Skip to main content

TULIA ACKSON MGENI RASMI LEO HAFLA UTOAJI TUNZO

 


NA HAJI NASSOR, DAR-ES-SALAAM@@@@

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Tulia Ackson, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi, jioni ya leo Septemba 28, 2024 kwenye hafla ya 15 ya kuwakabidhi tunzo waandishi wa habari mahiri.

Tunzo hizo ambazo zimekuwa zikiandaliwa na Baraza la Habari Tanzania ‘MCT’, kwa mwaka wa 15, tokea zilipoanzisha mwaka 2009, zinatarajiwa kufanyika ukumbi wa AGA KHAN DIAMOND JUBILEE eneo la Upanga jijini Dar-es Salaam.

Akitoa taarifa hiyo jana, Katib Mtendaji mpya wa ‘MCT’ Ernest Sungura, alisema matayarisho yote yameshakamilika ikiwa ni pamoja na kupatikana kwa mgeni rasmi huyo.

Alisema, Spika huyo ndie atakaemkabidhi mshindi wa jumla kwa mwaka 2023/2024, huku washindi wingine mbali mbali wakikabidhi zawadi na tunzo zao, na wageni mashuhuri waalikwa.

Alieleza kuwa, katika hafla inayofanyika jioni hii ya leo, kutakuwa na mambo kadhaa mazuri ikiwa ni pamoja na zawadi kwa mwandishi nguli aliyefanya vyema zaidi katika maisha yake ya kihabari.

 Akizungumzia kuhusu zoezi hilo, alisema Majaji saba wa Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) wamehitimisha kazi ya kutathmini ubora na weledi wa kazi zipatazo 1,135 na kuwateua waandishi wa habari 72 watakaoingia katika kinyang’anyiro cha kumtambua mshindi wa kwanza, wa pili na wa tatu na mshindi wa jumla.

Kati ya waandishi wa habari 72, wanaume ni 45 (sawa na 62.5%) na wanawake 27 (sawa na 37.5%). Kati ya wateule hao, wateule 14 (19%) wanatoka katika runinga; 13 (18%) wanatoka vyombo vya mtandaoni, redio 20 (28%) na wateule 25 (35%) wanatoka kwenye magazeti.

Wateule wamepatikana kwa kukidhi vigezo vya ubora ambavyo ni pamoja na ukweli, usahihi, uanuai, haki, kina, utafiti, ubunifu, uvumbuzi, upekee, uchambuzi, uwajibikaji, ufichuaji maovu, uadilifu, uwasilishaji unaoeleweka na uchunguzi. Ifahamike pia kwamba vigezo maalum vilitumika kuzingatia aina tofauti ya vyombo vya habari kama vile redio, televisheni, magazeti na habari za mitandaoni.

Kabla ya kutaja majina ya wateule hao 72 ni muhimu ifahamike kwamba kinyang’anyiro cha kumtambua mshindi wa kwanza, wa pili na wa tatu na mshindi wa jumla kwa makundi 20 ya kushindaniwa kitakuwa jioni ya leo.

Alifafanua kuwa, moja ya jambo la kipekee katika kilele cha kinyang’anyiro hicho ni pamoja na kusikia kutoka kwa jopo la majaji kuhusu viwango vya uandishi wa habari za magazeti, redio, televisheni na mitandaoni  kwa habari zilizohusu uwekezaji wa kampuni ya DP world katika bandari za Tanzania, habari kuhusu Ngorongoro na wamasai na kuhusu maporomoko ya Hanang.

Jambo la pili la kipekee ni kumshuhudia Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Jerry Silaa akizindua Jarida la Tuzo na Tuzo magazine ambayo yanajikita kuhamasisha umahiri katika sekta mbalimbali Tanzania na nje ya Tanzania. Kwa kuanzia majarida hayo, moja la Kiswahili na lingine la Kiingereza yatabeba maudhui ya tuzo za umahiri wa uandishi wa habari Tanzania (EJAT).

Aidha ikumbukwe kuwa kwa mara ya kwanza kazi za kihabari kwa EJAT 2023 zimeongezeka hadi 1,135 kutoka kazi 893 za EJAT 2022. EJAT 2020 kazi zilikuwa 396 na EJAT 2021 kazi zilikuwa 608.

Taasisi zinaounda Kamati ya Maandalizi ni Wakfu wa Vyombo vya Habari (TMF), Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Jukwaa la Wahariri (TEF), HakiElimu, Umoja wa Waandishi wa Habari za Mazingira (JET)Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Umoja wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Sikika, Misa –  Tan  na Twaweza.

Sasa nimalizie kwa kusoma orodha ya wateule wa EJAT 2023 pamoja na vyombo vyao:

 

NA.

