Skip to main content

WADAU, WAANDISHI, WAMILIKI WATAJA SABABU KUTAKA SHERIA MPYA YA HABARI ZANZIBAR

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

KWA zaidi ya miaka 10 sasa wadau wa habari wamekuwa wakipaza sauti zao kutaka sheria mpya na bora ya habari Zanzibar.

Wadau mfano Baraza la Habari, TAMWA-Zanzibar na hata Shirika la Internews Tanzania ofisi ya Zanzibar wamekuwa wakiungana na waandishi kuhakikisha sheria moja ya habari inapatikana.

Mratibu wa Internews ofisi ya Zanzinar Zaina Mzee, anasema moja ya sababu ya kutaka sheria mpya ya habari Zanzibar, ni kuona zile mbili zilizopo zinafutwa.

‘’Ipo sheria ya Tume ya Utangaazaji Zanzibar nambari 7 ya mwaka 1997, pamoja na marekebisho yake, pamoja na ile ya sheria nambari 5 ya Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu ya mwaka 1988, ambayo imefanyiwa marekebisho mwaka 1997.

 

Anasema sheria hizo, zimekuwa na vifungu ambavyo sio rafiki kwa kuimarisha uhuru wa habari pamoja na uhuru wa kujieleza katika jamii.

 

Anaeleza kuwa, pamoja na ukongwe wake sheria hizo mbili kuu zinazosimamia vyombo vya habari, lakini kubwa zimekuwa zikiwabana waandishi katika kutekeleza haki ya kikatiba.

 

‘’Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kwenye kifungu chake cha 18 kimeweka wazi suala la kupata, kusambaaza habari habari tena bila ya kujali mipaka ya nchi,’’anasema ilivyoeleza sehemu ya katiba.

 

Mkurugenzi wa TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali anasema, kwa wakati uliopo sasa Zanzibar na duniani kote, lazima suala la kuwepo kwa sheria au vifungu vyenye ukakasi havina nafasi.

 

‘’Kwa mfano kwenye sheria mbili hizo, vipo vifungu vilivyompa uwezo mkubwa Waziri wa kulifungia au kuzuia uchapishaji wa gazeti, akihisi kwa maoni yake, kunataka kuchapishwa habari iliyokinyume na maadili,’’anasema.

 

Ndio maana TAMWA-Zanzibar imekuwa karibu mno na wadau wake kama vile Shirika la Internews, MCT na waandishi wa habari, kuhakikisha Zanzibar kuna kuwa na sheria rafiki.

 

Mwandishi Salim Said Salim, anasema huu sio wakati tena wa sheria zinazoongoza vyombo vya habari, kumpa uwezo mkubwa Mkurugenzi, au Waziri.

 


‘’Inashangaaza kuona katika sheria za habari, hadi leo kuna maneno kama waziri anaweza, mkurugenzi akihisi, Polisi anaweza kupekuwa, haya yote yanaleta ukakasi kwenye kazi za vyombo vya habari,’’anasema.

 

Mwandishi Khadija Kombo wa ZBC Pemba, anasema ukakasi wa sheria za habari hapa Zanzibar, wakati mwengine huwarejesha nyuma waandishi, kuibua changamoto za wananchi.

 

‘’Inawezekana waandishi wa habari wanataka kuibua changamoto kubwa inayowahusu wananchi, lakini vipo vifungu ambavyo vinatishia utendaji wao wa kazi,’’anasema.

 

Meneja wa redio Jamii Mkoani Said Omar Said, anasema uwepo wa vifungu kandamizi kwenye sheria za habari, wakati mwengine huwakosesha kujiamini waandishi katika kazi.

 

Mwanasheria wa Shirika la Magazeti ya serikali Zanzibar na mhariri wa habari wa shirika hilo, Juma Khamis Juma, anasema kwenye utekelezaji na tafsiri za vifungu vya sheria, hakutakiwi kuwepo neneo lenye utata.

‘’Kwa mfano neno waziri anaweza, akiona inafaa, akihisi na mengine yanayofanana na hayo, huwa ni hatari kuwepo kwenye maelezo ya utekelezaji wa sheria,’’anasema.

Khamis Iddi Mabrouk na mwenzake Issa Haji Khamis wa Kangagani, wanasema waandishi wasipokuwa huru, hata wananchi hawatokuwa huru, kufanya uamuzi sahihi.

Hidaya Mjaka Ali wa Vitongoji mwenye ulemavu wa viungo, anasema, wanavitarajia mno vyombo vya habari, kuibua changamoto za jamii.



Mwanasheria wa serikali Ali Amour Makame anasema kwamba, sio sahihi kifungu hicho kuwepo kwa sababu, kisheria halitakiwi kuwepo neno ‘kwa maoni yake’.

 VIFUNGU VYA SHERIA ZA HABARI VINAVYOUTETEMESHA UHURU WA HABARI ZANZIBAR

Sheria ya Tume ya Utangaazaji Zanzibar nambari 7 ya mwaka 1997, kwenye kifungu chake cha 13 (5) kimeutia doa huru wa habari Zanzibar.

‘’Mtu yeyote asiyeridhika na uamuzi wa Tume kutoa au kataka maombi, anaweza kukata rufaa kwa Waziri kwa namna ya njia itakavyoelezwa na kanuni,’’kinaeleza kifungu hicho.

Ambapo hapa, momba leseni, anapokataliwa na Katibu Mtendaji wa Tume, akate rufaa kwa waziri, ambae ndie aliyemteua au kusababisha kupatikana kwa Katibu huyo.

Wadau wa sheria wanasema, jambo hilo lina utata, maana Katibu Mtendaji wa Tume ya Utangaazaji na waziri anayehusika na utangaazaji, ni kiungo kimoja.

Mwandishi wa Shirika la Utangaazaji Zanzibar ‘ZBC’ Khadija Kombo anasema, kama Tume imekataa kutoa leseni, kifungu kingelekeza vyenginevyo, kwa mfano kukimbilia mahakamani.

Kifungu chengine chenye maneno yenye ukakasi kwa ukuaji wa wa uhuru wa habari ni cha 27 (1), ambapo waziri husika au mwengine aliyeidhinishwa, anaweza kutoa amri kumtaka mpewa leseni, atangaaze jambo lolote ambalo kwa maoni ya Waziri, lina maslahi kwa umma au uslama wa taifa.

Hapa wadau wa habari wanasema, kifungu hicho kipo kishari shari, maana kimebainisha uwezo wa Waziri, kumlazimisha mpewa leseni kutangaaza jambo ambalo anaona tu ni kwa maslahi ya umma au usalama wa taifa.

Mdhamini wa Baraza la Habaeri Tanzania ‘MCT’ Zanzibar Shifaa Said Hassan, anasema neno kwa maslahi ya umma, sheria hiyo haijalitafsiri, hivyo waziri anaweza kutumia mwanya huo kutangaaza jambo ovu.

Hata Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA- Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, anasema, neno usalama wa taifa, sheria hiyo kwenye vifungu vyake 30 na sehemu sita halikutajwa.



‘’Hapa mpewa leseni, amewekwa njia panda, maana Waziri akiamka vibaya anaweza kutumia mwanya huo, na kutoa taangazo ambalo halina maudhui na nchi, huku sheria ikimlinda,’’anasema.

Ndio maana Mratibu wa Shirika la Internews Zanzibar, Zaina Mzee, anasema vifungu ambavyo vinampa uwezo mkubwa waziri, au vyenye utata, kwa sasa wanasimama kutaka viondolewe.

Kama habari ni haki ya kikatiba, sheria zinazosimamia ni vyema zisiwe na maneno au amelezo yanayoashiria kumpa mtu mmoja uwezo, kama vile anajiamulia kufanya mambo yake binafsi.

Mwandishi Malik Shahran wa ZCTV anasema, suala la habari ni haki ya binadamu, si vyema kuwepo kwa sheria inayoonesha nguvu za mtu mmoja kufanya uamuzi.

‘’Maneno kama Waziri akiweza, atakavyoona inafaa au kwa maoni yake, yanapekelea wengine kukosa hamu ya kuingia kwenye sekta ya habari,’’anasema.

Mwandishi wa Mwanahalisi mtandaoni Jabir Idrissa, anasema athari kubwa ni wawekezaji sekta ya habari, kukosa hamu ya uwekezaji, na kundi kubwa kukosa ajira.

Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa Habari Zanzibar ‘ZPC’ Abdalla Mfaume, anasema moja ni kuzisemea sheria na vifungu kandamizi, ili waandishi wa habari wafanyekazi zao kama ilivyo, kwa makundi mengine.

Rahma Suleiman wa Gazeti la Nipashe, anasema waandishi na wadau wa habari, waungane kusindikiza mswada wa sheria habari Zanzibar ulipofikia, upelekwe hatua nyingine.



Mchambuzi wa sheria za habari Zanzibar Imane Duwe, anasema maneno kama ‘uwezo wa Mkurugenzi, Waziri, akiona inafaa, akihisi, kwa maoni yake’ kwenye sheria mpya ya habari yasitumike.

Maryam Salum Habib mwandishi wa habari wa Gazeti la Zanzibarleo Pemba anasema, Mamlaka hayo aliyopewa Ofisa wa Polisi anaweza kukamata gazeti, atakapojisikia tu kukamata na sio kwa kufanya kosa.

 

Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Kajubi Mukajanga anasema, waandishi wasipozielewa sheria zao, mchakato wa kupitisha utakuwa kwenye mikono ya wanasheria na wanasiasa, na hivyo watapendekeza wanavyotaka.

 

Anasema, kuna vifungu vingi ambavyo vinahitaji kufanyiwa marekebisho ikiwemo cha 27 (1), (3), kwani vinawanyima waandishi uhuru na kuwakosesha wananchi haki ya kutoa maoni na kujieleza.

 

                                                       MWISHO.

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch