Skip to main content

''MASHAHIDI NJOONI MAHAKAMANI NAULI YENU IPO'

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::::

MAHAKAMA kuu kanda ya Pemba, imesema itahakikisha sasa inawapatia stahiki zao zote mashahidi wanaofika mahakamani, ikiwa ni pamoja na nauli, ili kusiwe na mkwamo wa kesi hasa za udhalilishaji unaosababishwa na mashahidi.

Hayo yameelezwa leo Septemba 21, 2022 na Naibu Mrajisi mahakamu hiyo kisiwani Pemba Faraji Shomari Juma, wakati akizungumza na waandishi wa habari mahamani Chake chake, pembeni ya kikao kazi za kusukuma kesi, kilichofanyika mahakamani hapo.

Alisema, kwa sasa mahakama imeshajipanga vizuri, kuhakikisha mashahidi wanaofika mahakamani, wanapatiwa stahiki zao zote, ikiwemo nauli na kuona hakuna kesi inayokwama, kwa kukosa mashahidi.

Alieleza kuwa, kesi kadhaa zikiwemo za udhalilishaji wa wanawake na watoto, zimekuwa zikikwama kutokana na mashahidi kutofika mahakamani, na kusema ikiwa sababu ni kuogopa kukopwa nauli na mahakama, sasa hilo halipo tena.



‘’Ni kweli tumegundua kuwa, kesi nyingi zimekuwa zikifutwa ama kuondolewa mahakamani, kutokana na mashahidi kutofika mahakamani, licha ya kupelekewa hati za wito,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Naibu Mrajisi huyo wa mahakama kuu kanda ya Pemba, alisema wamekuwa wakipokea kesi nyingi, ingawa mwisho wake, hulazimika kuziondoa kutokana na kukosa mashahidi.

Kwa upande Wakili wa serikali Seif Mohamed Khamis, alisema wakati umefika sasa, kwa sheria kuchukua mkondo wake, ikiwa watajitokeza mashahidi, wanaokataa kutii wito wa mahakama.

Alieleza kuwa, licha ya juhudi zinazochukuliwa na vyombo vya sheria, kuwaelimisha wananchi katika kufika mahakamani kutoa ushahidi, ingawa bado juhudi hizo hazijazaa matunda.






‘’Njia ya kufanya, ili mashahidi wafike mahakamani, ni kuendelea kuwaelimisha wananchi na kesi kuendeshwa kwa kasi, ili wanaohitajika mahakamani wasiochoke,’’alieleza.

Kwa upande wake, Mkuu wa upelelezi wa Jeshi la Polisi wilaya ya Wete Fakih Yussuf Mohamed, alisema changamoto bado ni kubwa kwa mashahidi, kutofika mahakamani, licha ya kufikishiwa wito kutoka mahakamani.

‘’Jamii bado haijataka kusimamia na kutilia mkazo, suala la upatikanaji wa haki, ndio maana imekuwa vigumu kufika mahakamani kutoa ushahidi,’’alieleza.

Aidha alisema, inashangaaza kuona walalamikaji siku ya kwanza wanafika kituo cha Polisi kwa hasira, kulalamikia jambo lililotokezea, ingawa baada ya muda, hukataa kutoa ushirikiano.

Hakimu wa mahakama ya mkoa Chake chake Luciano Makoye Nyengo, alisema inasikitisha kuona jalada la kesi lililoanzia Polisi na kisha kupitia ofisi ya Mkurugenzi wa mashataka, ingawa kisha mashahidi hawaonekani mahakamani.




‘’Kesi inamiezi yake, ikifika bila ya mashahidi kufika mahakamani, mahakama hutakiwa kuiondoa, kinchojitokeza lawama hizo hutupiwa mahakimu na majaji,’’alieleza.

Mratibu wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na dawa za kulevya dawa za kulevya Pemba Omar Juma Mbarouk, alisema mfumo wa mahakama wa kuwaita mashahidi wote kwa siku kwa kesi moja, ni mzuri na unaweza kupunguza changamoto.

‘’Kesi za dawa za kulevya ni nzito kuzifuatilia na kuzigundua, sasa tunapozileta mahakamani, lazima mahakimu na majaji wawe makini katika kuziendesha,’’alieleza.

Kikao hicho ni muendelezo wa vikao kadhaa vinavyofanywa na mahakama kuu Zanzibar, katika kuharakisha uendeshaji wa kesi kwa haraka na kutolewa hukumu.

                                          Mwisho     

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch