Skip to main content

JINSI VIFUNGU VYA SHERIA YA MAGAZETI ZANZIBAR VINAVYOUWEKA CHINI YA ULINZI UHURU WA HABARI

 



 

NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

 

SHERIA nambari 5 ya Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu ya mwaka 1988, ambayo imefanyiwa marekebisho mwaka 1997, inavyo vifungu 81, vilivyobebwa na sehemu 1O.

 

Pamoja na marekebisho hayo yaliyofanywa miaka 9, baada ya sheria hiyo kupita na sasa ikielekea kuwa na umri wa miaka 21, lakini bado kuna vifungu vinatajwa kuuweka chini ya ulinzi uhuru wa habari Zanzibar.

 

Ndivyo ilivyo kuwa sheria hiyo, kwa wakati huo na miaka hiyo ilitungwa na kisha kusainiwa na rasi wa wakati huo wa Zanzibar kwa nia nzuri, ingawa kwa sasa uzuri huo haupo tena.


WADAU WATAKA SHERIA MPYA

Ndio maana, kwa mfano Shirika la Internews Tanzania kwa kushirikiana kwa karibu na TAMWA-Zanzibar na wakati mkubwa na Baraza la Habari Tanzania MCT, wamekuwa wakita sheria bora na fariki Zanzibar.

 

Kwani Mratibu wa Internews Tanzania ofisi ya Zanzibar, Zaina Mzee, anasema sheria hiyo kwa sasa, inakinzana pakubwa na dhana ya demokrasia na utawala bora unaochapuzwa na uhuru wa habari duniani kote.

 

‘’Ni kweli sheria hiyo kwa wakati wake, ilikuwa mzuri mno lakini kwa wakati huu, sasa sisi Internews na wenzetu TAMWA-Zanzibar tunashirikiana ili kuona tunakuwa na sheria moja ya habari Zanzibar,’’anasema.

 





Anasema waandishi wa habari wa Zanzibar ni sawa na wengine duniani kote, hawana haja kuwekewa sheria yenye vifungu vya maajabu na wakati mwengine vinavyozorotesha utawalabora na uwajibikaji.

 

‘‘Kwa mfano ndani ya sheria hiyo nambari 5 ya Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu ya mwaka 1988, ambayo imefanyiwa marekebisho mwaka 1997, kuna vifungu haviendani na hali ya sasa,’’anasema.

 

Alikishangaa kifungu cha 14 (1) kinachomlazimisha mchapishaji gazeti lililochapwa Zanzibar kwa kila siku na kwa gharama zake, kuwasilisha nakala mbili kwa Mrajisi wa magazeti.

 

Akaeleza kuwa, kinachosikitisha kuwa nakala hizo ziwe kwenye aina ya mfumo, karatasi zile zile zilizochapishwa kwa ajili ya kusambaazwa au kuuzwa.

 

‘’Sheria hii kwenye kifungu hichi, ni sawa na kuuweka chini ya ulinzia uhuru wa habari Zanzibar, maana pamoja na gharama anazopata mchapishaji wa gazeti, anatakiwa tena kuingia gharama za kuwasilisha nakala mbili,’’anafafanua.

 

Mkurugenzi wa TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, anasema biashara ya magazeti ilivyongumu, kisha mchapisha sheria inamlazimisha kuwasilisha nakala mbili bure, hili sio sahihi.

 

Anasema, hili ni tatizo na linahitaji kutafuatiwa dawa ya haraka, maana Mrajisi alipaswa alinunue kwa gharama zake, ili kumsaidia mtu aliyeekeza kwenye sekta ya habari.

 

‘’Kwa hakika uwepo wa vifungu kama hivi na nvyengine, ni kuunyong’onyesha uhuru wa habari na uwajibikaji kwa waandishi hapa visiwani,’’anasema.

 

Kifungu hicho cha 14 (3) kinafafanua kuwa nakala hizo zitawekwa kwa ajili ya kumbu kumbu, katika eneo au mahala maalum.

 


Kifungu chengine kilichotajwa na wadau na waandishi wa habari kuwa si rafiki kwa uhuru wa habari Zanzibar ni kile cha 30 na 31.

 

Kifungu cha 30 cha sheria hiyo, kinafafanua uwezo wa waziri kusimamisha uchapishaji wa gazeti lolote ndani ya Zanzibar lililosajiliwa chini ya sheria hii.

 

’Endapo waziri ataona kwamba ni kwa maslahi ya umma, au ni kwa maslahi ya amani na utulivu, atatekeleza kwa kuamuru usimamishwaji wa kuchapishwa kwa gazeti husika,’’kinafafanua kifungu hicho.  

 

Kwenye kifungu cha 31 kimempa waziri husika, uwezo wa kukataza uchapishaji wa gazeti, ingawa kwa ushauri wa Bodi, ataona kukatazwa huko ni kwa maslahi ya umma au ni kwa maslahi ya amani na utulivu.

 

Hapa mwandishi Salma Said aliwahi kusema kuwa, sheria kumpa uwezo mkubwa waziri sio sawa, maana wapo wengine wanaweza kufanya uamuzi huo, kwa maslahi yao binafsi.

 

Akahojiwa kuwa, ndani ya sheria hiyo neno maslahi ya umma hayana tafsiri ya kujitosheleza, hivyo inaweza kujitokeza kwa waziri kuzuia uchapishaji kwa maoni yake.

 

Mwandishi Amina Massoud Jabiri wa redio Jamii Mkoani, anasema kwa vile suala la kusambaaza na kupata habari ni haki ya kikatiba, sio busara kupewa uwezo waziri husika.

 

Mratibu wa Internews Tanzania ofisi ya Zanzibar Zena Mzee, anasema waandishi wa habari, hawatakiwi kuingiliwa kama zilivyosekta nyingine, wakati wanapokuwa wanatekeleza wajibu wao.

 

‘’Mbona daktari anapokuwa anatibu hakuna anayemuingilia, Polisi akilinda usalama yuko huru, sasa iweje kwa sekta ya habari iwekewe vifungu vikali,’’anahoji.

 

Mwandishi Najat Omar wa the Chanzo online anasema, wakati ndio huu kwa Zanzibar kuwa na sheria inayokwenda sambamba na ulimwengu wa leo.

 

Mwanasheria wa Shirika la Magazeti ya serikali Zanzibar Juma Khamis Juma, anasema sheria inapotoa fursa ndogo, inaweza kuzaa janga wakati wa utekelezaji.

 

Mchambuzi wa sheria za habari Zanzibar Imane Duwe, anasema, kazi inayofanywa na waandishi sio kwa maslahi yao, bali ni utekelezaji wa haki ya kikatiba.

‘’Haki za kikatiba wakati zinapotekelezwa hazitakii kuwekewa masharti mazito, kama yalivyo kwenye kifungu cha 14, 26, 27, 30 na 31 cha sheria ya nambari 5 ya Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu ya 1988,’’anasema.

 

Hata kifungu cha 27 (1) ni miongoni mwa vifungu kinachompa Mamlaka Ofisa yeyote wa Polisi, kukamata gazeti lolote, popote litakapoonekana limechapwa au kuchapishwa au ambalo kwa maoni yake tu, atalituhumu kuchapishwa kinyume na sheria.

 

Ambapo kifungu cha 27 (3) pia kinampa Mamlaka hakimu kumuamuru Ofisa yeyote wa cheo cha mkaguzi au zaidi, ikiwa ana sababu ya maana ya kuamini kwamba, atachelewa kupata hati ya upekuzi anaweza kutekeleza uwezo alio nao kwa mujibu wa sheria.

 

Vifungu hivi kwa nyakati za sasa, havipaswi kuwepo katika sheria hiyo kutokana na kuwa sio rafiki kwa uhuru wa vyombo vya habari nchini.

 

Meneja wa radio Jamii Micheweni Ali Massoud Kombo anasema, sio sahihi kwa Ofisa Polisi kupewa mamlaka hayo, kwani uhuru wa habari, itakuwa bado haujakuwepo nchini.

 

"Ikiwa afisa atakuwa na ugomvi na mwandishi, anaweza kufanya upekuzi au kukamata gazeti, hali ambayo itasababisha taharuki katika vyombo vyetu,’’ anasema.

 


Mwanasheria wa serikali Ali Amour Makame anasema kwamba, sio sahihi kifungu hicho kuwepo kwa sababu, kisheria halitakiwi kuwepo neno ‘kwa maoni yake’ na haifai kwa Afisa Polisi kupewa mamlaka hayo kwani, habari inaweza kuwa sahihi kwa mujibu wa maadili yao, lakini yeye isimfurahishe.

 

‘’Elimu za Polisi tunazijua, iweje wapewe mamlaka hayo kwa taaluma nyengine?, hii sio sahihi, kinachoshangaza zaidi ni pale sheria hii ilipoeleza kwamba kwa maoni yake, akituhumu, hichi kitu hakipo kwenye sheria’’, anafafanua.

 

Fat-hiya Mussa Said ambae ni Mratibu wa TAMWA Pemba anaefahamisha, Polisi wana mamlaka ya kulinda raia na mali zao na kulinda amani ya nchi, ndio maana walipewa mamlaka hayo, lakini kwa wakati wa sasa kifungu hicho kinahitaji maboresho.

 

"Kitakapoboreshwa kifungu hicho, waandishi watakuwa huru kufanya kazi zao za kihabari na wananchi watapata habari, uhuru wa kutoa maoni na kujieleza", anasema.

 

Afisa Mdhamini MCT Zanzibar Shifaa Said Hassan anasema, pamoja na kuzieleza sheria hizo na mapungufu yake tangu 2010, lakini bado inaendelea kutumika, jambo ambalo linawapa wakati mgumu katika kuendeleza tasnia ya habari nchini.

 

"Haya mamlaka aliyopewa Ofisa Polisi sio sahihi kwa kweli na wala haileti picha nzuri, mimi naona ni udhalilishaji wa waandishi na vyombo vyetu, tuendelee kuzisemea sheria hizi ili vifungu vinavyotukwaza viondoshwe", anafafanua Shifaa.

 

NINI KINAFANYIKA

Mkuu wa taaluma wa Chuo cha uandishi wa habari na mawasiliano ya Umma Zanzibar Imane Duwe, anasema kwanza kufutwa kwa sheria hiyo kongwe na kuwa na sheria rafiki kw auhuru wa habari.

 

Mwananchi Asha Salim Ali mkaazi wa Wete anasema, ili kuwe na uhuru wa vyombo vya habari kuna haja ya kuvifanyia maboresho vifungu vyote vinavyominya uhuru wa habari.

 

Khamis Mohamed mkaazi wa Gombani Chake Chake anafahamisha kuwa, Ofisa wa Polisi asipewe mamlaka hayo na badala yake iundwe bodi maalumu ya kuweza kuchunguza tuhuma na itakapothibitika chombo kimekiuka sheria ndipo kichukuliwe hatua.

 

"Mimi iliyonishangaza ni hii kwamba Ofisa Polisi hata akituhumu tu anaweza kukamata gazeti au hata kitabu cha mwandishi, kwa kweli hii sio sahihi hata kidogo", anafahamisha.

 

Mratibu wa Iternews Zanzibar Zaina Mzee, anasema kwa sasa wako bega kwa bega kati yao na TAMWA-Zanzibar na waandishi wa habari, ili kuviibua vifungu kandamizi.

 

Anasema anaamini serikali hii ya awamu ya nane inayoongozwa na Dk. Hussein Ali Mwinyi, itachapuza upatikanaji wa sheria mpya na rafiki ya habari Zanzibar.

 

               MWISHO.

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch