Skip to main content

'WAFIKISHENI HOSPITALI HARAKA MNAPOWAGUNDUA NA DALILI HIZI.........'

  



NA HAJI NASSSOR, PEMBA::::


JAMII ya Zanzibar, imeshauriwa kuwapeleka hospitali haraka, ndugu na jamaa zao, wanapowaona na dalili kadhaa ikiwa ni pamoja na kutokwa na jasho lisilo la kawaida hata kwa msimu wa baridi, kwani hiyo ni moja ya dalili za kuugua kifua kikuu.

Dalili nyingine za kifua kikuu zilizoanishwa ni kikohozi cha wiki mbili zau zaidi, kutoa makohozi yaliyochanganyika na damu, kukonda na kupungua uzito kusiko kwa kawaida pamoia na homa za mfululizo.

Hayo yameelezwa na mtaalamu kutoka kitengo shirikishi cha maradhi ya ukoma, kifua kikuu na Ukimwi Zanzibar, Said Khamis Ahmada, wakati akiwasilisha mada ya kifua kikuu, mbele ya waandishi wa habari, kwenye mkutano uliofanyika leo Septemba 18, 2022, Maabara ya afya ya jamii Wawi Chake chake Pemba.

Alisema jamii, haina njia mbadala wanapowagundua wapendwa wao na moja ya kati ya dalili hizo au na nyingine, bali wawafikishe vituo vya afya na hospitalini, ili kufanyiwa uchunguuzi wa afya zao.



Alieleza kuwa, maradhi ya ukoma yanatibika, ikiwa mtu anapojihisi kuwa na mabadiliko mwilini mwake, na kukutana na muhudumu wa afya, na kisha kuanza dozi mapema kwa wakati.

‘’Lazima jamii isithubutu kuwachelewesha ndugu na jamaa zao kuwafikisha hospitalini, na kuanza kufanyiwa uchunguuzi na kisha kuanza dozi, ikiwa hali imelazimika hivyo,’’alifafanua.

Hata hivyo alisema, ugonjwa kifua kikuu upo wa aina mbili kuu, moja ukiwa ni ule unaoshambulia nje ya mapafu, ambao kwa kawaida, haumbukizi na ule unaoshambulia ndani ya mapafu unaoambukiza.

Nae Mratibu wa Kikfua kikuu na Ukoma kanda wa Pemba dk. Hamad Omar Hamad, alisema kwa idadi ya wananchi wa Zanzibar, kuwa na watu 7,524 wanaoishi na Virusi vya Uki,mwi ni kubwa mno.



‘’Utafiti uliofanywa na shirika la misaada ya Marakani UNAIDS Globan HIV mwaka 2019, ulionesha watu milioni 38 wanaishi na VVU, na kati ya hao milioni 25.4 wanatumia dawa za kupunguza mali ya VVU na watu milioni 1.7 waliambukizwa VVU mwaka 2019,’’alifafanua.



Hata hivyo alisema utafiti huo kwa Zanzibar, uligundua kuwa, kuna asilimia 0.4 ya watu wanaoishi na VVU, tokea pale alipogundulika mgonjwa wa mwanzo, hospitali ya Mnazi mmoja Unguja mwaka 1986.

Kuhusu ugonjwa wa Uviko19, aliitaka jamii, kuendelea kuchukua tahadhari za maksudi, kwani ugonjwa unaosambaa kwa mfumo wa hewa, ni rahisi kuupata.

Valeria Rashid kutoka kitengo hicho, alieleza kuwa moja ya njia inayochelewesha kutokomeza magonjwa kama kifua kikuu, ukoma na korona ni kuwanyapaa wagonjwa walioambukizwa.

‘’Waliogundulika na magonjwa mbali mbali wamekuwa wakipewa majina kadhaa, yanayoonesha unyanyapaa na kurejesha nyuma mikakati ya kutokomeza magonjwa hayo,’alieleza.

Akifungua mkutano huo Meneja Mpango wa Shirikishi wa magonjwa ya Ukimwi, Kifua kikuu na Ukoma Pemba Khamis Hamad Khamis, alisema vyombo vya habari ni nyenzo pana ya kutoa elimu ya kupambana na magonjwa hayo.

‘’Tafiti zinaonesha kuwa, hadi mwaka 2020 duniani kulikuwa na watu milioni 10, waliopata ugonjwa wa kifua kikuu na kati yao, milioni 1.5 sawa na watu wote wa Zanzibar (sensa 2012) waliripotiwa kufariki dunia,’’alifafanua.



Baadhi ya waandishi wa habari akiwemo Mchanga Haroub Shehe wa Shiria la Utangazaji Zanzibar ZBC, na mwenzake kutoka Sauti ya Ist-qama Salim Ali Msellem, walisema mikakati endelevu inahitajika ili kutokomeza magonjwa hayo.

                                 Mwisho    

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch