Skip to main content

MIAKA 59 YA MAPINDUZI: DK. MWINYI AFUNGUA SKULI YA GHOROFA MWAMBE, AAHIDI KUJENGA NYINGINE

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA::

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameigaiza wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, kushirikiana kwa karibu na Idara ya Utumishi, ili kuajiri waalimu nchini.

Alisema, changamoto ya uhaba wa waalimu anajua kuwa, ipo, lakinini ni vyema kwa wizara husika, kuongeza kasi ya kuajiri waalimu na kipaumbele, iwe ni wale ambao walishajitolea siku za awali.

Alieleza kuwa, wakati serikali ikijenga skuli mpya zikiwemo za ghorofa na kuzifanyia ukarabati zile za zamani, lazima na suala la kuajiri waalimu nalo liangaliwe kwa haraka.

Dk. Mwinyi ameyasema hayo Mwambe wilaya ya Mkoani Pemba, mara baada ya kuifungua skuli mpya ya ghorofa mbili ya msingi Mwambe, wakati akizungumza na wanafunzi na wananchi wengine, ikiwa ni shamra shamra za miaka 59, ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.

Alieleza kuwa, anasisitiza kuwa, wakati wizara hiyo ikiajiri waalmu wakiwemo wa masomo ya sayansi, iwape kipaumbele waalimu wenye sifa, na ambao walishawahi kujitolea, ili kuzingatia moyo wao wa kizalendo waliouonesha.

‘’Kama walionesha moyo wa kujitolea kwa taifa lao, kwa kuwatumikia wananchi wenzao, sasa wakati ukifika wa uajiri, nao wapewe kipaumbele kwa wenye sifa,’’alisisitiza.

Katika hatua nyingine Rais huyo wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameahidi kujenga skuli nyingine ya ghorofa eneo hilo la Mwambe, ili kukabiliana na uwingi wa wanafunzi uliopo.

Alieleza kuwa, ameshtushwa na idadi ya wanafunzi wanaoendelea kuandikishwa wa darasa la kwanza kwa mwaka huu, ambao kwa sasa wameshafikia 970.

‘’Kwa hili, lazima niwaahidi wananchi wa Mwambe na vijiji jirani kuwa, serikali itajengwa tena skuli nyingine ya ghorofa, ili mwakani tukisherehekea miaka 60 ya Mapinduzi, nayo iwepo,’’alieleza.

Hata hivyo rais huyo ameelezeam kuridhishwa na usimamizi mzuri wa fedha wa shilingi bilioni 68, walizopewa wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, kwa ajili ya ujenzi wa skuli mbali mbali nchini.



Hata hivyo alisema, bado serikali ya awamu ya nane, itaendelea kuona kuwa, elimu ndio kipaumbele cha kwanza, na azma ya kujenga skuli za kisasa na vifaa vya kufundishia ipo.

‘’Ndio maana zipo skuli 24 za zamani kwa Unguja na Pemba, zinaendelea kufanyiwa matengenezo makubwa, ambapo kwa wilaya ya Mkoani, ni skuli za Mauwani Kiwani, Chambani na Maendeleao Ngwachani.

Hata hivyo alisema, ndani kipindi cha mwaka mmoja, serikali imeshajenga madarasa 143, kati ya hao 95 yalianzishwa kwa nguvu za wananchi na 48 ndio mapya, samba mba na ujenzi wa vyoo 318 kwa skuli za maandalizi, msingi na sekondari mkoani humo.

Kuhusu mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, alisema kuwa, moja ya shabaha ni kuhakikisha watoto wa taifa hili, wanapata nafasi ya kujifunza, wakiwa kwenye skuli kisasa.

Alisema, ndio maana serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya awamu ya nane, imeweka kipaumbe cha miradi mbali mbali ya wananchi, ikiwemo ya elimu, ili kupunguza athari za ukosefu wa makaazi ya kisasa ya kujifunzia.

‘’Leo tukiwa tunaadhimisha miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar, tunayo mengi ya kujivunia, ikiwa ni pamoja sekta ya elimu, afya, miundombinu ya barabara na huduma nyingine za kijamii, kuimarika,’’alieleza.

Kwa upande wake Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Leila Mohamed Mussa, alisema kasi ya Dk. Mwinyi ndani ya wizara hiyo, imesaidiai kutatua changamoto mbali mbali, zikiwemo za maakazi.

Alisema, sio Mwambe pekee lakini kila wilaya ya Unguja na Pemba, Rais huyo, ameshaacha alama kwa kuhakikisha kunajengwa skuli za kisasa na za ghorofa, kuingiza na fanicha zake kamili.



‘’Malengo ya Mapinduzi ya Zanzibar baada ya kuasisiwa na viongozi waliotangulia, sasa yanaendelezwa kwa kasi na serikali ya awamu ya nane, chini ya Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, kwa hili hongera sana,’’alisema.

Aidha alimpongeza Dk. Hussein kwa kuwapatia fedha shilingi bilioni 68, kwa ujenzi wa skuli na kutia samani, na ununuzi wa vitabu, sambamba na kukamilisha ujenzi skuli 25 za maandalizi Unguja na Pemba.

Nae Katibu Mkuu wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khamis Abdalla Said, alisema ujenzi huo ambao sasa umejumuisha madarasa 46, yakiwemo 5 ya zamani

Alisema kuwa, fedha za sherehe ya mapinduzi shilingi milioni 450, zitawasaidia kwa ununuzi wa samani na vitambu katika skuli mbali mbali za Unguja na Pemba.

Alifahamisha kuwa, ujenzi wa skuli hiyo na nyingine ni utekelezaji wa ahadi zake kwa vitendo, alizozitoa kipindi cha kampeni.

‘’Skuli hii yenye ghorofa mbili na moja ya chini (ground) ni ya kwanza kwa Zanzibar, ambayo itapunguza changamoto ya makaazi wa wanafunzi wa Mwambe,’’alieleza.



Hata hivyo aliafafanua kuwa, wizara tayari imeshaingiza viti, meza mpya na za kisasa ndani ya skuli hiyo na iko tayari kwa ajili ya kuhamiwa.

Mapema Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, amewakumbusha wananchi wa Mwambe, kuilinda miundo mbinu ya skuli hiyo.

Aidha alieleza kuwa, sasa vipo vyumba vya madarasa 1,116 ndani ya mkoa wa kusini Pemba, ikijumuisha hivyo 42 vya skuli ya ghorofa ya Mwambe. 

Afisa Mdhamini wizara ya elimu na mafunzo ya Amali Pemba Mohamed Nassor Salim, alisema matayarisho ya kuongoeza idadi ya waalimu skuli hapo, yameshakaa vyema.

Mwakilishi wa Jimbo hilo Mussa Foum Mussa, aliiomba serikali kuhakikisha kunaongezwa idadi ya waalimu, ili kwenda sambamba na idadi ya wanafunzi.



 Mwalimu mkuu wa skuli hiyo, Ali Mohamed Omar, alisema ujenzi wa skuli hiyo, umetoa mwanga mpya wa kupata elimu kwa wanafunzi wao.

Alisema sasa kilichobakia ni jukumu la wazazi na walezi, kuwahimiza wanafunzi wao ili, uwepo wa jengo hilo la ghorofa mbili, thamani yake iaendane na kasi ya kupata elimu.

Mwananchi Hassan Kombo na Aisha Omar Ali waliipongeza serikali kwa kutimiza ahadi yake ya ujenzi wa skuli hiyo, ambao umefanikiwa kuondoa msongamano wa wanafunzi madarasani.

Skuli hiyo ya ghorofa mbili ya msingi ya Mwambe wilaya ya Mkoani Pemba, ujenzi wake umechukua mwaka mmoja, umejengwa na kampuni na Mwamba kwa shilingi bilioni 3.571 fedha za UVIKO 19, kupitia Shirika la Fedha Duniani ‘IFM’.

                     Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch