Skip to main content

SIKU 180, ZABEBA MATUKIO 610 YA UDHALILISHAJI ZANZIBAR

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

MATUKIO 610 ya ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na watoto, yameripotiwa kutokea  Zanzibar, kwa kipindi cha miezi mitatu mitatu ya mwaka 2021 na 2022, taarifa za ofisi ya  Mtakwimu Mkuu wa serikali Zanzibar, zinaeleza.

Kwa miezi ya Januari hadi Machi mwaka 2021, Ofisi hiyo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Zanzibar, ilikusanya matukio 363, ingawa kwa mwaka jana, katika kipindi hicho matukio hayo yaliripotiwa 247, upunguzu wa matukio 116.

Takwimu hizo zinafafanua kuwa, kwa mwaka 2021 kwa miezi mitatu ya mwanzo, mwezi ulioongoza ni mwezi wa Machi ulioripoti matukio 141, ukifuatiwa na mwezi wa Januari matukio 122 na Febuari matukio 100.

Kwa mwaka 2022, mwezi uliokihiri kwa matukio mengi ni mwezi Febuari, ulioripoti matukio 100, huku mwezi Machi ukiripoti matukio 82, wakati mwezi wa Januari yakishuka kwa 17, na kuripoti matukio 65 pekee.

Taarifa hiyo ikeleza kuwa, mwezi wa Febuari kwa miaka yote miwili, iliripoti matukio sawa ya 100 kwa wanawake na watoto kudhalilishwa kwa Unguja na Pemba. 

Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba Juma Saad Khamis, alisema moja ya vyanzo vya matukio hayo ni mporomoko wa maadili, uliozoeleka ndani ya jamii.

‘‘Lakini hata kwa jamii, kutokuwa tayari kutoa ushahidi makamani, na kusababisha kesi kufutwa, huchangia matukio hayo kuendelea,’’alieleza.

Kwa upande wake, Hakimu wa mahakama amaalum ya kupambana na makosa ya udhalilishaji mkoa wa kusini Pemba Muumini Ali Juma, alisema chanzo ni wazazi kuacha malezi ya pamoja.

Mwanasheria dhamana wa Mahakama kuu Zanzibar Ali Rajab, anasema kuongezeka kwa matukio hayo, ni jamii kukosa elimu ya kisaikolojia, na kutoyapa uzito matukio hayo yapotokezea.

Mzazi Saumu Haji Said wa Machomane anasema, kutotumika kwa sheria kama zilivyoandikwa, baada ya mshitakiwa wa udhalilishaji kutiwa hatiani, ndio sababu ya kuongezeka.

‘’Wahalifu hawana woga wanajua kuwa, atafungwa miaka saba, 10 au 20 na atatumikia nusu yake, baada ya muda anatoka chuo cha mafunzo,’’anasema.

Wakili wa kujitegemea Pemba Zahran Mohamed Yussuf, anaona chanzo ni harufu ya rushwa katika baadhi ya vyombo vya sheria, kunakopelekea watu kuachiwa huru.

Mtoto Hidaya Haji Mkame wa Mizingani amesema chanzo cha matukio hayo, ni wazazi kutowajibishwa kisheria, ikiwa tukio la udhalilishaji wa mtoto wake kuna uzembe.



Mkurugenzi mtendaji wa Chama cha Waandishi wa habari wanawake Tanzania ‘TAMWA’-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, anasema moja ya athari ya matendo hayo, ni kupata madhara ya kiakili kwa muathiri.

‘’Mtu aliyedhalilishwa na hasa mtoto, hata hamu ya kuendelea na masomo hana, kujichanganya na wenzake huondoka, maana kila wakati anajihisi mpweke,’’anasema.

Aziza Iddi Ali anasema, ni kupungua ufahamu wake hasa kwa wale walioko masomoni, na wakati mwengine hadi kupekekea utoro.

Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC' Harusi Miraji Mpatani, anasema athari nyinge ni kupewa majina mabaya na wenzake.

Mtoto Khamisuu Is-haka Ngwali wa Msingi Mkoani, anasema hata kusemwa ovyo na wenzake, moja ya athari, ambayo mtoto aliyebakwa anaipata.

Daktari Mohamed Ali Jape anasema, kupoteza haiba ya viungo vya mwili, ndio athari kubwa inayowaumiza watoto hasa kutokana na umri wao, kutokuwa tayari kupokea tendo hilo.   

Jaji wa mahakama kuu Zanzibar Mshibe Ali Bakari, amesema ni kwa washtakiwa kupewa adhabu ndogo lakini yenye kufunza, inaweza kusaidia.

Mkurugenzi wa Mastaka Zanzibar Mgeni Jailan Jecha, alipendekeza kuwa, elimu ya kiroho inahatajika kwa jamii, ili kumuogopa Muumba.

Mwanaharakati wa haki za wanawake na watoto Tatu Abdallah Msellem, anasema kama kutakuwa na adhabu kali kwa wakosaji, wengine wataogopa.

Mtoto mwenye ulemavu Maimuna Himid Mkombe wa Uwandani Chake chake, anasema kama adhabu ya kifungo cha maisha itatolewa, itakuwa dawa.



Sheikh Said Ahmad kutoka Ofisi ya Mufti Pemba na Mchungaji Benjamin Kissanga wanasema, elimu bado inahitaji kwa waumini, ili kujua athari ya wanayofanya kidini.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, anasema kama sheria zikifanyiwa marekebisho, zile zinazokwaza, inaweza kusaidia watu kujenga hofu.

                     Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch