Skip to main content

KIZUNGUMKUTI TUHMA ZA UKATILI, UDHALILISHAJI KWA KIZIWI MICHEWENI

 


SAIDA ALI, PEMBA

MAMA mzazi ambae mwanawe mwenye ulemavu wa uziwi wa miaka 38, alifanyiwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji, ameviomba vyombo vya ulinzi na usalama, kuwa haki itendeke kufuatia unyama aliodai kufanyiwa, kijana wake.

Aliyasema hayo, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, shehia ya Shumba vyamboni wilaya ya Micheweni, kufuatia sitofahamu ya majibu ya hospitali na athari aliyonayo kijana wao.

Alisema kuwa kitendo alichodai kufanyiwa kijana wao huyo, ambacho alimshuhudia akiwa amefungwa mikono nyuma akiwa na tambara mdomoni, ni cha kikatili na udhalilishaji.

Alieleza kuwa, muda wa saa 8:00 usiku baada ya kusikia kelele za kukorota kwa kijana wake, alikimbilia chumbani kwake, na kufika alijonea maajabu.

‘’Kwanza alikuwa amevungwa mwiili mzima nguo nyeusi mithili ya beibui, nilishuhudia vichupa vidogo viwili, kimoja kikiwa na majimaji, (dawa) nusu na chingine kikiwa kitupu,’’alifafanua.

Aidha mzazi huyo alisema, jingine ambalo limemshitua kwa kijana wake huyo ambae ni kiziwi, ni kumuona na kitambaa cheusi shingoni mwake, kukatwa nywele za kichwani na nguo yake ya ndani kuchanwa.

Aliongeza, jingine ambalo alilishuhudia usiku huo, ni kuchinjwa mtoto wake mmoja mdogo mguuni, kunyofolewa nywele zao, na kupewa maelekezo na watu hao kutosema chochote.

Mzazi huyo, alisema baada ya tukio hilo, alimpigia simu sheha wa Shumba vyamboni, ingawa baada ya kujibu kuwa anaogopa usiku huo, alipelekewa usafiri wa pikipiki (bodaboda) na kufika.

‘’Sheha alipomshuhudia kijana wangu hali ilivyo, alitushauri tumpeleke spitali na harakati, zilianza usiku huo, na kulazwa,’’alisema.

Aliongeza kuwa, baada ya kulazwa hospitali hiyo ya wilaya ya Micheweni, siku ya pili yake, majira ya saa 7:00 waliotolewa na kuelezwa kwamba, mgonjwa hana shida yoyote.



Mama huyo alisema, baada ya kufika nyumbani kwao, wakati kijana huyo, alipodai kwenda haja kubwa, aliwamuonesha mama yake, vitu alivyotoka.

‘’Ni kweli mwanangu, baada ya kumaliza haja, aliniita na kunionesha mapande ya damu na kifuko mithili ya glavu, ambacho ndani yake, mlikuwa na vichupa vidogo viwili,’’alifafanua.

Kijana huyo akizungumza kwa njia ya lugha ya alama chini ya familia yake, alisema ni kweli siku ya tukio, aliwaona vijana watatu wakiwa wamefunika nyuso zao na kumfanyia ukatili na udhalilishaji.

‘’Chaajabu mlango na dirisha halikuvunjwa, na mimi nilikuwa chini ya ulinzi wao, badaa ya muda sikujifahamu nilijikuta nipo hospitali,’’alifafanu.

Aidha kijana huyo, alikiri kutokwa na vitu hivyo, na kisha baada ya kuongezeka kwa maumivu walirejea tena hospitali, ingawa baadae walihamishiwa spitali ya Mkoani, kwa uchunguuzi zaidi.

Sheha Shumba vyamboni Time Said Amour, ambae alikuwa wa mwanzo kufika nyumbani kwao kijana huyo, alikiri kuona maajabu hayo siku ya tukio.

Alisema, ni kweli alitoa rai ya kupelekwa spitali, ingawa kwa hatua za awali, walijibiwa kuwa mgonjwa hana tatizo.

