Skip to main content

MRATIBU BARAZA LA WATU WENYE ULEMAVU PEMBA: AWAPA NENO WANAKIKUNDI PANDANI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

WANAKIKUNDI cha watu wenye ulemavu, kiitwacho ‘USHAURI’ kilichopo shehia ya Pandani wilaya ya Wete Pemba, wanaojishughulisha na kilimo cha njugu, wameshauriwa kujitenga mbali na migogoro, kwani ndio sumu inayoweza kuwagawa na kurudi tena, kwenye umaskini.

Ushauri huo umetolewa leo Januari 26, 2023 na Mratibu wa Baraza la Taifa la watu wenye ulemavu Zanzibar ofisi ya Pemba, Mashavu Juma Mabrouk, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kumaliza ziara maalum, ya kukitembelea kikundi hicho.

Alisema, vikundi vingi huanzishwa kwa furaha na malengo, mikakati mikubwa, lakini mwisho wa siku wanachama hufarakana kwa kuingia kwenye migogoro.

Alieleza kuwa, suala la migogoro ni jambo lisiloepukika, lakini suala la kuitatua ni jambo la lazima, ili kutimiza ndoto na azma ya kuanzisha umoja wao.

‘’Niwatake wenzetu hawa wenye ulemavu kuwa, kikundi chao hichi kisijekikaparaganyika, kwa kule kuikaribisha migogoro, kwani, mnaweza kurudi tena kwenye umaskini,’’alieleza.




Aidha Mratibu huyo alisema, ziara hiyo aliyoifanya ni kuangalia mafanikio, changamoto na mwelekeo wa kikundi hicho, ili kuona wapi wanahitaji kusaidiwa.

Katika hatua nyingine, alisema tayari wamewakabidhi mbegu za njugu mawe kilo tano na mbegu za matikti, kwa ajili ya kuendeleza mbele eneo lao lililobakia hapo awali.

‘’Kwa sasa kilichomo chao cha njugu mawe na nyasa zimeshakuwa vizuri, lakini wamekuwa na hamu ya kuendeleza mbele kilimo hicho na ndio maana, tumeshawakabidhi mbegu,’’alisema.

Hata hivyo Mratibu huyo, aliwakumbusha kuwa, mvuno wa mwanzo watakapovuna, wajihadhari na kuwagawana faida, hadi kupelekea kurudi tena kwenye kuomba mbegu.

Mapema Mwenyekiti wa kikundi hicho cha ‘ushauri’ Seif Omar Ali, alisema kwa sasa wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji ya uhakika.

Alisema, kilimo chao kinategemea mno huduma ya maji kwa kiwango kikubwa, hivyo kwa sasa wamekuwa wakitumia maji kwenye mashimo waliyoyachimba kienyeji.

‘’Tumeshaanza na tunandelea kupanda mbegu za njugu mawe na nyasa, na tumeshaanza na kilimo cha matikti, lakini maji ndio changamoto hapa,’’alieleza.

Kwa upande wake Katibu wa kikundi hicho, Rashid Hamad Khamis, alisema wanamatumaini makubwa, kufikia ndoto zao ikiwa watapatiwa mikopo ya masharti nafuu, kuendeleza kazi zao.

Alisema, tayari ardhi wanayo na hamu ya kufanyakazi ipo, lakini suala la ukosefu wa mtaji ya uhakika, ndio jambo ambalo wanaendelea kuumiza kichwa.

‘’Ukiangalia kikundi hichi kimenzishwa mwezi Oktoba mwaka 2022, lakini kwa sasa tumeshapiga hatua, kwa kua na kilimo cha njugu na matikti tena kwa gharama zetu,’’alieleza.

Wanachama wa kikundi hicho Salim Ali Salim na mwenzake Salim Rubea, wamesema wanamatumaini kuwa, kuungana kwao katika kikundi hicho, matunda yatapatikana.

Kikundi cha ‘Ushauri’ cha watu wenye ulemavu mchanganyiko ambacho kinawanachama 15, wakiwa wanawake saba na wanaume wanane, kimeanzishwa Oktoba, 2022 na tayari kwa sasa wameshapanda njugu mawe, nyasa na matikti.

                          Mwisho    

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch