Skip to main content

WAZAZI WATAKIWA KUWALEA WATOTO WAO KATIKA MAADILI MAZURI

 


IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@

WAZAZI na walezi wa shehia ya Kambini Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba wametakiwa kujitathmini na kuweka mikakati katika malezi, ili jamii iwe na vijana wenye malezi bora na maadili mema.

Akizungumza na wanajamii hao katika mkutano wa elimu ya udhalilishaji na kutambua haki zao, Msaidizi wa Sheria Wilaya ya Wete ambae pia ni Mkaguzi wa Shehia hiyo kutoka Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Khamis Shoka Ame alisema wazazi waliowengi wamefeli katika malezi.

Alisema kuwa, mporomoko wa maadili wameusababisha wenyewe wazazi kwa kukosekana kwa malezi ya pamoja, hivyo kuna haja ya kujitathmini na kuweka mikakati imara ili kizazi chao kiweze kukuwa katika maadili mema na malezi bora.

‘’Watoto tunawalea sisi lakini hawaendi skuli wala madrasa, wanaingia ndani usiku mkubwa, halafu wanakwenda nae Jeshi la Polisi kusema kuwa mtoto amemshinda, lakini tujue kwamba mwenye jukumu la malezi ni wewe mzazi, hivyo tujitahidi sana kwani tunapofeli hapo ndipo tunapofeli kwenye maisha,’’ alieleza.

Aidha Shoka alisema kuwa, wananchi wana tabia ya kusuluhisha kesi wenyewe kutokana na muhali walionao, jambo ambalo linasababisha matukio ya udhalilishaji na wizi kuongezeka kila siku.



''Kesi hizi sana zinafanyika wenyewe kwa wenyewe, hivyo kesi inakaa mahakamani au Polisi kwa muda mrefu huku ikisubiri maelezo kutoka kwa waathiriwa, lakini mwisho wa siku kumbe wameshakaa kikao cha kusuluhisha, hii haikubaliki na tunachangia kuongezeka kwa matendo maovu katika jamii yetu,’’ alieleza.

Kwa upande wake Hakimu wa Mahakama ya Wilaya Wete Maulid Hamad Ali alisema, kutokujua sheria ni changamoto kubwa inayowakabili wanajamii, ambapo husababisha kukoseshwa au kuvunjiwa haki zao.

‘’Mtu yeyeyote hana kosa mpaka pale mahakama itakapomtia hatiani, kwa hivyo huwa anatuhumiwa tu kutenda kosa na pia Polisi inapokuja kufanya upekuzi ni lazima awe na kibali maalumu, hivyo mnatakiwa kuzijua sheria zenu ili ziweze kuwasaidia,’’ alisema Hakimu huyo.

Nae sheha wa shehia hiyo Ali Omar Ali alieleza kuwa, watu wengi wanaishi ingawa hawajui sheria ambazo ndizo zinazowasababishia kufanya mambo maovu, hivyo wamefarajika sana kupata elimu hiyo kwani anaamini itawasaidia katika utatuzi wa changamoto mbali mbali kwenye jamii.

‘’Nawaomba wananchi kuacha tabia ya kuwakingia kifua wabakaji kwa sababu wanaendelea kudhalilisha watoto huku wakidunda mitaani, tuwafikishe kwenye vyombo vya Sheria na tuwe tayari kutoa ushahidi,’’ alisema sheha huyo.



Mapema wakitoa malalamiko yao wananchi wa shehia hiyo walieleza kuwa, waliomba kufahamishwa Sheria ili wazielewe vizuri hali ambayo itasaidia kujua na kutetea haki zao kisheria endapo zitavunjwa.

Mkutano huo ni muendelezo wa mikutano ya kutoa elimu kwa wananchi ili wajue haki zao kisheria, ambao umeandaliwa na Jumuiya ya Wasaidizi wa Sheria Wilaya ya Wete (WEPO) chini ya ufadhi wa Shirika la UNDP.

                                                          MWISHO.     

                                                     

                                                              

                                 

 









Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan