NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@
MAKABURI ya Mazrui, ni sehemu ya
kihistoria inayopatikana Chwaka, shehia
ya Tumbe mashariki wilaya ya Micheweni Kaskazini Pemba.
Ni sehemu
moja wapo ya kivutio cha kihistoria, hutembelewa na wageni wa ndani na nje ya nchi,
ili kulinda urithi na utamaduni unaopatikana humo.
Makaburi ya
mazrui ni eneo la tatu la sehemu ya kihistoria, katika eneo hilo na lenye
mabaki ya utawala wa Mazrui waliohamia
katika karne ya 18.
Ni miongoni
mwa mabaki yaliyopo hapo ni hayo makaburi yaliyokuwepo sehemu hiyo.
Tukisema
makaburi ni sehemu maalum ,iliyotengwa kwa ajili ya kuzikwa kiumbe kilichokufa
na kuhifadhiwa, kwa safari yake ya milele.
MAZRUI KUHAMA KWAO KUINGIA PEMBA
Mohamed
Yussuf Khamis, ni Afisa Mambo ya Kale anasema
Wamazrui kwa jina jengine wanaitwa (Waarabu), wa kabila la kimazrui,
wanatokana na asili ya taifa la Oman.
Anasema, walihama
kwao na kuja katika upwa wa Afrika Mashariki kwa lengo la kufanya biashara na
kutawala.
Kabla ya
kuhama Oman, kulikuwa na sababu ya kuingia vitani na kabila la Albusait.
Albusait ni kabila
ambalo, lililikuja kutawala Zanzibar nzima, ukoo huo ulijulikana kwa jina la
Said Saiyd bin Sultan kwa wakati huo.
Makabila ya
mazrui na Albusait, walipigana vita huko nchini kwao Oman, kabla ya kuhamia
katika ukanda huu wa pwani.
Kutokana na
Said bin Sultani, alitawala hapa Zanzibar na wamazrui, waliamua kupigana vita
na Said bin Sultani huko Oman.
Inasemekana
vita hivyo, vilipiganishwa na Muengereza kwa sababu ya matakwa yake ya kiutawala,
rasilimali na biashara.
Vita hivyo
viliendelea mpaka pale Albusaiti, akashinda na kupata madaraka nchini Omani.
Baada ya
kushindwa kwa vita hivyo, lilitoka tamko kuwa Mazrui aondoke aende Afrika Mashafriki.
Hapa sasa Mazrui,
walitawala ukanda wa Afrika Mashariki katika miji mikubwa katika karne ya 18 na
kuenea maeneo ya Zanzibar, Kilwa, Mombasa na Pemba.
Kutokana na Mazrui
kuenea ukanda huo, ndipo walipoingia katika kijiji cha Chwaka Tumbe na kuanza
maisha yao mapya.
KWA NINI PAKAITWA MAKABURI YA MAZRUI
Kuhusiana na
makaburi ya Mazrui, kielelezo cha kuwa baada ya kufa katika eneo, walilohamia
hapo Chwaka Tumbe, walichagua eneo maalum kwa ajili ya kuzikana baada ya kufa.
Hata kama ilikuwa ni eneo lilotengwa na
makaburi yao yalikuwa, maalum yaani siyo ya kawaida kutokana famila ya kiutawala katika sehemu hiyo.
‘’Makaburi
hayo unaweza kutofautisha kutokana na hadhi ya makaburi yalivyojengwa, ikiwa la
kiutawala, mtoto au mwanamke na mwanamme,’ anasimulia.
Ingwa kwa
sasa makaburi hayo, hayakujulikana ni mangapi ila walizikwa kwa heshima na
makaburi yalijengwa ili kutofautisha kaburi, moja na jingine.
Makaburi yalitofautishwa
kutokana na hadhi ya mtu aliyekufa, ikawa kila mtu anazikwa kwa kujengewa
kaburi kutokana na hadhi, na utawala wake.
‘’Mijengo
hiyo ilikuwa ikizingatia sana kiutwala na ukubwa na hadhi ya makaburi,’’ anafafanua.
Hapo palikuwa
na kielelezo ya kuwa palikuwa na watu walikufa na kuzikwa sehemu hiyo.
Saleh Omar
Juma, ni mkuu wa divisheni na Uthibiti wa Mambo ya kale, anasema katika kisiwa
cha Pemba, kuna urithi wa kimaumbile na urithi wa ndani.
Unaweza
kusema urithi, unaoshikika na urithi usioshikika, kwa urithi unaoshikika yaani
ni huu wa kimaumbile amabo unaonekana katika maeneo ya kihistoria.
Anasema katika
upokeaji wa wageni, upo kiasi kwa mwaka na itaegemea na msimu wa kipindi
unavyokwenda.
Aina ya watu
wanaotembelea katika eneo hilo ni watafiti, watalii na wanafunzi, ila kiingilio
kinatofautiana baina ya mgeni na mzawa.
‘’Katika
jamii zetu za kawaida, tunazoishi muamko bado mdogo wa utembeleaji wa eneo hilo
zaid kwa watu maalum,’’anafafanua.
Anasema
katika makundi, wanaotembelea eneo hilo wapo na wageni kutoka nje ya nchi na
kila mwaka, hutokezea watafiti kuingia sehemu hizo, kwa ajili ya utafiti
hulipia ada ya eneo hilo.
Kutona na
jamii iliyopo, kwa sasa imekuwa ni sehemu ya kihistoria lilojengewa na ndani yake
yamo makaburi.
Kwa sasa
eneo hilo, limo katika orodha ya maeneo
ya sehemu za kihistoria yanayohifadhiwa na kutunzwa na serikali.
Kwa mtalii
kiingilio ni dola tano, mtu mzima mzawa shilingi 2,000 na makundi ya wanafunzi
wa sekondari, hulipia shilingi 1,000 na skuli za msingi shilingi 500 pamoja na
maandalizi huingia kwa makundi kwa bei ya masikizano.
Kumbe makaburi hayo yalikuja karne ya 18,
baada ya utawala wa Haroun eneo la makaburi ya Mazrui ni kijiji ambacho
kilikaliwa na wakaazi hao.
Kutokana na
umuhimu wa eneo hilo, serikali imekuwa ikiyaenzi na kuyathamini maeneo hayo, hata
hotuba ya bajeti ya Utalii na Mambo ya Kale katika baraza la wawakilishi ya
mwaka 2025/2026, imelithibitisha hilo.
Inasema lengo
la kuyaendeleza ni kukuza pato la taifa kupitia sekta ya utalii, kuwashawishi
wawekezaji wa ndani na nje, kuanzisha miradi ya utalii na urithi wa kihistoria,
itakayotoa tija kwa wananchi.
Kusimamia na kuendeleza makumbusho ya
kihistoria na mambo ya kale kuyalinda, kuyahifadhi na kuyatangaza maeneo ya
urithi wa kihistoria yaliyopo nchini.
Wizara inayoshughulikia
maeneo ya kihistoria, imekuwa ikishirikiana na taasisi za elimu ya juu, za
kitaifa na kimataifa katika jitihada za kufanya tafiti kubwa za akiolojia, kwa
lengo la kufahamu kwa kina historia ya sehemu husika.
Maeneo
ambayo yamefanyiwa utafiti ni pamoja na eneo la kihistoria la Chwaka Tumbe,
lilikoko kaskazini wa kisiwa cha Pemba.
Wizara imekuwa ikiendelea kutekeleza programu
ya kuyaimarisha na kuyaendeleza maeneo ya kihistoria, yaliyopo nchini kwa
ujumla.
Katika
kipindi hiki cha miaka mitano ya serikali ya awamu ya nane, imefanikiwa kufanya
matengenezo makubwa kwa eneo la kihistoria la Chwaka Tumbe.
Kuendelea
kuyafanyia matengenezo eneo hilo ni hatua moja wapo ya kutunza na kuhifadhi
historia iliyopo nchini, kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.
MWISHO.


Comments
Post a Comment