Skip to main content

FEDHA ZA UVICO19 ZAPUNGUZA MSONGAMANO WA WANAFUNZI MADARASANI PEMBA

 



NA BAKAR MUSSA, PEMBA::

MARCH 2020 Tanzania, iligundua kesi ya mwanzo ya ugonjwa Corona baada ya dunia kugubikwa na janga kubwa la uwepo wa gonjwa huo, 'UVICO19' ambalo ulianza mwezi disemba 2019 nchini China.

Licha ya Zanzibar kupoteza roho za watu wake kadhaa, lakini pia kwa kiasi fulani, iliathirika kiuchumi, ijapo kwa asilimia ndogo kutokana na watalii kutoingia kwa kasi kama ilivyozoeleka.

Ikumbuke kuwa, ugonjwa huo unaelezwa unasambaa kwa kasi kutokana na kuwepo kwa makaazi ya watu karibu (msongomano) na hivyo kuwepo na hadhari ya kutokukaa karibu na kuvaa Mask (Barkoa).

 Kwa vile ugonjwa huo ulitawala dunia nzima, ni wazi kulitokea mtikisiko wa uchumi, ingawa waswahili husema ‘Mwenyeezi Mungu akikupa kilema hukupa na mwendo’.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ilipata mkopo wa fedha kutoka Umoja wa Mataifa, baada ya kuonekana nchi nyingi kukumbwa na ukosefu mkubwa rasilimali fedha za kujiletea maendeleo kutokana na kuwepo ugonjwa huo.

Zanzibar ikiwa ni nchi mbili zilizounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nayo ilifaidika kutokana na fedha hizo na kuziekeza katika maeneo mbali mbali.

Sina nia kubwa ya kuelezea kuhusiana na gonjwa la Covid 19 lilivyoingia, bali ni kuelezea fedha hizo za Covid 19 zilivyoifaidisha Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na watu wake walivyofaidika kupitia miradi ilioanzishwa na mfuko huo.

Zanzibar, imekuwa na miradi hiyo nilioeleza lakini leo nitagusia ujenzi wa madarasa katika skuli za msingi na Sekondari kisiwani Pemba, ulivyoweza kuondoa msongamano wa wanafunzi madarasani.

Akizungumza na makala hii, Ofisa Mdhamini Wizara ya Elimu na mafunzo ya amali Pemba, Mohamed Nassor Salim, anasema ujenzi wa madarasa ya skuli yaliojengwa, kupitia fedha za ahuweni wa mfuko wa Covid19, utapunguza kwa kiasi kikubwa, japo hautaondosha kabisa tatizo liliopo.

Madarasa hayo licha ya kupunguza wimbi la uwepo wanafunzi wengi madarasani, lakini pia utapunguza masafa kwa wanafunzi kufuata elimu, wimbi la utoro, udhalilishaji.

Wastani kila darasa la mita 7 hadi 8, watakaa wanafunzi 45 hadi 50, ingawa lakini kwa Pemba wanakaa 120 wa msingi na Sekondari na maandalizi ni 25 lakini wanakaa 90 hadi 120.

Anasema uwepo wa wanafunzi wengi madarasani, waalimu hufundisha kwa kutumia mbinu shirikishi kwa  kuuliza masuali na humfanya atumie mbinu ya muhadhara ya kufundishia ambayo sio njia nzuri.

Anaeleza kuwa ujenzi wa madarasa hayo, mkoa wa kusini Pemba yalijengwa 143 na kaskazini 208 , madarasa ya chini mkoa wa kusini ni 63 na ghorofa 3 na vyumba 8 vya wanafunzi wa mahitaji maalumu .

Na mkoa wa kaskazini 203 ya chini na ghorofa vyumba 21 ambapo katika kisiwa cha Pemba kina wanafunzi zaidi 174,000.

Madarasa ya chini kwa mkoa wa kusini yametumia shilingi bilioni 2.6, wakati yale ya ghorofa tatu kwa mkoa wa kusini, yametumia wastani wa shilingi 4.3, ambapo mkoa wa kaskazini zilitumika shilingi bilioni 3.6 ya chini na ya ghorofa ni shilingi bilioni 1.2 .

Ofisa Mdhamini wa wizara ya elimu na mafunzo ya amali anasema skuli zinazoingia katika mikondo miwili nyingi, zikiwa ni za msingi na mikondo 3 ni Skuli za Mwambe pekee kwa Pemba.

Ingawaje kwa asilimia kubwa tatizo la uwepo wa wanafunzi wengi madarasani, litaondoka kwa skuli za sekondari.

Anasema kuna tafauti ya saa 1.15 ya masomo wanayoingia wanafunzi wa mkondo mmoja na wanaoingia mikondo 2 na 3, kwani  wanaoingia mkondo mmoja husoma masaa 7.15 mpaka 30 na mikondo miwili husoma kwa masaa 6, hivyo kunaupotevu wa masaa ya masomo.

“ Kwa vyovyote kutakuwa na tofauti ya muda wa masomo baina ya wanafunzi, wanaoingia skuli mkondo mmoja na mikondo miwili na mitatu lakini uwepo wa madarasa haya ya Uviko 19 utapunguza tafauti hiyo”, anaeleza.

Nae Msimamizi mkuu wa  wa miradi ya maenedeleo ambayo inatekelezwa kupitia fedha za ahuweni ya  uviko 19, mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, anasema hatua iliyofikiwa katika ujenzi ni kubwa.

Anaeleza ni faraja iliopo, kwa wananchi wa mkoa wa kaskazini na pemba kwa ujumla kupata madarasa mengi, ambayo yako ya ghorofa na ya chini yote ni juhudi za Dk. Mwinyi kuwawekea mazingira bora ya kusomea watoto wa Zanzibar.



Kwa upande wake Ofisa Elimu na mafunzo ya Amali mkoa wa Kaskazini Pemba maalim Khamis  Said Hamad anasema, idai ya wanafunzi wakiwa wengine madarasani, changamoto kadhaa hujitokeza ikiwa ni pamoja na kupoteza ufahamu.

''Ujio wa madarasa haya ya UVICO ndani ya mkoa wangu, sasa utakwenda kuondoa msongamano wa wanafuzi madarasani na kuchechemua ufahamu wa wanafunzi,''anasema.

“ Kwa mfano skuli ya Makangale ambako wanafunzi wanaingia mikondo miwili, ingawa kwenye ujenzi huu wamejengewa vyumba 20 vya madarasa, hii ni wazi kuwa, kuna mwanafunzi wa sekondari atakae atakaeingia mikondo mwili”, anafahamisha.

Anaeleza kuwa ndani ya mkoa huo kuna Skuli nyingi ambazo zilikuwa na wanafunzi wanaoingia mikondo miwili litaondoka tatizo hilo kama vile skuli ya Micheweni, Maziwani,Tumbe.

Anasema  ziko skuli 43 kati ya hizo ni asilimia 5 zilikuwa zinaingia mkondo mmoja , kwa uwepo madarasa ya Uviko asilimi 40 ya skuli za sekondari zitakuwa zinaingia mkondo mmoja ,ingawaje kwa msingi haitokuwa rahisi kuingia mkondo mmoja.



Kwa upande wa Ofisa Elimu wilaya ya Mkoani Mohamed Abdalla Omar anasema, kutokuwepo madarasa ya kutosha, kuna tatizo kwa wanafunzi kutokujifunza kwa ufanisi.

Idadi ya wanafunzi wanaoandikishwa, imekuwa ikiongezeka kila mwaka na hupelekea kuwa kero kwa mwalimu katika ufundishaji kwani hamudu kufanya wajibu wake ipasavyo.

Kwa mwaka 2021 pekee, wilaya ya Mkoani wanafunzi 3,608 waliandikishwa katika madarasa ya maandalizi, Tutu waliandikishwa 3,846 na skuli za maandalizi za binafsi 439.




Omar Ali Omar ni mwalimu wa msingi katika skuli ya Shengejuu anasema serikali ya awamu ya nane, imejitahidi kujenga madarasa hayo kila skuli.

Alisema kuwepo kwa wingi wa wanafunzi darasani kunakuwa na changamoto kubwa hata wanafunzi, wanakosa kupata ufahamu kama inavyotakiwa. 

“Mimi kwa hili niseme Serikali imefanya jambo jema sana, kwani kuwekeza katika elimu ni jambo la msingi sana, sasa ni juhudi za wanafunzi na waalimu kwani mazingira ya kusomea yako vizuri”,alisema.

Nao Wazazi wa wanafunzi Ali Mohamad Issa wa Wingwi anasema uwepo wa ujenzi wa madarasa mapya kupitia Uviko 19, umeleta faraja kubwa sio kwa Wizara ya Elimu pekee bali hata kwa wazazi.

“ Sisi wazazi tutaondokewa na michango ya kila siku, ambayo tumekuwa tukichangia kwa ujenzi wa madarasa, igawaje ujenzi wa madarasa hayo ya Uviko 19 hayawezi kuondowa tatizo la wingi wa wanafunzi madarasani moja kwa moja”, alieleza.


Anaeleza kila wakati wanafunzi walikuwa wakidai mchango kwa baadhi ya Skuli, kwa ajili ya kuongeza madarasa wako waliofanikiwa na wako wasiofanikiwa kutokana na hali za wazazi zilivyo.

Anasema lakini kwa usimamizi wa Dk. Hussein Mwinyi kupatikana kwa fedha hizo za Uviko 19 kwa sasa hakuna pahala ambapo hakuna ujenzi wa madarasa mapya hii ni hatuwa kubwa sana kwao.


                      MWISHO.

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch