NA HAJI NASSOR, PEMBA@
WIZARA ya Elim una Mafunzo ya Amali Zanzibar, ni
moja ya wizara tegemezi hapa Zanzibar, katika kufanikisha maendeleo ya kila
siku.
Wizara hii, awali ilikuwa na mfumo wa elimu ya msingi,
sekondari na chuo kikuu pekee, kwa miaka kadhaa.
Kisha, wizara hiyo ikaanzisha mfumo wa Mafunzo ya Amali, ambao
mfumo huu uliwahusu zaidi wale, walioshindwa kuendelea na elimu ya sekondari.
Na kwa wakati huo, elimu ya lazima kwa Zanzibar, iliishia
darasa la kumi (F11), ingawa miaka 1980, elimi ya lazima iliishia darasa la
kumi na moja (F111).
Haja ya kuongeza kiwango cha elimu Zanzibar, haikuja bure
bali, ilitokana na maendeleo ya kielimu ya kidunia, nah apo sasa elimu ya
lazima hadi sasa kwa Zanzibar inaishia kidato cga nne.
JE WALIOSHINDWA KUMALIZA ELIMU YA LAZIMA WAFANYE
NINI
Wizara kwa muda mrefu sasa na kama alivyowahi kusema Katibu
mkuu wa wizara hiyo Khamis Abdalla Said, kuwa hakuna mtoto wa kizanzibari ambae
hatopata elimu.
Hapa, akaenda mbali zaidi, kuwa hilo linawezekana, maana zipo program
za elimu mbadala na watu wazima, ambapo kwa Pemba, kituo chake cha kisasa kipo
Wingwi tokea mwaka 2017.
Akasema Idara ya Elimu Mbadala na Watu Wazima na ina lengo la
kupunguza kiwango cha wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu kwa wanajamii.
Ndio maana anasema kwa mwaka wa fedha 2024/2025, programu hii
ilitengewa shilingi bilioni 3.404, ambapo kati ya fedha hizo shilingi bilioni
1.391 ni kwa ajili ya mishahara na shilingi bilioni 2.013 ni kwa ajili ya
matumizi mengineyo.
Ingawa kwa mwaka jana wa fedha, hadi kufikia Aprili 2025,
jumla ya shilingi bilioni 1.315 sawa na asilimia 39 zilipatikana.
Tena kati ya fedha
hizo, shilingi milioni 233.438 sawa na asilimia 12 ni fedha za matumizi
mengineyo na shilingi milioni mia 1.081 sawa
na asilimia 78 ni kwa ajili ya mishahara.
Imefahamika kuwa, wanafunzi
1,902 wakiwemo wanaume 1,171 na wanawake 731 wamesajiliwa kujiunga na madarasa
97 ya Elimu Mbadala Unguja na Pemba.
Kwa sasa wizara
inaendelea na kazi ya tathmini ya progamu zinazoendeshwa na Idara ya Elimu
Mbadala na Watu Wazima kwa lengo la kuimarisha programu zilizopo na kuanzisha
programu mpya.
Eneo jingine wizara inaendelea kuwajengea uwezo vijana, katika
fani mbalimbali ambapo wapo 150, Unguja 75 na 75 Pemba, wamepatiwa mafunzo ya
ushoni, vijana 42 wakiwemo wanaume 35 na wanawake saba wamepatiwa mafunzo ya
uchongaji wa samani pamoja na ukarabati wa madawati yaliyoharibika.
Ikafahamika kuwa, matokeo ya muda mfupi ya program hiyo ni wanafunzi
1,902 wakiwemo wanaume 1,171 na wanawake 731 wenye umri kati ya miaka 7 hadi 14,
waliokuwa nje ya skuli wamerejeshwa masomoni Unguja na Pemba.
YEPI
MATUNDA YA KIUTUO CHA ELIMU MBADALA WINGWI?
Vijana wa kike, wametajwa sasa kujisomea
ufundi wa uunganishaji umeme majumbani, kupitia Kituo cha Elimu Mbadala cha Wingwi
Pemba, ambapo hapo awali fani hiyo, ikisomwa na wanaume pekee.
Maana Kaimu mkuu wa Kituo hicho Mussa
Faki Iddi, anasema wastani wa vijana wa kike 25 kila mwaka, huwapokea kituoni
hapo, wakiomba fani ya ufundi wa umeme wa majumbani.
Anaongeza kuwa, fani hiyo pamoja na
ushoni wa nguo ndio pekee, ambazo zimekuwa na idadi kubwa ya wanafunzi.
Kumbe kuanzia mwaka 2019 hadi sasa,
wanawake wanaojiunga na kituo hicho, wapo wastani wa 25, ambao wanaomba ufundi
wa umeme wa majumbani.
‘’Fani hapa zipo kadhaa ikiwemo ya
ushoni wa nguo, upambaji maharusi na uchoraji piko, fundi bomba ingawa kwenye
fani ya umeme, sasa na wanawake wamekuwa wingi,’’anafafanua.
Fani nyingine zinazobeba wanawake
wingi ni ushoni wa nguo za aina mbali mbali kwa kutumia cherhan.
‘’Fani ya pili ambayo ninaiyona
inawanafunzi wingi ni ushoni wa nguo, ambapo kila mwaka nayo hubeba kundi kubwa
la wanafunzi,’’anafafanua.
Akizungumzia sifa za kujiunga na
Kituo hicho, ni pamoja na wale walioshindwa kupata elimu kabisa katika maisha
yao, kwa changamoto moja ama nyingine.
Sifa nyingine ni kwa wale walioshindwa
kumaliza elimu ya msingi, wakiwa walikatisha njiani, kupata ujauzito au
waliacha kwa mifumo ya matokeo mabaya ya maisha.
‘’Tunazingatia umri, ambapo ni
kuanzia miaka 17 na mwanafunzi asizidi miaka 23, akija hapa atasomea ufundi na
masomo mingine kwa miaka mitatu bure,’’anafafanua.
Kihusu vifaa vya kujifunzia, anasema
vipo kwa wingi, ingawa hutokezea changamoto ua uhaba pindi idadi ya wanafunzi,
ikiongezeka, katika mwaka.
‘’Hapa wanafunzi wanapata
kufanyakazi wa vitendo, iwe ni wale wa upishi, uchoraji piko, fundi bomba,
uchongaji na wakimaliza wanakuwa vibarua wazuri,’’anafafanua.
Sasa akawataka wazazi na walezi,
kuendelea kuwaandikisha vijana wao katika kituo hicho, ili kila mmoja aweze
kujiajiri katika maisha yake.
Wahitimu waliopita kituoni hapo, akiwemo
Mohamed Issa Jafari, ambae kwa sasa amekuwa fundi wa uunganishaji wa umeme
majumbani, anasema anaendelea kujiajiri mwenyewe.
‘’Kwa hakika kituo kile cha Elimu
Mbadala kwangu ni mkombozi, maana nilishakata tamaa ya maisha, ingawa baada ya
kujiunga na kumaliza, sasa nimejiajiri,’’anasema.
Mhitimu Maryam Haji Kombo wa
Micheweni, anasema kwa sasa ni fundi mzuri wa nguo wa kike, na anaowateja hadi mikao
ya Tanzania bara.
‘’Wapo wateja wangu hadi mikoa ya Arusha,
Tanga, Dar-es Salaam, Morogoro ambao nawashonea nguo za watoto wao,’’anaeleza.
Mwanafunzi aliyejitambulisha kwa
jina moja la Hidaya, anasema kituo hicho ni kizuri mno, ikiwa serikali
itaendelea kukiwezesha vifaa vya mazoezi.
Mohamed Haji Hamza na Mayasa Issa
Hija ni wazazi ambao watoto wao, wameshamaliza ufundi wa aina mbali mbali, wanasema
kituo hicho, kinafaa kuongezea chingine.
‘’Kwa mfano, sio kituo kuwepo Wingwi
pekee, bali kila wilaya kinatakiwa kiwepo, ili kuwarahisishia wingine kunufaika
na huduma hizo,’’anafafanua.
Hili la uwepo wa vituo hivi
linachangiwa, na nia ya thati ya serikali ya awamu ya nane, chini ya uongozi wa
Dk. Hussein Ali Mwinyi.
Maana, wizara hiyo kwa sasa
imeshaongezewa bajeti yake kuu kutoka shilingi bilioni 265.5 kwa mwaka wa fedha
2021/2022 hadi kufikia shilingi bilioni 830 mwaka 2024/2025 sawa na ongezeko la
asilimia 212.6.
Mwisho

Comments
Post a Comment