Skip to main content

SMZ KUJENGA MJI WA KISASA WA SERIKALI

 

 


                                      

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar Dkt Mngereza Mzee Miraji amesema wizara yake imeshakamilisha ramani ya  mji wa Serikali kiutendaji kwa awamu ya kwanza ambapo maeneo sita yameshaainishwa kwaajili ya kujenga mji huo.

Akizungumza  mara baada ya kumaliza kikao baina ya wizara yake na Taasisi ya Rais ufuatiliaji na Usimamizi wa utendaji Serikalini (PDB), kilichofanyika mwisho wa wiki katika hoteli ya Golden Tulip Kiembesamaki, Unguja, alisema ramani ya Mji wa Serikali imekamilika  na muda sio mrefu Serikali itaamua wapi ujengwe mji huo.

Dkt Mngereza aliyataja baadhi ya maeneo ambayo wizara yake imependekeza kujenga mji wa Serikali ikiwemo, Fumba, Kisakasaka, Dunga na Tunguu ambapo maeneo hayo kwa unguja yameonekana yanafaa kujengwa Mji wa Serikali kutokana vigezo vinavyohitajika katika Mji wa Serikali.

“Ni kweli mwezi mmoja  uliyopita tuliwaita watendaji wa wizara zote za Serikali tuliwaita wizarani watupe maoni yao ya mwisho ili tukafanye marekebisho katika dizaini (design) ya Mji wa Serikali iliyokuwepo, lakini leo maeneo yaliyoanishwa nitayataja matatu, Fumba, Kisakasaka, na Dunga. Naongeza na moja Tunguu“ Alisema Dkt Mngereza.

 Alisema chanzo cha fedha za ujenzi wa Mji wa Serikali bado hakijafahamika lakini Serikali ikishaamua kujenga sehemu Fulani bila shaka kutakuwa na chanzo cha fedha na bajeti yake ambapo Ofisi ya Rais Fedha na Mipango itaeleza chanzo hicho na bajeti yake.

Pia alisema kupitia kikao hicho kunamajukumu wamekubaliana baina Wizara ya Ardhi na Taasisi ya PDB na majukumu hayo yametakiwa kukamilika kwa kipindi cha muda wa wiki moja.

Aidha Dkt Mngereza waliishukuru Taasisi ya Rais Ufuatiliaji wa Usimamizi Utendaji Serikalini (PDB) kwa kuanda kikao cha pamoja na Wizara yake kwa lengo la kuleta ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Ardhi Zanzibar.

Naye Mkurungenzi Mkuu Shirika la Nyumba (ZHC) Mwanaisha Ali Said alisema kikao hicho ni muhimu sana kwasababu ZHC bado inachangamoto ya kiutendaji ikiwemo fedha, jinsi ya kupata fedha na jinsi ya kuandika maandiko ya kupata fedha na vipaumbele mbali mbali.

“PDB imekua taasisi muhimu kwa ZHC kwa kutumia utaalamu wao katika sekta ya nyumba na  sekta ya uendeshaji miradi wametusaidia kutuongoza kwani vipaumbele vya Mhe Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali Mwinyi ni vingi hata vipaumbele vya Shirika la Nyumba Zanzibar pia ni vingi” Alisema Mwanaisha.

Kwa upande wake Mkuu wa kitengo cha Mawasilino na Habari Kutoka Taasisi ya Rais Ufuatiliaji na Usimamizi wa Utendaji Serikalini (PDB) Dr. Mohamed Mansour Nassor alisema Taasisi yake imeweza kujua Shirika la Nyumba Zanzibar namna gani linavyofanya kazi, mikakati yake , mafanikio pamoja na changamoto.

Alisema kikao hicho ni muendelezo wa  vikao vya PDB na Wizara mbali mbali za Serikali katika kufuatilia utekelezaji wa miradi ili waweze kujua ni changamoto zipi zinazoikabli miradi hiyo na kuipatia ufumbuzi ili kufikia malengo ambayo Mhe. Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali Mwinyi anataka katika uongozi wake.

MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch