Skip to main content

WANAFUNZI WA MADRASSA CHAKE CHAKE WAPEWA NJIA KUJIKINGA NA UDHALILISHAJI

 




NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

IDARA ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, ofisi ya Pemba, imewakumbusha wanafunzi wa madrassa za qur-an kisiwani Pemba, kujitenga mbali na watu wanaowanesha dalili za vitendo vya udhalilishaji, ikiwa ni pamoja na kuwawekea picha chafu kupitia simu zao.

Kauli hiyo imetolewa leo Januari, 7 2023 kwa nyakati tofauti, na mwakilishi wa Idara hiyo Mohamed Massoud Said, wakati akizungumza na wanafunzi wa madarassa za Vikunguni na Machomane wilaya ya Chake chake, kwenye ziara maalum, ya kutoa elimu ya kupambana na matendo hayo.

 Alisema, moja ya dalili ya mtu anaetaka kumdhalilisha mtoto huanza kwa kumuonesha picha za ngono, kumnunulia zawadi, kumpa fedha, na kuendelea kwa maneno ya ushawishi juu ya udhalilishaji.



Alisema ni jukumu lao, kwanza kutoshirikiana na watu wa aina hiyo, hata ikiwa ni wazazi wao, au kutoa taarifa kwa watu wengine, kabla ya kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji.

Mwakilishi huyo wa Idara ya Katiba na msaada wa kisheria, aliwataka wanafunzi, pamoja na kujitenga na watu wa aina hiyo, lakini wasisite kuwatangaaza juu ya nia yao ovu.

‘’Wanafunzi mjue kuwa, wanaotaka kuwadhalilisha wana njia nyingi, moja wapo ni kuwapa zawadi, pesa au kuwaonesha picha za vitendo vichafu, kama njia ya kuwarubuni kabla ya kuwadhalilisha,’’alisema.



Hata hivyo, amewataka wanafunzi, waalimu, wazazi na walezi kuitumia Idara hiyo kwa kutoa taarifa za matukio hayo, au uwepo wa watu wanaojaribu, kuzifanyia sulhu kesi za udhalilishaji.

Mkurugenzi wa Jumuiya wa wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, amesema kama jamii haikushirikiana katika ulinzi wa watoto, kusitarajiwe matendo hayo kupungua.

Alieleza kuwa, watoto ni rasilimali ya taifa, hivyo kama jamii ya sasa haikuchukua tahadhari ya kuwalinda, inaweza kuwa vigumu hapo baadae, kupata viongozi na waalimu bora.




Mlezi wa madrassa na miskiti kutoka Ofisi ya Mufti Pemba Sheikh Abdulla-taif Abdalla Salim, alisema moja ya vichecheo vya kuongezeka kwa matendo hayo kwa wanafunzi, ni wazazi na walezi kutoshirikiana na waalimu.

Alisema, kama wazazi wanatabia ya kutoshiriki vikao vinavyoitwishwa na waalimu, inaweza kuwa vigumu, kuwalinda watoto waalimu peke yao.



Akizungumza kwenye ziara hiyo, Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ tawi la Pemba Safia Saleh Sultan, aliwataka wanafunzi hao, kutomruhusu mtu yeyote, kuuchezea mwili wake.

‘’Sehemu zako za siri ni mali yako, usimuonesha mtu mwengine wala usikubali kuguswa kama hakuna sababu inayokubalika, maana huo ndio mwanzo, wa udhalilishaji unapoanzia,’’alieleza.



Mratibu wa Idara ya watu wenye ulemavu Pemba, Mashavu Juma Mabrouk, ameitaka jamii, kuwatoa ndani watoto wenye ulemavu, ili kupata haki yao masingi kama elimu.

Hata hivyo amesema, lazima ulinzi kwa watu wenye ulemavu uimarishwe mara mbili, ili wawe huru na matendao ya udhalilishaji wa kijinsia, yaliokithiri.

‘’Watoto wote wanapaswa walindwe dhidi ya vitendo vya ukatili na udhalilishaji, ingawa hawa wenzetu wenye ulemavu, wanatakiwa juhudi iongezwe, kutokana na mazingira yao,’’alifafanua.

Mwalimu mkuu wa almadrassatul-Annajah Imani Ali Mohamed, alisema ziara hiyo kwao ni faraja, katika kuwakumbusha wanafunzi na matendo hayo.






Kwa upande wake Msaidizi mwalimu mkuu wa almadrassatul-Umi ya Vikunguni Zubeda Yussuf Mohamed, alisema bado wazazi hawajaona umuhimu wa kushirikiana na waalimu, katika malezi ya watoto.

Baadhi ya wanafunzi wa madrassa hizo, walisema elimu walioipata, imewasadia katika kujikinga na matendo ya ukatili na udhalilishaji.

Hata hivyo walisema, bado adhabu kali kwa wakosaji haijatolewa mahakamani, na ndio maana makosa hayo, yamekuwa yakijitokeza, kila siku ndani ya jamii.

Zira hiyo ya kutoa elimu ya kupambana na makosa ya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia, ni muendelezo ya mikakati ya Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, katika kuhakikisha kundi la wanawake na watoto, linaishi pasi na ukatili.



Ripoti ya Jeshi la Polisi Zanzibar, inaonesha, kwa mwaka 2021, kulikuwa na matendo 1,222 ya wanawake na watoto kudhalilishwa Unguja na Pemba.

Aidha ripoti nyingine ikaonesha kuwa, kulikuwa na matukio 610 ya aina hiyo, kwa kipindi cha miezi mitatu mitatu ya mwaka 2021 na 2022.

Kwa miezi ya Januari hadi Machi mwaka 2021, Jeshi la Polisi Zanzibar, lilikusanya matukio 363, ingawa kwa mwaka jana katika kipindi kama hicho, yaliripotiwa matukio 247, upunguzu wa matukio 116.

Takwimu hizo zinafafanua kuwa, kwa mwaka 2021 kwa miezi mitatu ya mwanzo, mwezi ulioongoza ni Machi, ulioripoti matukio 141, ukifuatiwa na Januari 122 na Febuari matukio 100.

Kwa mwaka 2022, mwezi uliokihiri kwa matukio ni mwezi Febuari matukio 100, mwezi Machi matukio 82, wakati mwezi wa Januari yakishuka kwa 17, na kuripotiwa matukio 65.

Taarifa hiyo ikeleza kuwa, mwezi wa Febuari kwa miaka yote miwili, iliripoti matukio sawa ya 100 kwa wanawake na watoto kudhalilishwa kwa Unguja na Pemba. 

Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba Juma Saad Khamis, alisema moja ya vyanzo vya matukio hayo, ni mporomoko wa maadili, uliozoeleka ndani ya jamii.

Hakimu wa mahakama amaalum ya kupambana na makosa ya udhalilishaji mkoa wa kusini Pemba Muumini Ali Juma, alisema chanzo ni wazazi kuacha malezi ya pamoja.

Mwanasheria dhamana wa Mahakama kuu Zanzibar Ali Rajab, anasema kuongezeka kwa matukio hayo, ni jamii kukosa elimu ya kisaikolojia, na kuyapa uzito matukio hayo yapotokezea.

Mzazi Saumu Haji Said wa Machomane anasema, kutotumika kwa sheria kama zilivyoandikwa, baada ya mtuhumiwa wa udhalilishaji kutiwa hatiani, ndio sababu ya kuongezeka.

Daktari Mohamed Ali Jape anasema, kupoteza haiba ya viungo vya mwili, ndio athari kubwa inayowaumiza watoto hasa kutokana na umri wao kutokuwa tayari kufanya tendo hilo.   

                     Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch