Skip to main content

CHANGAMOTO HEDHI SALAMA KWA WANAFUNZI PEMBA ZAELEKEA KUWA HISTORIA




NA BAKAR MUSSA, PEMBA:::
HEDHI ni hali ya mabadiliko katika mwili wa mwanawake ambayo hutayarisha nyumba ya uke kupata ujauzito.

 

Kila mwezi mji wa uzazi hupata kokwa ambapo mwanamke akipata ujauzito, mtoto ataweza kukuwa.

Ingawaje mwanamke asipo pata ujauzito, kokwa haihitajiki damu
itatokea ukeni na hiyo huitwa damu ya hedhi.

Wanawake wengi walio komaa, hupata hedhi, na wasichana hupata hedhi zao kati ya miaka tisa (9) na miaka 16, lakini huacha kupata hedhi wanapotimia miaka 50.

Mwanamke, akiwa na hedhi anapaswa kutumia visodo au pedi kuzuia damu, ambazo  zimeundwa na vifaa vya laini zinazo nyonya damu hiyo.

Kutokana na umuhimu wa jambo hilo Umoja wa Mataifa imetenga kila tarehe 28 mwezi Mei, dunia huadhimisha siku ya hedhi safi na salama.

Usafi ni jambo muhimu katika maisha ya mwanadamu, awe mke au mume lakini mwanamke inasisitizwa sana, kwa vile akifikia balegh huingia katika mazingira fulani ambayo humlazimu kila wakati kuhakikisha yuko msafi.

Wizara ya Elimu ndio mlezi mkubwa watoto, kwani hupata fursa ya kuwa nao kwa muda mrefu, hata kuliko kwenye familia zao ingawaje baadhi ya wakati wanafunzi hao wenye jinsia ya kike hukumbana na changamoto inayotokana na maumbile yao(Hedhi).

Itoshe kuzungunzia hilo ila tuone Wizara ya Elimu na mafunzo ya amali Pemba, inavyochukuwa juhudi ya kukabiliana na suala hilo kwa wanafunziwakiwa skulini.

Ofisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba Mohamed Nassor Salim, akizungumza na makala hii anasema, wizara imekuwa ikichukuwa juhudi ya kupambana na hedhi salama kwa wanafunzi, kwakuwapa stadi za maisha ‘ABC’ .

Anaeleza kuwa stadi za maisha hizo ni pamoja na kujitambuwa na udhalilishaji, kuwa salama na hedhi na kuimarisha miundo mbinu hususan yyoo.

 


Jengine anasema wapo waalimu wa kutosha wa ushauri nasaha wa msingi na sekondari, akimaanisha kila skuli lazima wawepo waalimu kati mmoja hadi wawili.

Kutokana na umuhimu wa kuwahifadhi wanafunzi wa kike waliofikia katika kuingia kwenye hedhi, wameamuwa kuwa na Ped za muda mrefu, kwa kuwafundisha kushona wenyewe na baadae kuzisafisha.

wakati mwengine hupata misaada mbali mbali ya PED na hivi sasa wanazo 3000 ambazo watazigawa kwa wanafunzi walioko katika dakhalia (mabweni) kwa wanafunzi wastani wa 314 kisiwani Pemba pekee.


Anafahamisha kuwa wanafunzi wa kike ambao wanatumia vifaa hivyo ni wengi, kwani hadi Septemba mwaka 2022 kutoka kidato cha kwanza hadi cha sita kwa Pemba wako wanafunzi 19,649 na Chuo cha Kiislamu pekee wako wasichana 488.


“ Hizi tulizonazo ni kidogo kulingana na idadi ya wanafunzi wa watu wa kike tulionao, ingawa tutaendelea kutafuta wafadhili wengine ili waweze kutusaidia na kuwapatia wanafunzi wetu”, anaeleza.

Ofisa mdhamini huyo anasema kuwepo kwa vifaa hivyo (Ped) litaondosha kabisa suala la wanafunzi ambao wamekuwa wakikata masomo kutokana na kupata siku zao za kawaida Hedhi.

“Suala hili la wanafunzi kukata masomo kutokana na kuingia katika kawaida yao (wanapopata hedhi) lipo, lakini limekuwa likiondoka kidogo kidogo na wizara inaendelea kupambana nalo.


 

Sasa akawaelekea wazazi na walezi watoe ushirikiano na hasa wasiwakatishe masomo wanafunzi kutokana na tatizo hilo waendelee kuwaamini kwani, wamewaandaliwa mazingira salama.

Ofisa huyo anaeleza wamekuwa wakipata wahisani mbali mbali wanaotowa elimu ya kujihifadhi kwa wanafunzi wa kike kama vile TAMWA, UNICEF na Serikali wenyewe.

Ofisa ushauri nasaha wa kujitegemea kisiwani Pemba Sabahi Mussa Said anasema,  wamekuwa mstari wa mbele kutowa ushauri nasaha pale wanapokutana na wanafunzi ili kukabiliana na hali hiyo.

Anaeleza kuwa mbali na wizara ya elimu kuchukuwa juhudi katika kukabiliana na tatizo hilo, lakini zimekuwepo na taasisi mbali mbali, ambazo hutoa mafunzo kwa walimu iliwaweze kukabiliana na suala la hedhi salama kwa wanafunzi.

“Ushauri nasaha umekuwa juu ya tatizo hili, umekuwa ukitolewa na taasisi mbali mbali, kwani sio jambo la mtu mmoja unapomuelimisha mwanamke mmoja ni sawa kuielimisha jamii mzima”, alisema.

Mfano wa taasisi hiyo ni KFHI ( yaani mradi wa wajengea  uwezo walimu katika mazingira rafiki ya moto wa kike) unaofadhiliwa na Korea ambao kwa Zanzibar umeshatowa mafunzo kwa skuli 5.

 

Ikiwa ni pamoja na kwa Pemba skuli ya sekondari Shumba Vyamboni na Chwaka Tumbe sekondari.

Ambapo mkurugenzi wa mradi  huo Esther Mwakarobo anaeleza kuwa lengo la mradi huo, ni kutaka kutengeneza mazingira rafiki kwa wanafunzi hasa wa kike.

 

Hasa wakati anapokuwa skuli, ambapo itasaidia kuondoa changamoto ambazo zinaweza kujitokeza, wakati wakiwa katika kipindi cha Hedhi.

 Esther anasema, kuwa wameamua kuendesha mradi huo kwa upande wa Zanzibar, kutokana na kuona kuna uhitaji na kuangalia miundombinu iliyopo, katika skuli hizo ina mapungufu.

“ Mradi wetu huu tutauwendesha katika Skuli tano za Zanzibar, ikiwa Pemba ni Skuli ya Sekondari Chwaka Tumbe na Skuli ya Sekondari Shumba Vyamboni huku Unguja ni Paje Mtule, Fukuchani na Jendele," alisema Park.

Anafahamisha usafi usipozingatia katika kipindi cha Hedhi kunaweza kusababisha maambukizi katika mfumo wa uzazi na kwenye njia ya mkojo hivyo huathiri afya ya mwanafunzi.

“Tunavyozidi kukuwa mabadiliko mbali mbali ya matokeo ya miili yetu hutokea ikiwemo hedhi kwa Wasichana , mabadiliko haya ni kawaida na husababishwa na vichecheo ndani ya miili yetu”, anaeleza.

Anasema ni muhimu kuweka miili ya wasichana katika hali ya usafi kwa kipindi chote cha Hedhi kwa kutumia taulosafi za wasichana ambazo wanaweza kuzitengeneza majumbani au kununuwa madukani.

Nae Taiwa Park kutoka mradi huo wa KFHI unaofadhiliwa na KOICA na kwa ushirikiano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  anaeleza kuwa mradi huoutakuwa ni wa miaka (3) na utatoa elimu kwa wanafunzi wapatao 1,300 na walimu 100 kwa Skuli tano (5).




“ Tumeamuwa kutowa mafunzo haya kwa walimu na wanafunzi ili
kuwawezesha wanafunzi kuweza kujitambuwa zaidi na kutumia vifaa ambavyo vitawasaidia kujistiri wakati wa hedhi na watapata kuhudhuria masomo kama kawaida na sio kukata kata kila mwezi”, anasema.

Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Sekondari Shumba Vyamboni Khatib Rashid Mwinyi alieleza kuwa katika Skuli yake, yako matatizo mbali mbali ambayo huwa yanawakabili watoto wa kike hasa pale wanapokuwa katika hedhi.

"Mara nyingi watoto wa kike wanapopata hedhi wakiwa Skuli kiukweli hatujui  nini cha kufanya, lakini kupitia elimu tuliyoipata ni dhahiri tutaweza kuitumia vyema katika mazingira yetu ya Skuli kwa watoto wetu," alisema.

Nae Mwalimu mkuu wa skuli ya sekondari Chwaka Tumbe Hamad Dadi Khamis, anasema kuwa mafunzo hayo wataweza kuyatumia vizuri, kwa kuwahamasisha wanafunzi pamoja na jamii kwa ujumla, ili kudumisha usafi wa mazingira yao.

Dadi anafahamisha kuwa elimu ya afya ni jambo zuri sana, hivyo ni wajibu wa jamii kushirikiana pamoja katika kuendeleza jambo hilo.



"Kabla ya kupata elimu hii changamoto nyingi zilikuwepo lakini
tulikuwa tunasaidiana na wizara katika kuzitatua," anasema Dadi.

Nae Mwalimu Salma Tahir Omar kutoka Skuli ya Sekondari Shumba Vyamboni anasema changamoto kubwa ni ukosefu wa taula za kike (pedi) hivyo wanafunzi kushindwa kuwasaidia wanapopatwa na hedhi.


Hata hivyo kwa sasa Skuli imeamua kununua taulo  hizo (pedi) na kuweka akiba ili mwanafunzi anapopatwa na tatizo hilo waweze kumsaidia na kuondokana na usumbufu wa kurudi nyumbani na kukosa  masomo.

Mwanafunzi ambae hakutaka jina lake litajwe  nasema  wamekuwa wakipatiwa ushauri nasaha kutoka Skuli na hivyo umewasaidia sana na wamekuwa wakihudhuria madarasani kama kawaida ingawaje kuna changamoto wanazokumbana nazo baadhi ya wanafunzi ikiwemo kuumwa na tumbo.


Anafahamisha kwa sasa wanafunzi waliowengi wamekuwa wakihudhuria Skuli kama kawaida, na wala hawajuilikani wako katika kipindi hicho, kwani kunataaluma mbali mbali wanazopewa na walimu wao.

“ Tumekuwa tukihudhuria masomo yetu bila ya wasi wasi wowote hata tukiwa katika siku zetu za Hedhi, na wala huwezi kumuelewa mtu kirahisi kuwa yuko na hedhi,”alieleza.

Hapo awali baadhi ya wanafunzi  wa kike hususan wale ambao
wameshafikia umri wa baleghe, walikuwa wakikata masomo kila mwezi kutokana na kuingia katika siku zao(hedhi) iliosababishwa na kukosa elimu juu ya kujitambuwa na  kujihifadhi.

                        MWISHO





 

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch