Skip to main content

TAMWA-ZANZIBAR, WAANDISHI WAZIJADILI SHERIA ZENYE MAPUNGUFU KATIKA KUPINGA UDHALILISHAJI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA::


MRATIBU wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, amesema sheria zenye mapungufu katika mapambano dhidi ya ukatili na udhalilishaji, ni changamoto nyingine inayohitaji kufanyiwa kazi.

Alisema kwa mfano, sheria Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, kwenye vifungu vyake vya 108 na 109 vilipotaja kosa la ubakaji na dhabu, hakuna adhabu sawa kwa washitakiwa wa kosa la aina moja.

Mratibu huyo aliyasema hayo Januari 24, mwaka 2023 ofisi ya TAMWA Chake chake Pemba, wakati akiyafunga mafunzo ya siku mbili, kwa waandishi wa habari, kwenye mradi wa Kuhamasisha hatua za kitaifa, dhidi ya kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji, unaoendeshwa na tasisi za TAMWA, KUKHAWA, TUJIPE, ZAFELA na ZAMWASO.

Alisema, bado sheria zinaendelea kuwaweka njia panda wananchi, kwa kule washtakiwa wa makosa ya ubakaji, kupewa adhabu tofauti, na sio iliyotajwa kwenye sheria husika.

‘’Kwa mfano, wapo wanaotiwa hatiani kwa ubakaji, hufungwa miaka 20, mwengine miaka 15 na mwengine miaka 30, hii ni kasoro inayohitaji, kufanyiwa kazi,’’alieleza.

Katika eneo jingine, Mratibu huo wa TAMWA Pemba, alisema bado kundi la watu wenye ulemavu na vijana, wamekuwa hawaamini na jamii hasa katika eneo la uongozi.

Alieleza kuwa, jamii imekuwa na mtazmo mbaya kuwa watu wenye ulemavu, hawezi kuongoza, jambo ambalo sio sahihi.

‘’Kwa kasoro ziliomo ndani ya baadhi ya sheria na imani potofu kwa jamii, ndio maana tunafanyakazi na waandishi wa habari, ili kwenda kuibua hayo, ili yafanyiwe kazi,’’alieleza.

Akiwasilisha mapungufu ya sheria mbali mbali, Mwanasheria wa serikali Ali Amour Makame, alisema yapo makosa kwa mfano kwenye sheria Adhabu kifungu cha 116, kunajisi mtu mwenye ulemavu awe mtoto, mtu mzima mtuhumiwa, anaweza kupewa dhamana.

Aidha alisema kasoro iliyopo, kosa la ubakaji kwa mtu mwenye akili timamu, mtuhumiwa hawezi kupewa dhamana, jambo ambalo linaukakasi.

Kasoro nyingine alisema, ni pamoja na upelelezi wa makosa ya udhalilishaji kukosa muda maalum, pamoja na kukosekana kwa miundombinu rafiki, kwenye mahakama ya watoto.

Hivyo Mwanasheria huyo, amesema hayo yanaweza kuwa vizuri ikiwa waandishi wa habari, watafanyakazi kazi zao kwa ufanisi.

Hassan Msellem mwandishi wa habari wa Bahari FM, alisema kuwa, kazi iliyoko mbele yao ni kuziibua changamoto hizo, ili kuona zinafanyiwa kazi, na ufanisi katika mapambano dhidi ya ukatili na udhalilishaji.

Salim Ali Msellem wa kituo cha redio cha Ist-qama, alisema kama kufanya mapenzi na mwari sio kosa, ni vyema sheria ikaliunganisha, kama ilivyo kumpa ujauzito kuwa ni kosa.

‘’Ukimpa ujauzito mwari kwa mujibu wa sheria ni kosa, usipompa sio kosa, sasa napendekeza yote haya yawe makosa, maana ni uvujifu wa maadili, kwa jamii,’’alishauri.

Kwa upande wake, Amina Ahmed mwandishi wa Zenj fm alisema, ni vyema sheria ya sasa ya mwari aliyepata ujauzito kutumikia jamii, iondolewe kwani, itakuwa amempa adhabu mara mbili.

Afisa mawasiliano wa TAMWA Pemba Gaspery Charles, alisema anawategemea sana waandishi hao, kwenda kuibua hayo, ili kuwa na sheria nzuri.

Awali mafunzo hayo yalifunguliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, ambae alisema, vyombo vya habari ni jukwaa muhimu katika mageuzi ya sheria mbali mbali.

Mradi huo wa miaka miwili, unafadhiliwa na the foundation for civil Society, na unaendeshwa na Jumuiya ya wanasheria wanawek Zanzibar ZAFELA, KUKHAWA, TUJIPE, ZAMWASO na TAMWA Zanzibar.

                                      Mwisho  

  

Comments

  1. Big up mafunzo ni mazuri sana ila msiangalie sheria moja tu bali sheria nyingi zinamapungufu

    ReplyDelete

Post a Comment

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch