Skip to main content

'SHERIA ZINAZOLINDA HAKI ZA WANAWAKE ZITEKELEZWE KWA VITENDO'

                          


NA HAJI NASSOR, PEMBA:::::

WANAWAKE wa kiislamu ambao wanachuma mali pamoja na waume zao, wametakiwa kufuatilia haki zao za kupatikana kwa mali, mara baada ya ndoa kuvunjika, kwani sheria ya Mahakama ya kadhi, nambari 9 ya mwaka 2017 imetoa haki hiyo.

Ilielezwa kwenye sheria hiyo, kifungu cha 5 (1) (f) kuwa, mwanamke aliyeachwa na ikiwa wamechuma mali pamoja na aliyekuwa mume wake, anaweza kulalamika mahakamani, kupata mchango wa kuanzia maisha.

Hayo yalibainika hivi karibuni, kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika ofisi ya PEGAO, Chake chake, wakati Mkurugenzi wa asasi hiyo Hafidh Abdi Said, alipokuwa akitoa taarifa kwa waandishi hao, juu ya utekelezaji wa haki za mwanamke.

Alisema, wapo baadhi ya wanaume wamekuwa wakichuma mali pamoja na mwanamke, ingawa baada ya ndoa kuvunjika, hajali na wala hazingatii suala la kumpa mchango wowote mwanamke, kwa ajili ya kuanzia maisha.

Alieleza kuwa, ndio maana wakati umefika sasa, kwa wanawake waliomo kwenye ndoa, na mara wanapoachwa na ikiwa kuna mali wameichuma na aliyekuwa mume wake, kuitumia mahakama ya kadhi kulalamika.



‘’Wapo wanandoa wanaishi zaidi ya miaka 10 au 25 kwenye ndoa, na wakati mwanamme anaoa hakuwa na mali, lakini baada ya muda na ustahamilivu wa mwanamke, anapoachwa hakuna hata mchango wowote anaopewa,’’alifafanua.

Alieleza kuwa, baada ya mwanamke kulalamika, mahakama huangalia uwiyano wa mali iliyochumwa katika uhai wa ndoa yao, na kisha nae kupewa chochote kwa ajili ya kuanzia maisha ya anapokwenda.

Mkurugenzi huyo alisema, uwepo wa sheria hiyo, ni kuondoa uonevu wa muda mrefu kwa wanawake, kuishi katika wimbi la umaskini, na hasa baada ya ndoa kuvunjika.

‘’Ingawa changamoto iliyopo kwenye sheria hiyo, haikuelezwa kuwa ni lazima, bali imeeleza kuwa ni mchango wa kumsaidia mwanamke, kwa ajili ya kuanzia maisha yake,’’alisema.

Kuhusu sheria ya Ajira namba11 ya mwaka 2005, Mratibu wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hiya Mussa Said, amesema imetoa ulinzi mzuri kwa mwanamke, na kinachotakiwa ni utekelezaji wake.

Alieleza kuwa kifungu cha 10 (2) cha sheria hiyo kuwa, mwajiri analazimika kuthibitisha malipo ya mishahara sawa, kati ya mwanamke na mwanamme, wenye elimu na ngazi zinazowiayana.




Aliekeza kuwa, ulinzi mwengine upo kwenye kifungu cha 11, kinakemea unyanyasaji wa kijinsia, kumtaka muajiriwa mwanamke kimapenzi, matumizi ya vitisho, lugha inayoashiria mapenzi kwa mtumishi huyo.

‘’Lakini pia ni kosa, kwa muajiri, kuacha kumuajiri mwanamke, kwa madai kuwa muda mwingi hatokuwepo kazini, kwa sababu ya kujifungua na kunyonyesha, kwani huo ni aina ya udhalilishaji,’’alisisitiza.

Katika hatua nyingine, Mratibu huyo wa TAMWA, alisema ulinzi mwengine alionao mwanamke ni kupata mapumziko ya siku 100, ikiwa amejifungua watoto mapacha, zaidi ya siku za kawaida anapojifungua mtoto mmoja.

Kwa upande wake, mwanaharakati wa haki za wanawake na watoto, Safia Saleh Sultan, alisema ulinzi mwengine wa sheria kwa wanawake, ni uwepo wa marufuku wa kuajiriwa kwenye mionzi na kemikali za sumu, zinazotishia usalama wake na mtoto.

‘’Kwenye sheria hiyo ya Ajira kifungu cha 83 (1) na kifungu cha 84 (4), kinakataza kumpa kazi mwanamke wakati wa usiku, katika shughuli za viwanda, na hasa ikiwa usalama wake uko hatarini kimazingira,’’alifafanua.

Wakili wa watoto wanaokinzana na sheria kutoka Kituo cha Huduma za sheria Zanzibar ‘ZLSC’ tawi la Pemba Siti Habib Mohamed, anasema sheria ya Elimu nambari 6 ya mwaka 1982, kifungu cha 19, kinaelezea ulazima kwa kila mtoto aliyefikia umri wa miaka 7 na hajafikia miaka 13 kuandikishwa elimu ya msingi.

‘’Kama wapo wazazi na walezi hadi leo hii, wanawazuia watoto wao wa kike, wasipate haki ya elimu, wanapingana na sheria hiyo na hawawatendei haki,’’alifafanua.



Hata hivyo wakili huyo alisema, ulinzi mwengine upo kwenye sheria ya Kuwalinda wari na mtoto wa mzazi mmoja, nambari 4 mwaka 2005 kifungu cha 5 (1), kinataka mwari, mtoto wa kike au mwanamke ambae hajaolewa anaweza kufungua kesi ya kudai ya matunzo mahakamani dhidi ya mtu aliyepma ujauzito.

Kwa upande mwengine, wakili huyo alisema pia wanawake wanalindwa kwenye sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, kifungu cha 108 na 109 inayotoa ulinzi na adhabu ya kifungo cha mtu atakaepatikana na hatia ya ubakaji.

Mratibu wa mradi wa kuiwezeshaji  jamii kudai haki zao za uongozi, siasa na demokrasia ‘SWIL’ kutoka PEGAO Dina Juma, ameziomba mamlaka husika, kusimamia utekelezaji wa sheria hizo, ili kundia la wanawake  lipate haki zao.

                               Mwisho    

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch