Skip to main content

WENYE WATOTO WALEMAVU PEMBA WAPEWA MBINU KUWAKINGA NA UDHALILISHAJI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA::::


WAZAZI na walezi wanaoishi na watoto wenye ulemavu kisiwani Pemba, wametakiwa kuzidisha ulinzi zaidi kwa watoto wao, kwani wadhalilishaji wamekuwa wakiwatumia zaidi, kumalizia shida zao za kibinadamu, kutokana na mazingira yao.

Ushauri huo umetolewa na Afisa Mipango wilaya ya Chake chake Kassim Ali Omar, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi, kufuatia kuwepo kwa wimbi kubwa la watu wenye ulemavu kudhalilishwa, wilayani humo.

Alisema, pamoja na shughuli za kila siku walizonazo wazazi na walezi za kutafuta maisha, lazima wajiwekee utaratibu wa kuwawekea ulinzi maalum, watu wenye ulemavu.

Alieleza kuwa, haiwezekani wazazi au walezi, wawatelekeze watoto wao majumbani, kwa muda mrefu, bila ya kuwepo mwangalizi maalum.

‘’Shughuli za kutafuta maisha ni nzito, lakini suala la kuwapa ulinzi watu wenye ulemavu, hutakiwa lifanywe mara dufu, maana sasa wadhalilishaji wamehamia kwao, wakijua hawawezi kujitetea mahakamani,’’alieleza.



Katika hatua nyingine, Afisa Mipango huyo Kassim Ali Omar, alivishauri vyombo vya ulinzi na usalama, kuyasaidia makundi ya watu wenye ulemavu, wanapofika katika tasisi hizo kutafuta haki.

Katibu wa kamati ya kupambana na udhalilishaji wilaya ya Chake chake Rashid Said Nassor, alisema kamati hiyo imekuwa karibu mno na makundi ya watu wenye ulemavu.

‘’Hata katika kamati yetu, yumo mjumbe kutoka Idara ya watu wenye ulemavu wilaya ya Chake chake, lengo ni kuona tunasaidianaje, ili kupunguza matendo hayo kwao,’’alieleza.




Kwa upande wake, Mratibu wa watu wenye ulemavu wilaya ya Chake chake Mwadini Juma Ali, alisema lazima jamii ishirikiane na familia, katika kuimarisha ulinzi wa watu wenye ulemavu.

‘’Kama jamii itaona jukumu la kuwalinda watu wenye ulemavu ni la familia na tasisi za watu wenye ulemavu pekee, kundi hilo linaweza kukosa haki zake mbali mbali,’’alieleza.



Mwakilishi kutoka kituo cha mkono kwa mkono Chake chake Nuru Ali Nassor, alisema kesi nyingi zinazowahusu watu wenye ulemavu, hazina mwisho mzuri.

Akizungumza hivi karibuni, Mratibu wa Jumuia kwa ajili ya watu wenye ulemavu Zanzibar ‘ZAPDD’ Pemba Khalfan Amour Mohamed, alisema makundi yote yanaathirika ingawa wanachama wao ni zaidi.

‘’Zipo kesi kadhaa zimekuwa zikifutwa au kutoendelezwa mahakamani na vituo vya Polisi, ambazo zinawahusu watu wenye ulemavu wa akili, lazima jamii ishirikiane,’’alifafanua.

Afisa mawasiliano wa TAMWA-Pemba Gasper Charles, alisema kama vyombo vya habari vitaweka mkazo wa kukemea matendo hayo, kundi la watu wenye ulemavu linaweza kubakia salama.

Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, ameendelea kuitaka jamii kuhakikisha hakuna sulhu ya aina yoyote kwenye matendo ya ukatili na udhalilishaji.

Mratibu wa Kituo cha Huduma za sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba Safia Saleh Sultan, alisema kama jamii itashirikiana hasa kwenye hatua ya kutoa ushahidi, kesi hizo kwa watu wenye ulemavu zinaweza kukoma.

Mjumbe wa kamati tendaji ya Jumuiya ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar ‘JUWAUZA’ Hidaya Mjaka Ali, alisema bado vyombo vya mahakama na jeshi la Polisi, havijakuwa rafiki na kundi la watu wenye ulemavu.

Mtoto Hadia Mjaka Mosi (17) wa Mwambwe mwenye ulemavu wa viungo, alishauri kuwa, lazima kuwe na adhabu ya ziada kwa washitakiwa watakobainika kuwadhalilisha.

Jumla ya matukio sita ya watu wenye ulemavu yametokezea ikiwa ni pamoja na kubakwa na kulawitiwa, ingawa tayari yameshafikishwa mahakamani.

                        Mwisho    

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch