Skip to main content

JAMII YATAKIWA KUZIDISHA KASI MAPAMBANO YA UDHALILISHAJI, UKATILI


NA MWANDISHI MAALUM, PEMBA

JAMII imetakiwa kuendelea kushirikishiana katika kupinga ukatili wa kijinsia wanao fanyiwa wanawake na watoto nchini, ili kuondosha vitendo hivyo.


Wito huo umetolewa na mweyekiti wa Madiwani Baraza mji Mkoani Mohamed Said Ali akifunguwa kongamano la kujadili ukatili kijinsia kwa wanafunzi na wanajamii wa mkoani liloandaliwa na mtandao wa utetezi wa haki za wanawake Tanzania kisiwani Pemba ikiwa ni shamra shamra ya kuadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia duniani.

Amesema serekali inaendelea kuchukuwa jitihada mbali mbali za upinga vitendo hivyo ikiwemo kuwachukulia hatuwa za kisheria watendaji wa makosa hao.

Aidha amesema licha jitihada hizo lakin bado kuna baadhi ya Jamii wanakwamisha jitihada hizo kwa kutotowa tarifa za ukatili kwa vyombo vya sheria kuchukuliwa hatuwa na badala yake kuzimaliza wenywe majumbani au kutotowa ushahidi wa katika vyombo vya sheria.



"Serekali inajitahidi kupambana kuona vitendo hivi vinaondoka lakin Hadi sasa Kuna baadhi ya familia vikitokea munamalizana wenywe majumbani Tena muna kaa maeneo ya Mbali na tokea munajadili mwatowa mamuzi "alisema 

Mratibu wa mtandao wa utetezi wa haki za wanawake Tanzania Riziki moh'd amesema katika kuadhimisha siku kumi na sita za ukatili wa kijinsia wameamuwa kuanda kongamano hilo Wilaya ya mkoani ili kuwajengea uwelewa wanajamii juu kupinga vitendo hivyo ndani ya Jamii zao.

Akiwasilisha mada ya ukatili wa kijinsia Saada Abdallah Suleiman kutoka mtadao wa utetezi wa haki za wanawake Pemba  amesema ukaji wa muda mrefu wa ufuatiliaji wa mashahid kwa baadhi ya vyombo vya Sheria hupelekea baadhi ya mashahid kukata tamaa kutowa ushahid mahakaman na kupeleka kesi hiyo kutopata hukum.

Aidha ameitaka Jamii kuwa na malizi ya pamoja katika kuwalea watoto wao ili kuwa watoto wema wenye madili.

Pia ametowa wito kwa vijana kutumia mitandao ya simu katika natumizi mazuri na kujiepush na utandawazi wa mitandao ya kijamii.

 

Ameongezea kuwa endapo vitatokea vitendo hivyo ndani ya Jamii ni vyema kutowa ripoti kwa sheha,Polis ustawi wa Jamii pamoja na jumuiya na tasisi zinazotetea vitendo hivyo ikiwemo Tamwa Zafela mtandao wa utetezi wa haki za wanawake Tanzania.

Nao baadhi ya washiriki wa kongamano hilo wamesema bado kuna hitajika nguvu za pamoja katika kupinga vitendo hivyo sambamba na kufika katika Jamii Zaid kutowa Elimu hiyo.

Hussan khamis mkazi wa Jondeni Mkoani amesema kwa sasa tayari jamii imeshapata uwelewa katika kutowa tarifa ukatili katika vyombo vya sheria lakini bado kuna hitajika kutolewa elimu zadi.

Amesema Hali ya vitendo hivyo kwa muonekano wa kawaida tayri vimepunguwa vitendo hivyo nivyema kama wanajamii kuendelea kushirikiana na vyombo vya Sheria ili wakosaji wachukuliwe hatuwa pale vitakapo tokea.



Nae Khamis Ali Hassan makazi wa mapinduz ameshukuru kwa Elimu hiyo waliyoipata ya ukatili wa kijinsia na kuomba vyombo vya Sheria kuangalia pande zote mbili za utowaji wa adhabu kwa kesi za udhaliilishaji wa kijinsia (uja uzito).

Jumla ya wanajamii wanafunzi mia mmoja na hamsini (150) wameshiriki katika kongamano hilo liloandaliwa na mtandao wa utetezi wa haki za wanawake Tanzania kisiwani Pemba .
                                                  MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...