‘’Baada ya kurejea spitali kwa mara ya pili, walihamishiwa spitali ya Mkoani, na huko walifanyiwa uchunguuzi, ambapo majibu yake tuliarifiwa tuende baada ya siku tatu,’’alifafanua.

Baadhi ya majirani wakieleza mkasa huo, waliviomba vyombo vya ulinzi na usalama, kufanya uchunguuzi wa kina.

Walisema, changamoto ya kijana huyo kushindwa kujieleza, isiwe chanzo cha kukosa haki yake, kwani kwa maumivu aliyonayo, kuna kitendo kimefanyika.

Mapame Naibu waziri Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Zawadi Amour Nassor, alifika kwa familia huyo na kuahidi kushirikiana nao.



Alisema, serikali inakerwa mno ya wimbi la kuwadhilishaji na kuwafanyia ukatili wanawake na watoto, kwani kufanya hivyo ni kuwazimia ndoto zao.

‘’Serikali haikufurahishwa na tukio hili, na tunaungana na familia na wanaharakati wingine, kwanza kulaani na kuwataka wawe wastahamilivu,’’alifafanua.

Hata hivyo Naibu huyo Waziri, aliitaka familia hiyo kuwa watulivu wakati huu vyombo vya serikali, vikiendelea na taratibu nyingine.

‘’Msikubali kughilibiwa na watu kwa kuwachochea chochea, na endeleeni kuviamini vyombo vya ulinzi na usalama na spitali zetu,’’alifafanua.

Kaimu Mratibu wa TAMWA-Pemba Amina Ahmed Mohamed, alisema wamepokea kwa masikitiko tukio hilo, na kuviomba vyombo vinavyofuatilia kutenda haki.

Alisema, wamekuwa wakiielimisha jamii siku hadi siku, ili kujikinga na matukio hayo au vinapotokea kuviripoti maeneo husika, kama alivyofanya mama huyo.

‘’Kwanza niipe pole familia kwa tukio hili la kusikitisha, lakini nimpongeza mama mzazi kwa ushujaa wake wa kuripoti changamoto hiyo,’’alifafanua.

Hata hivyo aliviomba vyombo vya habari, kufuatilia hatua kwa hatua, tukio hilo hadi mwisho, ili kuona haki imetendeka.

Mkuu wa wilaya ya Micheweni Khatib Juma Mjaja, aliipa pole hiyo, na kuahidi kushirikiana nayo hatua kwa hatua.



Kamanda wa Polosi Mkoa wa Kaskazini Pemba Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi ‘SACP’ William Mwampangale, amekiri kutokea kwa tukio hilo na alisema hawakumbaini muhusika aliyefanya tukio hilo.

‘’Tumekagua tukio hilo na kufanya upelelezi wa kina ingawa hadi sasa hakuna mtu tunaemshikilia hadi leo,’’alifafanua.

Daktari dhamana wa spitali ya Micheweni Khamis Rashid Salim alisema kuwa, mgonjwa huyo alipokelewa na kufanyiwa uchunguzi wa kina, ingawa hawakubaini madhara yoyote.

Alisema kuwa hakukuonesha tofauti yoyote ya dalili  ya kuingiliwa kwa nguvu au kaingiziwa kitu chochote, katika sehemu zake za siri, kama familia inavyodai.

Tukio hilo lililonasibishwa na imani za kishirikiana, lilitokea Mei 15 mwaka huu, majira ya saa 8:00 usiku, kwa watu watatu wasiofahamika wakiwa wameziba nyuso zao, kuingia hadi chumbani cha kijana huyo ambae ni kiziwi na kumfanyia ukatili na udhalilishaji.

Hayo yakijiri, takwimu za Mtakwimu Mkuu wa seikali Zanzibar, imeonesha kuwepo matukio 143 ya udhalilishaji wilaya ya Micheweni, kuanzia mwaka 2023 hadi 2025. wastani wa matukio 48 kwa mwaka.

Maana kwa Zanzibar yote, matukio kwa kipindi hicho, yalikusanywa 4,991, huku mwaka 2023 yakiwa 1,954, mwaka 2024 1,809 na mwaka jana yalikuwa 1,228.

   MWISHO.

 



Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...