JINA

JINSIA

CHOMBO

MKOA

1

Thomas Masalu Lunyalo

M

Mazingira FM

Mara

2

Abdallah Bakari Nassoro

M

Nipashe

Mtwara

3

Jacob Mogesi Musenda

M

The Citizen

Dar es Salaam

4

Marco Maduhu

M

Shinyanga Press Club

Shinyanga

5

Salum Vuai Issa

M

Zanzibar Leo

Zanzibar

6

Jackline Victor Kuwanda

F

The Chanzo

Dodoma

7

Stanslaus Lambert

M

Swahili 360

Dar es Salaam

8

Zacharia Nyamoga

M

IPC Mkombozi TV

Iringa

9

Irene Mwakalinga

F

TBC1

Iringa

10

Said Ally Sindo

M

Storm FM

Geita

11

Joshua Stephen

M

Nukta

Dar es Salaam

12

Samweli Mpogole

M

Highlands FM

Mbeya

13

Shekha Suleiman

F

ZBC

Pemba

14

Abel Kilumbu

M

Dar 24

Dar es Salaam

15

Khamis Mohamed

M

Zanzibar Leo

Zanzibar

16

Abdiel Jumanne Siffi

M

UFM

Dar es Salaam

17

Julius Maricha Maricha

M

The Citizen

Dar es Salaam

18

Eliya Solomon

M

Mwanaspoti

Dar es Salaam

19

Huwaida Nassor Moh’d

F

As Salaam FM

Zanzibar

20

Rehema Evance Mwaikema

F

UTV

Simiyu

21

Philip Mwihava Mwihava

M

Clouds FM

Dar es Salaam

22

Zourha John Malisa

F

Mwananchi

Dar es Salaam

23

Linus Ananias Gamarwa

M

TBC

Dodoma

24

Catherine Sekibaha

F

Pangani FM

Pangani Tanga

25

Herieth Makwetta

F

Mwananchi

Dar es Salaam

26

George Helahela

M

Mwananchi

Dar es Salaam

27

Esau Ezra Ng’umbi

M

Nukta Habari

Dar es Salaam

28

Benson Eustace Jacob

M

UTV

Kagera

290

Mariamu Ally Abdallah

F

Pangani FM

Tanga

30

Adam Gabriel Hhando

M

CG FM

Tabora

31

Sanula Renatus Athanas

M

Nipashe

Dar es Salaam

32

Elizabeth Edward Kusekwa

F

Mwananchi

Dar es Salaam

33

Pamela Nasphory Chilongola

F

Mwananchi

Dar es Salaam

34

Rodgers Simon

M

ITV

Dar es Salaam

35

Mukrim Mohamed Khamis

M

KTV TZ Online

Zanzibar

36

Ephrahem Edward Bahemu

M

Mwananchi

Dar es Salaam

37

Mkwaji Reuben Masatu

F

UTV

Dar es Salaam

38

Lukelo Francis Haule

M

The Chanzo

Dar es Salaam

39

Benjamin Mzinga

M

ITV

Dar es Salaam

40

Dickson Shukran Kanyika

M

RFA

Njombe

41

Hamisi Makungu Hamisi

M

Pangani FM

Pangani Tanga

42

Halfan Chusi

M

Nipashe

Dar es Salaam

43

Kelvin Paul Matandiko

M

Mwananchi

Dar es Salaam

44

Waryoba Musa Waryoba

M

Montessory Tanzania

Mwanza

45

Anna Peter  Mbuthu

F

TBC

Arusha

46

Egan Salla

M

BBC

Dar es Salaam

47

Imma Rashid Mbuguni

M

Majira Online

Dar es Salaam

48

Haika E. Kimaro

F

The Citizen

Mtwara

49

Margareth Msafiri Geddy

M

TBC Safari

Dar es Salaam

50

Yohana Chance Challe

M

Mwanaspoti

Mbeya

51

Mgongo Kaitira Mafuru

M

Mwananchi

Mwanza

52

Mercy Yasin Mbaya

F

UTV

Dar es Salaam

53

Imani Raphael Makongoro

F

Mwananchi

Pwani

54

Fatma Abdallah Chikawe

F

UTV

Dar es Salaam

55

Brown Benny Mbwawa

M

Wasafi FM

Mbeya

56

Ayoub Stanley Nyondo

M

Shamba FM

Iringa

57

Warioba Igombe Warioba

M

Uhuru

Mara

58

Salome Gregory Sumbya

F

The Citizen

Dar es Salaam

59

Veronica Natalis Mataba

F

DW Swahili

Arusha

60

Saa Mbwana Zumo

F

Pangani FM

Pangani Tanga

61

Said Ali Ngamba

M

Uyui FM

Tabora

62

Lugendo Madege

M

UFM

Dar es Salaam

63

Anna Potinus

F

Mwananchi

Mwanza

64

Christina Mwakangale

F

Nipashe

Dar es Salaam

65

Rauhiya M Shaban

F

Bomba FM

Zanzibar

66

Hazla Omary Quire

F

The Tanzania Times

Arusha

67

Lucy Patrick Samson

F

Nukta

Dar es Salaam

68

Mohamed Hammie Rajabu

M

Habari Leo

Dar es Salaam

69

Amina Deogratias Semagogwa

F

Radio Kwizera

Kigoma

70

Hellen Nachilongo Mkisi

F

The Citizen

Dar es Salaam

71

Alfred Bulahya Jakuba

M

Dodoma FM

Dodoma

72

Waziri Iddi Suka

M

Tumaini TV

Dar es Salaam

Hongereni sana kuingia katika kinyang’anyiro cha Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) 2023.

Ernest S. Sungura

Mwenyekiti

Kamati ya Maandalizi ya EJAT 2023

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan