NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@
PANGO la kijij,
linalopatikana shehia ya Makangale, kaskazini mwa Pemba.
Ni mojawapo ya kivutio
cha kihistoria vyenye hadithi ya kipekee.
Umaarufu wa pango hili,
ulianza mwaka 2009 baada ya Profesa Felix Chami wa Chuo Kikuu cha Dar- es
Salaam, kugundua mabaki ya kihistoria, ikiwemo mifupa ya wanyama, shanga, mkaa,
na vigae vinavyoashiria uwepo wa makazi ya binadamu katika vipindi tofauti vya
kihistoria kwenye pango hilo.
Kwa mujibu wa historia, pango hili lilitumiwa na wapiganaji wa vita ya kwanza
ya dunia 1914 hadi mwaka 1918.
Na baadae vita ya pili
ya dunia yam waka 1939 hadi mwaka 1945, kama maficho yao na pia sehemu ya
kuficha silaha.
Leo hii, pango la kijiji Makangale limekuwa kivutio kikubwa cha watalii, wanaotembelea
hasa hoteli za kaskazini Pemba, hufika kushuhudia uzuri na historia ya pango
hilo, lenye milango miwili wa kuingilia na wa kutokea.
Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale Pemba imeboresha njia za kuingia pangoni
humo, ili kurahisisha wageni wanapokaribishwa.
Maana wageni hao huwa,
wanavutiwa na sauti za popo wadogo ambao ni wanyama wa kudumu wa katika pango
hilo.
Yussuf Haji Khatib ni Afisa
Muhifadhi wa Mambo ya Kale Pemba, anasema eneo la kihistoria la pango la kijiji
ni sehemu muhimu ya kihistoria, hapa kisiwani Pemba.
Umuhimu wake umekuja zaidi, baada
ya Proffesa Felix Chami kutoka chuo kikuu cha Dar-es- Saalam kufanya utafiti
mwaka 2009 wa kiaklojia.
Utafiti huo aliufanya kwa kuchimba
chini (systemically) na baada ya kufanya utafiti huo, alipata mabaki
mbali mbali.
Kama vile vigae vya zamani vya
vyungu, majagi ya kutilia maji vya udongo na kigae.
Mabaki hayo ya udongo na kigae,
yaliyokutikana chini yalitengenezwa nje na ndani ya nchi na paliashiria
kuwa eneo hilo palikuwa na makaazi ya watu na shughuli zao.
Kwa mujibu wa vigae watu hao,
walifanya biashara na watu wa nje na walikuwa wana mawasiliano baina yao
kutokana na vigae hivyo, vilionesha kuwa vinatoka mataifa kama China, Iran, India.
Vigae hivyo vilitoa tafsiri pana,
kutokana uhalisia wake, katika eneo hilo, palipatikana na mbegu za mimea ya
mitama.
Katika utafiti huo, hata kama
palikuwa na maakazi ya watu kutokana na mbegu hizo shughuli za kilimo kwa jamii
ya watu wa hapo, zilikuwepo tangu enzi za chuma.
Enzi za chuma hapo Afrika, kuanzia
miaka 200 kabla ukiristo mpaka miaka 1000 common error.
Mwaka 2012, alifanya utafiti tasisi
ya max plan na ikarejea tena mwaka 2016, na akapata mabaki kama aliyoyapata Chami
na mingine kama vile mifupa ya panya wakubwa.
Inafahamika kiwa, hao ndio waliopata
mabaki mingi zaidi na waliamini kuwa, kisiwa cha Pemba huenda ndIo kisiwa cha
minosia kilichotajwa katik kitabu cha zamani cha wagiriki yaani
(periplus).
Minosia ni kisiwa kinachoishi
mamba, ambao hawazuru kaskazini mwa pango la kijiji, kulikuwa na mji wa
kale unaoitwa Msuka mjini.
Pamoja na hilo, waliamini kuwa kuna
mawasiliano ya watu, katika kuhifadhi na kulitumia shughuli mbali mbali.
Na ilisemekana kuwa, katika vita
vya kwanza na vya pili vya dunia, watu walilitumia lile pango kwa
kujifichia.
Sababu ya kujifichia,
kuliokotwa mzinga wa wajerumani uliotumiwa na vikosi vya kiengereza, kati ya
kisiwa cha Njau na huba wa Mkiya wa ng’ombe.
Anasema kinadharia pango hilo, ni makaazi
ya wanyama na wadudu wa asili kama kaa, ambao ni kivutio kwa wageni na popo
wadogo wadogo wingi, wanaoishi pango hilo.
Popo hao huwa hawajifichi hata
wanapoona watu na pango hilo, likabakia kuwa ni la saili na lenye mandhari
mazuri kwa watalii.
Kwa sasa mabaki
yaliyofanyiwa utafiti yamehifadhiwa na hifadhi na Idara ya Mambo ya Kale Pemba,
kwa ajili ya kumbukumbu na kivutio kwa wengine.
Kumbe ukiingia katika Pango hilo, utapokelewa
na sauti nzuri za popo wadogo, ambao ni miongoni mwa wanyama wanaoishi katika
pango hilo.
Afisa anasema, hata magego ya meno ya
mwanadamu yalipatikana na hata hivyo yalipimwa na kufanyiwa uchunguzi magego
hayo.
Inafahamika kuwa, yaligundulikana kuwa makaazi
ya watu yalianza miaka ya 5,000 iliyopita.
Kwa sasa pango hilo hufanyiwa marekebisho, ila
likabakia na uhalisia wake ulele na marekebisho hayo ni pamoja na ngazi
za kupandia.
Na pembezoni mwa pango hilo, pamewekwa
huduma za kibinaadamu, hasa kwa waleo wanaotembelea, wakiwemo wanafunzi
Saleh Omar Juma ni mkuu wa
divisheni na Uthibiti wa Mambo ya Kale, anasema katika
upokeaji wa wageni upo kiasi kwa mwaka na itaegemea na msimu wa kipindi
unavyokwenda.
Kwa sasa eneo hilo limo, katika orodha ya maeneo
ya sehemu za kihistoria yanayohifadhiwa na kutunzwa.
Hata kama ni kivutio, kumbe
kumetofautiana baina ya mtalii kiingilio ni dola tano, mtu mzima mzawa shilingi
2000.
Na makundi ya wanafunzi wa
sekondari hulipia shilingi 1,000 na skuli za msingi ni shilingi 500 pamoja na
maandalizi huingia kwa makundi kwa bei ya mapatano.
MWISHO.
Comments
Post a Comment