Skip to main content

LEO NI SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI, HAYA UNAYAJUA?

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

KILA ifikapo Juni 5 ya kila mwaka, Zanzibar huungana na nchi nyingine, kuadhimisha siku ya mazingira duniani.

 

Siku hii kwa mujibu wa mitandao ya kijamii, ilianzishwa mwaka wa1972, ambapo ni miaka 54, sasa imeshapita.

 

Iliasisiwa wakati wa mkutano wa Stockholm wa Umoja wa Mataifa, tena kuhusu mazingira ya binadamu nchini Sweden.

 

Inafafanuliwa kuwa, pia mkutano huo, ulipitisha azimio la kuunda United Nations Environment Programme (UNEP), ili kuongeza juhudi za kimataifa za kupamba na uhifadhi wa mazingira.

 


Aidha mtandao wa dcc.go.tz unaripoti kuwa, sherehe rasmi ya kwanza, ilifanyika mwaka wa 1973 chini ya kaulimbiu “Dunia Moja Pekee”.

 

Tena tarehe hii, imekuwa jukwaa la kimataifa la kuhamasisha jamii, kuchukua hatua za kulinda , kuhifadhi mazingira na kuendeleza uendelevu wa rasilimali za asili.

 

UNEP, inahimiza jamii kuchukua hatua kali dhidi ya wale wachafuzi, waharibifu wa mazingira wakifafanua kuwa, anariharibu dunia na sio eneo moja pekee, bali ni yote.

 

Taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nalo pia limekuwa likitekeleza kampeni za kupunguza matumizi ya plastiki, ikiwemo kuhamasisha matumizi ya mifuko mbadala rafiki kwa mazingira.

 

Kupitia tovuti ya vpo.go.tz, inafafanua kuwa, siku hii ya leo ya mazingira duniani, huwa na umuhimu mkubwa kwa jamii, ikiwemo kuongeza uelewa wa kimazingira.

 

Umuhimu mwingine ni kuhamasisha watu kuchukua hatua za kulinda mazingira, na kupunguza uchafuzi, ambao athari yake ni kubwa.

 

Siku hii, huwasaidia wanajamii kupata fursa ya kuelewa wajibu wao, katika uhifadhi wa rasilimali za asili, na kuondoa dhana kuwa, miti hujioatea wenyewe.

 

IPI MIKAKATI YA SMZ KULINDA, KUHIFADHI MAZINGIRA

 


Kwa Zanzibar, ipo Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, ndani yake ikiwemo Idara na Mamlaka za kusimamia uhifadhi wa mazingira.

 

Maana hivi karibuni, akisoma bajeti ya wizara hiyo, Kaimu wa Waziri Hamza Hassan Juma, alisema wazi kuwa, uhifadhi wa mazingira ni jukumu la kila mtu.

 

Akafafanua kuwa, hilo litahakikisha kuwa, nchi inadumu, kwa kuzuia uchafuzi wa hewa, maji, na ardhi kupitia upandaji miti, utupaji taka sahihi, na kuepuka uharibifu wa misitu.

 

Akasema serikali yenyewe, haijalala katika kuhakikisha mazingira Zanzibar yanakuwa kama yale ya asili, kwani ipo mikakati kadhaa.

 

‘’Rasimu ya awali ya ripoti ya hali halisi ya mazingira ya miaka mitano ya 2021/2026, imeonesha ongezeko la joto katika bahari, na asidi ambayo imepelekea kufubaa kwa matumbawe,’’anafafanua.

 


Jingine anasema, ni kuongezeka kwa kina cha bahari, uingiaji wa maji ya baharí katika maeneo ya kilimo na makaazi, kupungua uzalishaji wa mwani na kuongezeka kwa kiwango cha uzalishaji taka.

 

Mkakati mwingine uliotajwa na Kaimu waziri huyo ni kuchukua juhudi za kutekeleza, matakwa ya Mkataba wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi (UNFCCC),

 

Tena ni kwa kukamilisha mikakati ya kitaifa, kikanda na kimataifa ikiwemo NDC, NAP pamoja kufanya tathmini ya maeneo 60, yanayoingia maji ya bahari.

 

Jingine ili kukabiliana na uharibifu na uchafuzi wa mazingira, matayarisho ya michoro na gharama za ujenzi wa matuta, kuta za kuzuia maji ya bahari katika maeneo ya Mtangani.

 

‘’Maeneo mingine ni Mtambwe, Ndagoni, Maisara na Bumbwini Mafufuni, pamoja na kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki,’’anaeleza.

 


Ambapo kwa mwaka 2025/2026 kilogramu 2,263, Unguja kilogramu 1,736.5 na Pemba kilogramu 526.5 zimekamatwa, kufuatia doria zinazofanywa.

 

Hamza anaeleza kuwa, baada ya kukamatwa kwa mifuko hiyo, wafanyabiashara walitozwa faini ya shilingi bilioni 9.100, ikilinganishwa na kilogramu 400 zilizokamatwa kwa mwaka 2024/2025.

