Skip to main content

TAMWA-ZANZIBAR: VYOMBO VYA HABARI BADO NI JUKWAA PEKEE LA MABADILIKO

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA::

MKURUGENZI Mtendaji wa Chama Cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, amesema, bado vyombo vya habari vitaendelea kuwa tegemeo kwa jamii, katika kuwabadilisha kutoka mtazamo finyu na kwenda wenye tija.

Dk. Mzuru aliyasema hayo leo Januari 23, 2023 wakati akifungua mafunzo pacha, kati ya waandishi wa habari wa Unguja na Pemba, kwa njia ya kielektronik, kwenye mafunzoi ya siku mbili, chini ya mradi wa Kuhamasisha hatua za kitaifa dhidi ya kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji, unaoendeshwa na tasisi zaTAMWA, KUKHAWA, TUJIPE, ZAFELA na ZAMWASO.

Alisema, vyombo vya habari ni jukwaa muhimu na limeshafanya magauzi kadhaa, ikiwa ni pamoja na kusababisha kupatikana kwa sheria mbali mbali zikiwemo za kupinga udhalilishaji na adhabu zake.

Alieleza kuwa, ndio maana TAMWA katika kutekeleza kazi zote, lazima kuwashirikisha waandishi wa habari, ili kuhakikisha wanachotaka kukifanya, iwe rahisi kupata matokeo.

‘’Bado vyombo vya habari, vimekuwa eneo muhimu kwetu sisi wadau, kwa kule kufanya kazi zao kwa ufanisi, na kusababisha uwepo wa mabadiliko makubwa,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo Mtendaji wa TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, aliwakumbusha waandishi hao, kuendelea kuibua changamoto za uongozi kwa wanawake, watu wenye ulemavu na fursa za kiuchumi kwa vijana.

Akizungumza kabla ya mafunzo hayo, Mratibu wa TAMWA-Pemba Fat-hya Mussa Said, alisema mradi huo, unalenga kuibua changamoto, hasa zinazowakwaza wanawake na watu wenye ulemavu, zinazopelekea wasifikie malengo yao.

‘’Kundi la vijana, wanawake na watu wenye ulemavu nayo yanahaki sawa kama yalivyo mengine, sasa iweje yakose kuaminiwa na jamii, ni wajibu wa vyombo vya habari kwenda kuona nini tatizo,’’alihoji.

Akiwasilisha mada ya ushiriki na ushirikishwa wa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika siasa, uongozi, uchumi na fursa nyingine, mwanaharakati Sabah Mussa, alisema kama vyombo vya habari, vitatumia mbinu mbadala, makundi hayo yataishi kwa salama.

Alieleza kuwa, vyombo vya habari vimeshasababisha mabadiliko ya sheria na mitazamo mbali mbali, hivyo kama vitendelea kujengewa uwezo, makundi hayo yatapata haki za fursa zao.

Mwandishi wa Mawio online tv Suleiman Rashid, alisema bado elimu ya kujitambua kwa vijana inahitajika, ili waaminiwe ndani ya jamii yao, pale wanapotaka kugombea nafasi mbali mbali.

Mwandishi wa habari wa ZBC Pemba, Khadija Kombo Khamis, alisema uwezeshwaji na ufuatiliaji kwa vyombo vya habari, ni jambo moja, linalohitajika kufanyika.

Mwandishi wa blog ya pemba ya leo Fatma Hamad, alisema moja ya changamoto ambayo inaendelea kujitokeza na makundi hayo kukosa haki zao, ni elimu ya kuondoa dhana potofu kwa jamii.

Mradi huo wa miaka miwili, unafadhiliwa na the foundation for civil Society, na unaendeshwa na Jumuiya ya wanasheria wanawek Zanzibar ZAFELA, KUKHAWA, TUJIPE, ZAMWASO na TAMWA Zanzibar.

                                      Mwisho  

  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch