NA HAJI
NASSOR, PEMBA@@@@
TAIFA
la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sasa limo kwenye shamra shamra ya kusherehekea
siku yake za kuzaliwa ‘birthday ’.
Taifa hili ambalo liliasisiwa mapema Aprili 26, mwaka 1964,
kwa wasisi, kuchanganya udogo kama ishara ya kuunganisha nchi mbili na kuwa na
taifa moja.
Maana kabla ya Muungano huo, tusema chini ya mwaka 1963,
Zanzibar ikijulikana kama Jamhuri ya watu wa Zanzibar, ambapo baada ya Muungano
huo, taifa jipya sasa limezaliwa, nalo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Yapo malengo mablimbali yaliosababisha hata waasisi wetu,
Julias Kambarage Nyerere kwa Tanzania bara na Sheikh Abeid Amani Karume kwa
Zanzibar, yaliowasukuma kuungana.
Moja wapo ni kuimarisha uhusiano wa umoja wa kitaifa,
sambamba na kutanua fursa za uongozi, kwa nchi mbili hizi, ikiwa ni pamoja na
kitaaluma, uongozi na biashara.
Na ndio maana katika safu ya uongozi, Serikali ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikitanua wigo wa uongozi kwa wazanzibari, ambao
nao ni wahusika wa Muungano huo.
Kundi la wanawake ambalo kwa muda mrefu lilikuwa limesahualiwa
hasa kwenye safu ya uongozi, kwa kuwepo dhana kadhaa, ikiwa ni pamoja na kwamba
hawawezi kuongoza.
Kwani si unakumbuka, ilipita karne kwa karne kundi hili,
tokea tumetawaliwa na wageni na hata baada ya kujitawala wenyewe bado, hawakuwa
wakipewa kipuambele.
Uwepo kwa Muungano wa Jamhuri ya watu wa Tanzania, na sasa ukitimiza
miaka 62, wanawake wa Zanzibar kama vile wameongeza wigo wa uongozi kwao.
Maana, fursa iliyopo kwa wanawake hawa wa Zanzibar, kwamba
wanaweza kuwa viongozi ndani ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, lakini hata
serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Na ndio maana, mzanzibari wa kwanaza mwanamke kushika
nafasi nyeti ya uwaziri wa fedha alikuwa na Zakia Hamdani Meghji, ambae anasili
ya visiwani.
Yeye Meghji kupitia uwepo wa Muungano wa Tanganyika na
Zanzibar, aliukwaa uwaziri huo kwenye awamu ya nne ya rais Dk. Jakaya Kikwete
na kuhudumu kuanzia mwaka 2005 hadi mwaka 2007.
Hapa ndio alipofungua dimba kwa wanawake wa Zanzibar
kuingia ndani ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa nafasi
mbalimbali.
Kumbe faida moja kubwa ya Muungano huu unaotimiza miaka 62
sasa, kwa wanawake wa Zanzibar ni kupata uweledi na nafasi ya kushiriki uongozi,
kwa serikali zote.
Wakati alipoteuliwa na Dk. Kikwete Novemba 2005 waziri huyo
wa kwanza wa Fedha mwanamke tena kutoka Zanzibar, na wapili baada ya uhuru,
Meghji alisema anachangamoto kubwa.
“Tanzania inakusanya mapato kidogo, lakini inahitaji
matumizi makubwa, sasa lazima nijipange sana ili kuhakikisha, watanzania wanapata
maendeleo makubwa,’’ aliwahi kusema wakati huo.
Waziri Meghji ingawa hakutokea Zanzibar moja kwa moja kupitia
nafasi hiyo, lakini ni mwenye asili ya Zanzibar, tena kupitia Muungano huu wa
Tanganyika na Zanzibar.
Ingawa mwafrika wa kwanza kushika nafasi hiyo ya uwaziri wa
fedha, alikuwa ndani ya utawala wa kigeni na nje ni Paul Bomani, aliteuliwa na
wageni kuanzia mwaka 1962 hadi mwaka 1965 mwaka mmoja baada ya huru, ambae sasa
ni marehemu.
Muungano huu wa Tanganyika na Zanzibar ambo ni miongoni mwa
tunu za taifa, ulimpa fursa ya utumishi mwanamke mwengine wa Zanzibar Saada
Mkuya Salum nafasi ya unaibu waziri wa fedha.
Yeye alianzia kushika nafasi hiyo tokea Machi 7, 2012 hadi
Januari 20, mwaka 2014, ambapo awali rais wa wakati huo, alimteua kuwa mjumbe
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Fursa na haki ya kuingia bungeni kwa wanawake wa Zanzibar,
ni ishara na nafasi ya wao, kujitoa kuikumbia kuelekea kwenye 50 kwa 50 ndani
ya vyombo vya maamuzi.
Maana Mkuya, ijapokuwa kwa kipindi kifupi alihudumu kwenye
nafasi ya uwaziri wa Fedha, jambo ambalo baadae lilimpa hamasa na ujemadari,
kisha kuingia ndani ya Jimbo la Welezo na kuukwaa ubunge kamili.
Ingawa Muungano huu uliwaamsha pia akina Mauwa Abied
Daftari hadi kuhuduma kwenye wizara inayosimamia Mawasiliano, lakini baada ya
kustaafu kwake na kujijenga vyema hata Rais wa Zanzibar ameshamteua kuwa
mshauri wake mkuu wa masuala ya Pemba.
Gwiji na mahiri wa
kuongoza hadi kimataifa, Amina Salum Ali nae alishabisha hodi kwenye Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, kwa nafasi pia uwaziri wa fedha.
Amina ambae alishahudumu kimataifa kwa miaka zaidi ya saba,
sasa amerejea tena Zanzibar, na aliwahi kuingia kwenye safu ya wanaoutamani
urais wa visiwani.
Lakini mwanamke wa kwanza wa Zanzibar alieingia ndani
serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na leo kuifungulisha dunia ukurasa
mpya ni Dk. Samia Suluhu Hassan, alienzia uwaziri Zanzibar na sasa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi
wa Ikulu mwaka huo 2010 mara baada ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo na Dk:
Kikwete, alisema anachotaka kuona, ni kutatua kero za Muungano.
Kuhudumu kwake ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
mwanamke huyu mzanzibari, alinogewa na kuaminiwa na watanzania kadhaa
walioshiriki Bunge maalum la Katiba.
Maana, Samia mwezi Machi, 2014 aliwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti
wa Bunge hilo, na kuwastaajabisha walimwengu pale alipomiminiwa kura 390 sawa
na asilimia 74.6 na kumuangasha mpinzani wake Amina Abdalla Amour, aliepata
kura 126.
Umahiri na uzoefu wake wa uongozi, aliouanza kwenye serikali
ya Zanzibar, kwa kuwa waziri kwenye wizara mbili na vipindi viwili tofauti,
kisha kuhuduma ndani ya Muungano, Samia hakuishia hapo.
Maana Julai, 2015 rais wa wakati huo, wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, alimteua kuwa mgombea mwenza, ambapo kwa sasa, ndie
mwanamke wa kwanza kwa Tanzania, kabla na baada ya uhuru kushika nafasi ya
Makamu wa Rais.
Hapa ndio wanawake wa Zanzibar hasa kwenye safu ya uongozi
wanapoona kuwa, Muungano huu umewatoa kiukumbi, maana wameshatanua mbawa na
kuwajengea umaarufu.
“Kazi yangu ni kuona wanawake wanasonga mbele kimaendeleao
na watanzania wote, bila ya kijali dini, rangi wala chama mtu anachoshabikia,’’
alisema.
Kumbe wanawake wa Zanzibar kuwepo kwa Muungano huu, kama
ndio waliofanikisha aidha kutatuliwa kwa kero za Muungano au wao kuwapa nafasi
kuionyesha jamii na duania kuwa wanaweza.
Wengi husema kama ukiwa kiongozi kwenye visiwa, dunia na
walimwengu huchelewa kukuona, lakini baada ya kujitupa ndani Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, leo mwanamke wa kwanza
kushika nafasi ya Makamu wa rais tena ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa hili heko Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, heko
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na heko waasisi wa Muungano huu na
viongozi na wananchi tunaoendelea kuutunza na kuenzi.
Ilishasemwa zamani na viogozi wa taifa hili kuwa, lazima
Muungano huu uendane na matakwa na haja ya wazalendo waliyopo, na ndio maana
baada ya miaka kupita, kuliibuka kero na kutafutiwa.
Leo tukiwa kwenye moyo na macho ya furaha, kila mmoja ni
shahidi jinsi Muungano huu, ulivyowatoa kiukumbi wanawake wa Zanzibar, kwenye eneo
la uongozi.
Wanasema bado tupooo….bado tunaendeleaaa….kuuenzi na
kuudumisha Muungano huu ambao, waasisi wake wameshatangulia mbele ya haki,
lakini fikra, mawazo na busara zao bado zipo na zinatumika.
Nakumbuka sana wakati Waziri aliyewahi kuhudumu uongozi kwa
nafasi ya uwaziri wa fedha ndani ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ile ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Amina Salum Ali, akiwania kiti cha urais, aliahidi
kuulinda Muungano huo.
Mkuu wa mkoa wa kusini Rashid Hadid Rashid, ameeleza kuwa Muungano huu wa Tanganyika na
Zanzibar, sio tu kwamba umewaunganisha wananchi, bali umetoa fursa za uongozi
kwa wanawake.
“Wapo wanawake leo hii, wamefukwa viongozi wetu wakuu,
akiwemo Dk. Samia Saluhu Hassan, ambae alilelewa na Muungano na sasa anaiongozi
serikali kuu,’’aliwahi kusema.
Khamis Haji Mbaraka Chakechake anaona, Muungano kama
umeletwa kwa ajili ya kuwapa nafasi wanawake wa Zanzibar, kuonyesha umahiri na
uwajibikaji kwenye uongozi.
Lakini Rais wa awamu ya saba wa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein, yeye daima amekuwa mkali kwa wale wanaoubeza,
kuudharua na kupuuza Muungano huu.
Hakuwa tofauti sana na rais wa awamu ya nane, ya Zanzibar
Dk. Hussein Ali Mwinyi, akisema wazi wazi kuwa, hatomvumilia yeyote,
atakaeonyesha dalili za kutaka kuuvunja Muungano huu.
Mwisho .




Comments
Post a Comment