Skip to main content

JAJI MSTAAFU LUANDA, ACHAGULIWA RAIS MCT

 

 

NA HAJI NASSOR, DAR-ES SALAAM@@@@

WANACHAMA wa Baraza la Habari Tanzania MCT, wamemchagua Rais mpya wa Baraza hilo, Jaji Mstaafu: Bernad Luanda, kupitia mkutano mkuu wa 26, uliofanyika Septemba 27, 2024 ofisi za ‘MCT’ Tegeta nje ya jiji la Dar-es Salaam.

Kati ya wanachama hai 29, waliohudhuria mkutano huo, waliomchagua rais huyo ni wanachama 27, kura moja ikimkataa na moja iliharibika, ambapo kisha Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi Nicholaus Mwaibale alimtangaaza.  

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi huo, Katib Mtendaji mpya wa baraza hilo Ernest Sungura, alisema kwa sasa baraza linakuja kivingine, lengo likiwa ni lile lile la kuwanoa waandishi wa habari.

Alisema, kuanzia mwakani, MCT itakua na mradi mkubwa unaojulikana kwa jina la ‘WAJIBIKA’ambao utakuwa wa miaka saba.

Alisema, mradi huo wa paund milioni 30, utagusa karibu kila eneo, ikiwemo kuwajengea uwezo hata waandishi wa habari mmoja mmoja, kupiti vyombo vyao.

Alieleza kuwa, jingine ambalo litafanyika mwakani, ni sherehe kubwa na za aina yake, ya mafanikio ya ‘MCT’ kwa miaka 30, tokea lilipoanzishwa mwaka 1995.

Katibu Mtendaji huyo mpya, aliwataka wanachama wenye madeni, ambayo kwa mwaka huu yamefikia shilingi milioni 167, kulipa haraka, ili kulipa uhai baraza hilo.

‘’Wanachama ambao wana deni la kufikia miaka 10, ni wengi na ndio maana, linafikia wastani wa shilingi million 167, fedha ambayo yengetusaidia, katika utendaji wa kazi zetu,’’alifafanua.

Aidha Katibu huyo Mtendaji, aliwapongeza waandishi wa habari kutoka kisiwani Pemba, kwa kujitokeza kwa wingi, katika kuwasilisha kazi za kutafuta mshindi wa tunzo za uhamiri wa mwandishi wa habari Tanzania ‘EJAT’, mwaka 2023/2024.

Nae Makamu wa Rais wa ‘MCT’ Yussuf Khamis, alisema anajivunia umoja na mshikamano, uliopo baina ya wanachama na watendaji wa MCT.

Hata hivyo, alisisitiza haja kwa wanachama wenye madeni, kusawazisha, ili kuona ‘MCT’ haitegemei mno fedha za wafadhili, katika kujiendesha kwake.

Akiwasilisha ripoti ya fedha, ya mwaka 2023, ‘CPA’ Happiness Nkya, alisema walipata mapato ya shilingi bilioni 1.1, ambapo ni punguzo la shilingi milioni 600, ikilinganishwa na shilingi bilioni 1.6 za mwaka 2022.

Alieleza kuwa, kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 1.0 ni za wafadhili na shilingi million 38 ni michango ya ndani, ikiwemo ada ya mwanachama wa MCT.

Hata hivyo, alisema katika ukaguzi uliofanyiwa, wamepata hati safi, jambo linaloonesha kuendelea kufuatwa kwa taratibu za manunuzi na matumizi.

Baadhi ya wanachama akiwemo mwandishi Jabir Idrissa kutoka Zanzibar, alisema ujio wa baraza huru la habari la serikali, isiwe sababu ya MCT kujiondoa.

‘’Hapa chakuzingatia tupate uzoefu katika baadhi ya nchi, kuona wanakwenda vipi, wanapokuwa na baraza la habari la serikali na lile binafsi kama MCT,’’alifafanua.

Nae rais wa Umoja wa Vilabu vya waandishi wa habari Tanzania ‘UTPC’ Keneth Simbaya, alimpongeza Katibu Mtendaji mpya wa MCT kwa maono yake, katika kulivuusha baraza hilo.

Nae Issaya Kisibuli kutoka Gazeti la Jibu la Maisha, aliomba wanachama ambao wanamadeni, kufuatiliwa kwa kina, ili waeleze sababu na misimamo yao.

Wakati huo huo, mkutano huo umewapitisha wanachama wapya kadhaa, ikiwemo blog ya Pemba tody, Bahari Media, Trust Media Agency, Star Tv, Pemba ya leo blog, star tv pamoja na Redio free Afrika.

     Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan