Skip to main content

HAYA HAPA YALIOJIFICHA NDANI YA 'GREAT WALL' YA CHINA

 


NA HAJI NASSOR, BEIJING@@@@

NI wastani wa saa 1:45 kwa mwendo wa gari isiyo kuwa ya umma, kutoka katikati ya jiji la Beijing, hadi iliko milima hiyo.

Milima hiyo, kwa hakika ni sawa na ile inayooko baadhi ya mikoa ya Tanzania bara, mfano mzuri ni Mwanza.

Maana imejengwa kwa mawe (majabali makubwa), ikiwa imezungurikia nje kidogo ya Beijing, na hata ardhi yake ikiwa ni mfumo wa mawe.

Wataalamu wa kichina, waliona milima hiyo isibakie bure, maana kwa zaidi ya miaka 100, sasa tokea kuasisiwa imekuwa ni sehemu ya kutunisha mfuko wao wa pato la ndani.

Ni eneo lenye utulivu kiasi, likiwa limezungurukwa na milima ya asili, na kwa hakika ingekuwa vigumu kupitisha barabara, pingine kupata upande wa pili.

NAMNA MILIMA HIYO ILIVYOGEUZWA ENEO LA KITALII

Zipo zaidi ya mita 5,500 (sawa na umbali wa viwanjwa 55 vya mpira wa miguu), ambavyo zilianza kujengwa vidaraja kuanzia chini.

Tunaelezwa kuwa, ujenzi huo ulijengwa kwa matofali maalum ya mawe, kwa mtindo wa kama vidaraja na kushukia ama kupandia mlima.

Pembezoni mwake, mumewekwa ukuta ulioshikamana na vyuma vizito, ili kumuhakikishai usalama mpanda mlima huo, baada ya kulipa wastani wa shilingi 5,000 kwa fedha ya Tanzania.



Unakisiwa kuwa, upana wake ni kati ya mita 4 hadi 5, baadhi ya maeneo yamenyanyuka kati ya mita 7.8 hadi mita 14 kwa nje, kulikoshikamana na ardhi ya mawe.

Namna ya upandaji wa vidaraja hivyo, unaweza kupumzika pasipokuwa na kibanda, kadiri utakavyopenda, ingwa kila wastani wa urefu wa viwanja viwili vya mpira wa miguu (mita 200), vipo vibanda vya kumpunzikia.

Ijapokuwa huzuiliki ikiwa afya ya kuanza mwanzo na kumalizia mwisho huna, lakini iwapo utafikia mwisho unakabidhiwa nishani maalum, yenye mfano wa dhahabu na wahusika.

Kumbuka, ushahidi wa kuanza mwanzo na kumaliza, kwa sasa unachungwa na ulinzi wa kamera maalum, ambazo zimeunganishwa, na kurahisisha kumuona kila mmoja.

Hapo wageni kutoka mataifa mbali mbali na hata wenyeji hufurika kwa wingi, kupanda ukuta huo, ambao maarufu huitwa ‘great wall’.

Kwa kawaida, wenyeji wetu wanasema idadi ya watu huongezeka mara dufu kwa siku za baridi, ili watu kuzalisha joto la mwili, hasa waakati wa kupanda, kwa kule kutumia nguvu za kunyanyua miguu.

‘’Na hata wanafunzi, wazee wenye magonjwa ya miguu, maradhi ya kupumua na wageni hata utawaona wanatembelea ukuta huu, ambao kwetu sisi wachina unahistoria yake,’’anasema muuza kofia Yeu Is Kwu.

Anasema, msimu wa baradi hujipatia fedha nyingi hadi Yuwan 2,000 kwa siku, baada ya kuuza kofia zenye jina na nembo ya China, kwa wageni na wenyeji.

‘’Ukipanda mlima huu, inapendeza uwe na kofia na ujiti maalum ‘mop’ ili kupata kasi ya kupanda na kupata kisaidizi wakati wa kushuka,’’anaeleza.

Muuza chai na mahindi eneo hilo la chini ya ukuta huo, Yu Usy Sun, anasema hakuna siku wanaofika eneo hilo watu wasizidi 80,000 wakipanda ukuta huo.

Anasema wageni, wazee na wanafunzi ndio wamekuwa hawaadimiki eneo hilo, wakija kijifunza mambo kadhaa, ingawa kwa wazee ni uchangamshaji wa mwili.

Mwananchi aliyetembelea eneo jilo Li Tes Yu (55), akizungumza kwa msaada wa mtoto wake kwa lugha ya kiingereza, anasema amekuwa na shida ya kupumua kwa mwezi mmoja sasa.

‘’Hapa sikuja kama mtalii wa ndani, nimekuja kutoka Shanghai kutimiza ushauri wa kitabibu wa kufanya mazoezi na kutembelea milimani,’’anaeleza.

‘’Wewe ni nani, ni mwandishi wa habari, umetoka wapi, Tanzania, mbona upo hapa, ni kutembelea kama mtaalii, aliniuliza, ingawa yeye akasema ni kufuata tiba.



Kumbe maeneo kadhaa ya China yako tambarare, na ndio maana, wanaotaka kufanya mazoezi kwa nguvu na kasi wapo wanofuata milima hiyo.

Mwenyeji wetu tuliyetoka nae katikakati ya jiji la Beijing Magic, anasema kila mmoja, hufika kwenye milima hiyo kwa azma yake mwenyewe.

Anasema, wageni ni kwa ajili ya kutembelea kwa mara ya kwanza au ya pili, ingawa wanafunzi kusoma kwa vitendo na wapo baadhi ya wazee na wagonjwa kutekeleza ushauri wa daktari.

Mc. John Gabreil kutoka Natharland, anasema hii ni mara yake ya kwanza, kufika katika eneo hilo, ambalo awali alikuwa analisoma kupitia mtandaoni pekee.

‘Ni eneo zuri ambalo wenzetu wa serikali ya China, wamelitumia na sasa limekuwa likiingia kwenye rikodi ya dunia kiutalii, ingawa ni jambo la kutengeneza,’’anasema.

KUNDI LA WAANDISHI WA HABARI KUTOKA AFRIKA

Momodou Jow kutoka Gambia anasema, ni eneo la kujifunza kwa mataifa mingine ya Afrika, namna ya kutumia malighafi kuchochea uchumi.

Mwandishi Aggrey Mutambo wa Kenya, anasema ni eneo zuri lililotumia utaalamu wa hali ya juu, namna milima ilivyosarifiwa na kuwa sehemu ya utalii.

‘’Milima ipo kila mahali na hasa ndani ya mataifa ya Afrika, lakini uwezo mdogo wa fedha za uwekezaji na utaalamu hafifu, imebakia kama ilivyo,’’anafafanua.

Mwandishi Yakali Tariku kutoka Ethiopia, anasema ijapokuwa ardhi ya eneo hilo ni la mawe na kukubalika kwa namna yoyote ambayo unataka, lakini kwanza ubunifu ulitumika kwa kiwango kikubwa.

 ‘’Kwenye mataifa ya Afrika milima ipo, lakini ni yenye kuporomoka, maana maumbile ya ardhi zenyewe ni mchanga laini, ingawa kwa hapa jiwe limetawala,’’anasema.

Mtaalamu wa sayansi ya jamii kutoka taasisi ya Magharibi mwa bara la Asia na Afrika, anayefaniya kazi zake nchini China Professa: He Wenping, anasema ukuta huo juu ya milima, ni sehemu ya kuimarisha historia ya ukombozi wa China.



Inawezakana misaada ambayo mataifa ya Afrika wameshayapokea kutoka China, yenye thamani ya dola bilion 615.8 kuazia mwaka 1950 hadi mwaka 2018, ilichangiwa na pato katika milima hiyo pia.

 Maana ukombozi wa China chini ya chama tawala cha CPC, kwa wakti huo wa kuanzia mwaka 1949 chini ya Chamen Mao, ilikuwa inabuni kila mbinu kuhakikisha, inajiendesha.

Kwani China ilikuwepo tokea mwaka 2070BC, (kabla ya ukiristo), huku chama cha kikomonisti ‘CPC’ kikiwa ndio mkombozi wa wananchi tokea kilipoasisiwa zaidi ya miaka 100 sasa.

Katika ziara ya eneo hilo, waandishi wa habari wa redio, tv, mitandao ya kijamii na magazeti waliopo nchini China, walitembelea milima hiyo, kama sehemu ya mafunzo ya siku 21.

Ni waandishi wa kutoka Gambia, Zambia, Kenya, Ethiopia, Tanzania Zanzibar na wenyeji China, ambao pia walishatembelea, makumbusho ya chama cha CPC, dawa asili, ofisi za star times, ofisi za uchapishaji wa gazeti la China-Aftika na dawa asili.

Mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...