Skip to main content

WAZIRI PEMBE: SHERIA MPYA YA HABARI ZANZIBAR KUTINGA BARAZANI MWAKA HUU

 

 



NA HAJI NASSOR@@@@

WIZARA ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar, imesema katika Baraza la Wawakilishi linalotarajiwa kuanza wakati wowote, sheria mpya ya habari, itasomwa kwa mara ya kwanza.

 

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa wizara hiyo Riziki Pembe Juma, jana Mei 2, 2026 hoteli ya Madinatul-Bahar iliyopo nje kidogo ya mji wa Unguja, kwenye hafla ya utoaji tuzo, kwa waandishi wa habari za takwimu, kuhusu wanawake na uongozi.

 

Alisema, tayari kila kitu kimeshakaa sawa na kinachosubiriwa, ni kufika kwa siku ya kuanza kwa kikao cha Baraza hilo, na mswada huo kusomwa.

 

Alisema, wizara imeshakamilisha taratibu zote, na sasa wadau wa sheria hiyo wakiwemo waandishi wa habari, wafuatilie Baraza la Wawakilishi lijalo.

 

‘’Najua mliowengi mnahamu ya kutaka kusikia, kuhusu nini wizara imefikia, juu ya sheria mpya ya habari, lakini niwaarifu kuwa, itapelekwa Barazani mwaka huu wa 2026/2027,’’alifafanua.

 

Katika eneo jingine Waziri Pembe, alikipongeza Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania ‘TAMWA’-Zanzibar, kwa kuendelea kuikumbushia sheria hiyo.

 

Kuhusu washindi wa tuzo hizo, aliwataka kuongeza bidii ya kuandika habari za wanawake na uongozi, kwa kutumia takwimu.

 

Mapema Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA-Zanzibar Nairat Ali Abdull, aliikumbusha wizara ya habari, kuhusu upatikanaji wa sheria, mpya ya habari Zanzibar.

 

Alisema, moja ya changamoto ambayo waandishi wa habari wanakumbana nayo, ni kuwepo kwa sheria kongwe, ambazo sio rafiki kwa uandishi wa habari wa sasa.

 

Kuhusu tuzo za takwimu kwa wanawake na uongozi, alisema TAMWA imefanikiwa kuendesha tuzo hizo kwa msimu wa awamu tano mfululizo.

 

Hata hivyo, aliwapongeza timu ya majaji waliopitia kazi hizo, na kuahidi mapendekezo walioyatoa kuyafayiakazi, ikiwemo kuzidi kuwaelimisha waandishi wa habari.

 

Mwandishi wa jumla ni Yussra Mohamed wa ZBC radio, mshindi wa tunzo ya elimu ni Zuhura Juma Said wa Gazeti la Zanzibar leo Pemba.

 

Mshindi kwa upande wa mitandao wa kijamii ni Fatma Hamad Faki wa Pemba ya leo blog, Khadija Rashid Nassor aliibuka na ushindi kwa Redio jamii, akitokea Mkoani Pemba.

 

Wingine ni Yussra Mohamed ni mshindi wa kwanza kwa redio kubwa, wilaya ya Kaskazini ‘B’ kwa Unguja na Wete kwa Pemba, waahamasishaji jamii wao, waliibuka na ushindi wa kwanza.

 

Wadau wa habari Zanzibar, wameshatoa mapendekezo yao, kwamba sheria ya magazeti namba 5 ya mwaka 1988, na ile ya Tume ya ya Utangaazaji namba 7 ya mwaka 1997, waliomba zifutwe, ili ziendane na wakati.

 

                         Mwisho

  

     

 

Comments