mapinduzi ya Zanzibar ndani ya miaka 59, basi kwenye mawasiliano sasa jamii iko vizuri, maana mawasiliano ndio kila kitu na sekunde moja ikiwa ikikosekana, kuna hasara,’’anasema.



Anaeleza kuwa, Dk. Mwinyi mara baada ya kuingia madarakani alifanya ziara maalumu ya kupita maeneo mbali mbali kwenye kisiwa hiki na kusikiliza wananchi.

Aliibua changamoto mbali mbali ikiwemo ya mawasiliano na kuwaahidi wananchi kwamba atalifanyia kazi na ndio maana kisiwa hiki kikapata minara hiyo 13 mipya iliyojengwa na kampuni ya HTC wakishirikiana na kampuni ya Zantel.

“Minara hiyo tayari imeshakamilika na inaendelea kutoa huduma za mawasiliano katika yale maeneo ambayo yalikuwa na changamoto kubwa ya mtandao”, anasema.

Kati ya minara hiyo 13, Wilaya ya Chake Chake ilipata minara mitano katika maeneo ya Wesha, Vikunguni, Mfikiwa, Shungi na Ngomeni hizo zote ni juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuhakikisha wananchi wake waishi maisha bora.

Kwa Wilaya ya Wete minara hiyo ilijengwa katika maeneo ya Kangagani, Mchangamdogo, Finya pamoja na Ukunjwi.

Kwa upande wa visiwa tayari wamejenga mnara katika kisiwa cha Fundo ambao unashika pia katika maeneo ya kisiwa cha Kokota, Funzi na Ukunjwi.

Serikali haijasimama hapo tu, bali itaendelea kuvifikishia visiwa vyengine huduma hiyo, ili mawasiliano yapatikane bila ya usumbufu.

Anasema, kwa wakati huu wanaendelea kufanya utafiti wa maeneo ambayo bado kuna shida sana ya mawasiliano ingawa asilimia 90 ya wananchi wanapata mawasliano bila ya usumbufu.

Aliwaomba wananchi kuendelea kuwa watulivu na kuiamini Serikali yao na kushirikiana pamoja, kwani ina malengo makubwa ya kuhakikisha kila mwananchi pale alipo anapata mawasiliano ya uhakika ambayo hayatakuwa na shida ya aina yeyote.

Mdhamini anaeleza pia wana mkonga wa taifa ambao unarahisisha kutoa huduma za mawasiliano za internet katika taasisi za Serikali na jamii kwa ujumla.

“Kwa Pemba tunavyo vituo vinne vya Tehama, vituo hivi vinawarahisishia sana wananchi kuweza kurahisisha mambo yao, mfano maombi ya kazi, kujifunza kuingia kwenye internet na pia tunawapatia mafunzo mbali mbali”, anafafanua.

Vituo hivyo vya Tehama vimejengwa Machomane Wilaya ya Chake Chake, Mtambile kwa Wilaya ya Mkoani, Utaani kwa Wilaya ya Wete na Micheweni, ambapo vinaendelea kutoa huduma ya kupatiwa mafunzo kwa wananfunzi na wananchi wa kawaida.

Mwanafunzi wa skuli ya Sheikh Idrisa Abdulwakil iliyopo Kizimbani Wete Raya Suleiman anasema, akimaliza kidato cha nne tu ataenda kituo cha Tehama Utaani kujifunza vitu mbali mbali, ili atakapoingia chuo asipate shida.

“Serikali yetu inatupenda sana kwa sababu kama haikuweka vituo hivi vya Tehama ingebidi tukalipie pesa ya kusomea na wazazi wengine hawana uwezo kifedha, hivyo inatusaidia sana”, anaeleza.

Mama mmoja mkaazi wa Chasasa Wete, Asha Juma Ali mwenye miaka 66 anasema kuwa, Mapinduzi ya mwaka 1964 yamekuja kuimarisha kila kitu, ikiwemo hiyo mtandao.

“Zamani ilikuwa hakuna simu wala hayo mambo yenu munayotumia siku hizi ‘internet’, ilikuwa pakitokea msiba watu wanakwenda kupeleka taarifa kwa miguu au baskeli, ata watu wakifika maiti ishazikwa”, anasema.

Anaeleza kuwa, yeye binafsi alishawahi kupeleka barua kwenda mpaka Dar-Es-Salaam, jambo ambalo lilikuwa likiwasumbua sana kwani walikuwa wanapotezea muda.



Ali Khamis Ali mkaazi wa Kichungwani Chake Chake anasema, mawasiliano ndio yaliyorahisisha kila kitu, kwa sababu watu mpaka biashara zao kwa sasa wanafanya kwenye mitandao.

“Mitandao ni kitu muhimu sana, kwa sababu dakika tu ikikosekana kwa dharura kama ikiwa kwenye matengenezo, basi tunalalamika, kwa kweli inatusaidia sana”, anaeleza.

Mkaazi wa Micheweni Suleiman Faki Hamad anasema kuwa, bila ya kuwepo kwa mtandao kwa maisha ya sasa hayawezi kwenda, kwa sababu hata unapokwenda sehemu kama huijua, ukiwa na simu tu basi hupotei.

Mfanyabiashara anaetumia mitandao kuuza bidhaa zake ambae hakutaka jina lake litajwe mkaazi wa Chake Chake anasema, amekuwa akiingiza mapato kupitia mitandao, kwani biashara inafanyika vizuri.

“Unapoweka bidhaa zako mtandaoni watungi wanaona, hivyo ni rahisi kuuza mara moja na kuingiza mzingo mwengine, mawasiliano yameturahisishia kila kitu kwa kweli”, anaseama.

Januari 12 mwaka 2023 wananchi wa Zanzibar wanaadhimisha miaka 59 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar yakiongozwa na Rais wa awamu ya nane Dk. Hussein Ali Mwinyi ambae anaendeleza kuimarisha uchumi na kuleta maendeleo katika sekta zote.

                                                               MWISHO.    

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch