Skip to main content

BLOG PEMBA TODAY YASAIDIA KUIREJESHA HUDUMA YA MAJI SHUMBA MJINI PEMBA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA::

WANANCHI 6,680 wa shehia ya Shumba mjini wilaya ya Micheweni Pemba, waliokuwa wakikabiliwa na ukosefu wa huduma ya maji safi na salama kwa muda wa mwezi mmoja, sasa huduma hiyo, imerejea kama kawaida.

 

Itakumbukwa kuwa, Novemba 20, mwaka 2022, blog hii  https://pembatoday.blogspot.com/2022/11/shumba-pemba-watumia-maji-ya-bahari-kwa.html ilichapisha habari ikielezea tatizo la ukosefu wa huduma hiyo kwa wananchi  hao.

 

Walisema, huduma hiyo kwa sasa imerudi kama asili yake, baada ya huduma ya nishati ya umeme, nayo kurudi kama kawaida hasa kwenye kisima chao cha maji safi na salama kilichopo Shumba wilayani humo.

 

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kupitia blog hii, walisema huduma hiyo imerejea vyema, baada ya blog ya pemba today kuripoti ukosefu huo mwezi mmoja uliopita.

 

Walisema kabla ya kurejea kwa huduma hiyo, awali walilazimika kununua kwa dumu moja lenye ujazo la lita 20, kati ya shilingi ya 500 hadi shilingi 1,000, kutoka shehia za Micheweni.

 

Wananchi hao wa vijiji vya Chamboni, Vumbini, Nduaga, Momogu, Mkunguni, Kichekwani, Tundumwe na Msasani kwa wale wasio na uwezo walilazimika kutumia maji ya bahari, kwa shughuli nyingine.

 

Mmoja kati ya wananchi hao Hamad Ali Hamad, alisema kwa sasa wanaishi kwenye furaha na kujipangilia vyema kazi zao, baada ya huduma hiyo kurejea.

 

‘’Ni kweli, kwa sasa huduma ya maji safi na salama imeanza kurejea na hili tulipofuatilia tuliambiwa ni baada ya huduma ya nishati ya umeme kurejea kama kawaida,’’alisema.

 

Nae Kurata Bakar Said, alisema huduma hiyo ya maji safi na salama, imekuwa nzuri sasa, na imewarahisishia kupanga na kuendesha shughuli zao mbali mbali.

 

Kwa upande wake Fatma Mohamed Awadhi, alisema maji ya ‘ZAWA’ sasa yamerudi na wanalishukuru shirika la Umeme la Zanzibar ZECO kwa kuituliza huduma ya umeme.

 

‘’Mwezi mmoja nyuma ilikuwa unaweza kukaa wiki ukasikia maji eneo fulani yanatoka, lakini ukifika unaweza kubahatika ndoo moja au mbili, na kisha yanafungwa, lakini sasa twashukuru,’’alifafanua.

 

Nao wananchi Omar Khamis Kombo na Biache Mohamed Hamad walisema, sasa kama imerejea ni vyema wenzao wakaitumia kwa uangtalifu sambamba na kuyalinda miundombinu husika.

 

 Sheha wa shehia ya Shumba Mjini mjini Rahila Ramadhan Juma, alikiri kuwa sasa malalamiko ya wananchi wake, juu ya ukosefu wa huduma hiyo, hayapo tena.

 

Alisema anaelewa kuwa, kwa zaidi ya siku 30, baadhi ya wanachi hawakuwa wakiipatia kabisa huduma hiyo, na baadhi ya maeneo yakitoka huwa ni kwa kusua sua.

 

‘’Kwa hakika, huduma ya maji safi na salama ndani ya shehia yangu, ilikuwa tatizo, lakini sasa imerejea kama zamani, twaamini kilio chetu kimesikika,’’alieleza.

 

Afisa wa Mamlaka ya Maji ‘ZAWA’ wilaya ya Micheweni Ali Rajab, awali alikiri kupokea malalamiko ya sheha huyo, juu ya huduma hiyo kuwa ndogo, ingawa kwa sasa imekaa pahala pake.

 

Alieleza kuwa, tatizo hilo halitokani na uhaba wa huduma ya maji kwenye kisima wanachokokitegemea cha Kijichame, bali ilikuwa ni kupanda na kushuka kwa nishati ya umeme.

 

Hata hivyo afisa huyo, alisema kuwa kisima hicho ambacho kinauwezo wa kuzalisha lita 17,000 kwa saa moja, na kuwekwa bomba lenye ujazo wa nchi tatu.

 

Afisa Uhusiano wa ‘ZAWA’ Pemba Suleiman Anasi Massoud, alisema mashine iliyopo kwenye kisima wananchokitegemea wananchi hao wa Shumba, kilipata hitilafu ya umeme kwa kule kupanda na kushuka.

 

‘’Mshine iliyopo kwenye kisima hicho ni ya kisasa, hivyo kama umeme ukiwa mkubwa au mdogo kama ilivyokuwa, hujizima wenyewe na kukosa nguvu ya kusukuma maji,’’alieleza.

 

Hata hivyo, alisema changamoto kubwa ambayo ipo kwa wananchi hao, ni ukosefu wa tenki la kuhifadhia maji, ambapo hilo huisababishia mashine iliyopo, kufanyakazi kwa saa 24 bila ya mapumziko.

 

 Afisa Mawasiliano na Huduma kwa wateja wa Shirika la Umeme Zanzibar ‘ZECO’ Pemba Haji Khatib Haji, hivi karibuni alinukuliwa na vyombo vya habari, akisema tatizo la kupungua kwa umeme ovyo ovyo, kutokana na eneo la Tanga kupata hitilafu.

 

Hivi karibuni, kwenye kongamano la kutimiza miaka miwili ya rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, ilifahamika kuwa, kwa Pemba kuna vituo 27 vya huduma ya maji safi na salama na ujenzi wa matenki matano (5), yenye uwezo wa kuhifadhi maji lita milioni 1, kila moja.

                                     Mwisho.

  

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch