Skip to main content

IDARA KATIBA YAUKARIBISHA MWAKA MPAY KWA KUTOA TAHADHARI

 





NA HAJI NASSOR, PEMBA::

WANANCHI kisiwani Pemba, wametakiwa kuufanya mwaka mpya wa 2023, uwe wa mageuzi kwa kupunguza matukio ya ukatili na udhalilishaji, kwa kuwatumia wasaidizi wa sheria, ili kupata elimu, ushauri na msaada wa kisheria.

 

Kauli hiyo imetolewa na Afisa sheria, kutoka Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar, ofisi ya Pemba Bakari Omar Ali, wakati akizungumza na mwandishi hizi, katika kuukaribisha mwaka mpya.

 

Alisema, matukio ya ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na watoto bado yalikuwa yameshika kasi kwa mwaka 2022, hivyo amewataka wananchi, kwa huu 2023 uwe mwaka wa mageuzi kwa kupunguza matukio hayo.

 

Alieleza kuwa, Idara inaowasaidizi wa sheria katika kila jimbo, la uchaguzi, hivyo ni vyema wakawatumia ili kupata uwelewa wa kisheria, sambamba na elimu ya kupambana na matukio hayo.

 

Afisa sheria huyo alifafanua kuwa, wasadizi hao wa sheria, wako tayari na saa yoyote kutoa elimu na msaada wa kisheria bila ya malipo, hivyo ni wajibu wa wananchi, kuwa nao karibu.

 

‘’Zanzibar bila ya kuwa na matendo ya ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na watoto inawezekana sana, ikiwa jamii itafanyakazi kazi, kwa karibu na wasaidizi wa sheria,’’alieleza.

 

Katika hatua nyingine Afisa sheria huyo, amewataka wananchi kushirikiana na vyombo vya sheria, kama jeshi la Polisi, Mahakama katika kutokomeza matendo hayo.

 

Alisema moja ya changamoto iliyojitokeza kwa mwaka uliomalizika, ni kwa wananchi kutofika mahakamani kutoa ushahidi na kusababisha kesi nyingine kuondolewa.

 

‘’Wapo watuhumiwa kadhaa wa makosa ya ukatili na udhalilishaji kwa mwaka jana, wameachiwa huru, baada ya mashuhuda wa matukio hayo, kukataa kufika mahakamani kutoa ushahidi,’’alisema.

 

Wakati huo huo Afisa huyo amezitaka jumuia za wasaidizi wa sheria Pemba, kuendelea kuwa karibu na Idara hiyo, ili kufanikisha majukumu yake mbali mbali.

 

Alisema kwa mwaka uliopita, walishirikiana vyema na Idara hiyo, hali iliyopelekea kufanikisha shughuli mbali mbali, kama mikutano ya wazi ya utoaji elimu ya kisheria.

 

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Jumuia ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, aliipongeza Idara hiyo, kwa kuendelea kuwaamini katika utendaji wao wa kazi.

 


‘’Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, imekua ikituamini katika utendaji wetu wa kazi, na tunashirikiana kwa karibu, katika kufanikisha azma ya kuwafikia wananchi,’’alieleza.

 

Hivyo Mkurugenzi huyo, ameuhakikisha uongozi wa Idara hiyo kuwa, kwa mwaka huu wa 2023, watazidisha kasi na kufanyakazi kwa karibu, ili wananchi wazitambur haki zao.

 

Nae Mkurugenzi wa Jumuia ya wasaidizi wa sheria Mkoani Nassor Hakim Haji, aliipongeza Idara hiyo kuwa kufanikisha jukwaa la pili la msaada wa kisheria, lililofanyika mwishoni mwa mwaka jana kisiwani Unguja.

 

Hata hivyo amewakumbusha watendaji wenzake, kuzidisha kasi, ari na hamu ya kuwahudumia wananchi, katika kupambana na matendo ya dawa za kulevya na udhalilishaji.

 

Akizungumza hivi karibuni kwenye jukaa la pili la msaada wa kisheria, Mkurugenzi wa Idara hiyo, Hanifa Ramadhan Said, alisema mwaka huu 2023, utakuwa mzuri kama ushirikiano utaongezeka.

 


‘’Mimi najua kwenye jumuia za wasaidizi wa sheria, zipo changamoto mfano gharama za kukodi za ofisi, ukosefu wa usafiri, lakini tuongeze juhudi za kuwafikia wananchi popote walipo,’’alishauri.

 

Baadhi ya wananchi kisiwani Pemba, walisema kazi inayofanywa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, kwa kushirikiana na wasaidizi wa sheria ni kubwa, ingawa kwa mwaka huu, lazima ushirikiano wao uongezeke.

 


Mnufaika wa msaada wa kisheria kutoka shehia ya Madungu wilaya ya Chake chake, Asha Hussein Seif, anasema upo umuhimu mkubwa wa wasaidizi wa sheria, kuendelea kujengewa uwezo.

                              Mwisho    

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch