Skip to main content

CHINA: WAANDISHI WA HABARI AFRIKA SAIDIENI KUKUZA UCHUMI

 



ZUHURA JUMA NA HAJI NASSOR, BEIJING@@@@

WAANDISHI wa habari wa nchi za Afrika, wametakiwa kuendelea kujifunza lugha mbali mbali, ili kusaidia kukuza uchumi katika mataifa yao.

Akifungua mafunzo ya siku 20 katika Ukumbi wa Hoteli ya RoyalLink ZiYu, Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Mawasiliano (CICG) Han Likiang alisema kuwa, kujua lugha mbali mbali ni muhimu katika kukuza uchumi wa nchi, hivyo kuna haja kwa wanahabari kujifuza zaidi.

Alisema kuwa, ili uchumi ukue unahitaji mambo mbali mbali ikiwemo waandishi wa habari kujifunza lugha ambazo zitawasaidia kuandaa makala, vipindi na habari zenye tija hususan zinazogusa viashiria vya ukuaji wa uchumi wa ndani.

‘’Watakapotumia lugha mbali bali itawasaidia kuwahabarisha watu wengi duniani ambao wanaweza kuvutia hata wawekezaji na wageni, ambayo ni miongoni mwa kukuza uchumi wa ndani,’’ alisema.

Akizungumzia umuhimu wa CICG kuandaa mafunzo hayo ni kuendeleza uhusiano wa kimataifa wa china na mataifa mengine ya Afrika kwa lengo kubadilishana uzoefu wa kisera za kiuchumi miongozi mwa mataifa hayo.

‘’Mafunzo haya yatasaida sana kuendelea kukuza ushurikiano kwa mataifa ya Afrika, kwani watatembelea sehemu mbali mbali ambazo zitawasaidia kutangaza fursa zilizopo katika nchi hii,’’ alisema.

Katika hatua nyingine Naibu Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa kabla ya kuanza kwa mafunzo hayo ya kuwaleta pamoja washiriki wa mataifa mbali mbali, CICG lilikuwa na utamaduni wa kuwafuata waandishi katika mataifa yao.

‘’Lengo la kuwaweka pamoja ni kuona kwamba tunakutana na kujuana, jambo ambalo litasaidia kufanya kazi zetu kwa ushirikiano, huku tukiamini kwamba ni sehemu ya juhudi ya kukuza uchumi katika nchi zetu,’’ alisema.

Mapema Mkurugenzi wa Idara ya Mafunzo ya kimataifa kutoka Shirika la CICG Feng Yin alieleza kuwa, mafunzo hayo ni fursa pekee kwa waandishi wa habari katika kukuza uchumi wa nchi yao, hivyo wanapaswa kuchukua juhudi za makusudi kuhakikisha nchi inapata maendeleo.

‘’Watakapoandika habari mbali mbali zitakazosaidia kukuza uchumi na nchi itapata maendeleo kwa sababu wananchi wanaamini sana vyombo vya habari,’’ alisema.

Akizungumza kwa niaba ya washiriki wenzake, mwandishi wa habari kutoka nchini Zambia, Emeldah Libaga alisema, mafunzo hayo ni muhimu kwao katika kuongeza uhusiano wa kutambua sera za kiuchumi za China ambazo zitasaidia kutanua wigo katika mataifa yao.

‘’Tunalishukuru sana Shirika hili kwa kutuweka pamoja na kutupa mafunzo, hii itatusaidia sana kuongeza uelewa wa masuala mbali mbali ya kiuchumi,’’ alifafanua.

Katika mafunzo hayo yaliyoandaliwa na CICG kwa ufadhili wa Wizara ya Fedha ya China, ambalo limeanzishwa mwaka 1949 yamewashirikisha waandishi kutoka mataifa kadhaa ikiwemo Tanzania Zanzibar, Zambia, Gambia, Kenya, Gana na wenyeji wa China.

MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...