 

Kaimu huyo Waziri, akasema wakati leo Zanzibar ikiadhimisha siku ya mazingira duniani, kumbe hayo ni mafanikio makubwa, yaliyopatikana katika kupunguza matumizi ya mifuko ya plastiki, kupitia operesheni 54 zilizofanywa.

 


 Juhudi nyingine za serikali, ni uimarishaji wa uhifadhi wa mazingira, ambapo kwa mwaka 2025/2026, maeneo139, yamekaguliwa kiwilaya ikilinganishwa na maeneo 185, kwa mwaka 2024/2025.

 

Tena ukaguzi ukaonesha kuwa, wilaya ya Kati Unguja, iliongoza ikifuatiwa na Chake chake Pemba, kisha Magharibi ‘B’ na Micheweni, kwa kuwa ni maeneo yanayochimbwa rasilimali, zisizorejesheka.

 

 Serikali, imekuwa ikitoa miongozo ya kimazingira iliyosaidia, kupunguza kero, uchafuzi na uharibifu wa mazigira, imetolewa na tathmini 101 za kimazingira, ambapo Unguja ni 68, Pemba 33 zilifanyika,

 

Kwa mwaka wa fedha huu, Afisi hiyo inayo programu kuu ‘P00201’, ya uratibu wa mabadiliko ya tabianchi.

 

Ambapo matokeo ya muda mrefu ni kuwa na mazingira endelevu, pamoja na kupungua kwa athari za mabadiliko ya tabianchi.

 


Zuri zaidi, kwa juhudi za serikali katika mapambano dhidi ya uchafuzi na uharibifu wa mazingira, kwenye programu hiyo, kwa mwaka uliopita, ilitekeleza shughuli kadhaa, ikiwemo kukuza uwelewa wa biashara ya kaboni.

 

Kaimu Waziri huyo, akagusia kuwa, kwa mwaka 2026/2027, malengo yao ni kuimarisha usimamizi na uhifadhi wa mazingira, pamoja jitihada za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

 

Na ndio maana, programu kuu ya uratibu wa mabadiliko ya tabianchi, imeombewa shilingi bilioni 7.909, zikiwemo fedha za mishara na miradi kadhaa ya maendeleo.

 

Kisha Afisi imepanga shabaha kadhaa, ikiwemo kutayarisha kanuni na miongozo ya kimazingira, na kufanya tathmini ya hali halisi ya mmong’onyoko wa fukwe.

 

 Jingine ni kuandaa mandiko ya miradi ya kimazingira na mabadiliko ya tabiachi, pamoja na kukuza uelewa kwa jamii, juu ya mazingira na mabadiliko tabianchi.

 

 JAMII INAONAJE MIKAKATI HII

Ali Khamis Makame wa Makoongwe Mkoani, anasema kama sio kelele za serikali, sasa kusingekuwa na mkoko hata mmoja, baharini.

 

Omar Haji Kassim wa Wambaa, ansema juhudi za serikali ikiwemo kutoa elimu kwao, ni jambo linalosaidia kuhifadhi na kutunza mazingira.

 

Mahamoud Mjabu Hamad wa Kojani Wete, anasema hata uwepo wa sheria, zinazopiga marufuku nyavu za kukokota na mitego haramu, imesaidia.

 

‘’Leo tukiadhimisha siku ya mazingira duniani, walau tunasema, Zanzibar bado kijani kibichi cha asili kipo, tofauti na baadhi ya nchi,’’anasema.

 

Sauda Khamis wa Tundaua Chake chake, anasema hata wao wamefikiwa na juhudi za serikali, maana wamepanda mikokoto zaidi ya 1,500.

 


John Chicomo mwandishi wa habari mbobevu wa mazingira, aliwahi kusema, kalamu ya mwandishi wa habari ikitumika vizuri, inakuwa msaada wa kuhifadhi na kulinda mazingira.

 

Wapo wanawake 2,086 ambao ni wakulima wa kilimo msitu wa shehia nane za Unguja na Pemba, wakiwemo wa shehia ya Mchangamdogo, Wete watanufaika na huduma ya maji ya umwagiliaji wa kilimo chao, kufutia ‘CFP’ kuanza uchimbaji wa visima 24.

 

Taarifa zinaeleza kuwa, wanawake hao walimo kwenye mradi wa miaka mitano wa kukabiliana na mabadiliko tabianchi, kwa hatua za awali CFP, itaanza na uchimbaji wa kisima kimoja kimoja, kati ya shehia hizo nane.

 

CFP kupitia Mkurugenzi wake Mtendaji Mbarouk Mussa Omar, anasema tayari zoezi hilo, limeshaanza kwa uchimbaji wa kisima kimoja, shehia ya Kiuyu Minungwini.

 


‘’Mradi huu wa kukabiliana na mabadiliko tabianchi, asilimia 80 unawalenga wanawake, na asilimia 20 ndio unawangalia wanaume, na ndio maana kati ya wanufaika wote 2749, wanawake ni 2086 na wanaume ni 663,’’anafafanua.

 

Mkulima Mtumwa Makame Shaame wa kijiji hicho, alisema kuwa, kwa sasa kilimo chao kimenusuriwa na uwepo wa mvua, ingawa baadae watahitaji kutekelezewa ahadi hiyo.

           MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...