Skip to main content

Wawakilishi wanawake waupiga mwingi majimboni 'Watatua changamoto lukuki, wananchi wafurahia'

 



 

NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@

 

Katika majimbo mengi Unguja na Pemba ni kawaida kusikia malalamiko ya waliochaguliwa kuingia Baraza la Wawakilishi, Bunge na Udiwani nadra kuonekana, tafauti na walipohangaika kuchaguliwa.

 

Hii ilipelekea majimbo mengi kuzorota kimaendeleo kwa vile hapakuwepo watu waliohangaikia shida zao na kilichosikika ni wananchi kulalamika kwamba waliowachagua kupeleka mbele madai yao hawaifanyi kazi kama walivyotarajia.

 

Hali ilianza kubadilika hivi karibuni kutokana na kuibuka wanawake majasiri na wanaojituma kuhangaikia kero hizi baada ya kushika hatamu za uongozi katika ngazi mbali mbali.

 

Wapo watu waliodiriki kusema laiti zamani kungekuwa na wawakilishi wanawake kama hawa waliopo sasa, matatizo ya majimbo mengi yangepatiwa ufumbuzi na yangepungua.

 

Licha ya kuwepo viongozi wanawake wachache, lakini kazi waliyoifanya wengi wao ni kubwa na inathibitisha maelezo ya kwamba siku zote mama huwa na huruma na ndio maana wawakilishi wanawake wanatumia vizuri fedha za mfuko wa Jimbo na wakati mwengine wanatoa mifukoni mwao ili kusukuma gurudumu la maendeleo katika majimbo yao.

 

Uchache wao haukuwa sababu wasitekeleze walichowaahidi wananchi na wamejitokeza kusimama kidete kuhakikisha wanatimiza ndoto za wananchi waliowapa nafasi za uongozi.

 

Zanzbar inayo wawakilishi wanawake 29, wakiwemo wanane (8) waliochaguliwa, 18 viti maalumu na watatu (3) wateule wa Rais.

 

Wote wanafanya kazi vizuri kwa kila siku kuibua matatizo ya wananchi na kufanya juhudi za kuyapatia ufumbuzi.

 

"Kila nilipoiangalia jamii niliona imeelemewa na mzigo wa changamoto na walioumia zaidi ni wanawake na watoto na walikosa watetezi.

 

Nilikuwa naumia na ndio maana siku moja nikaamua kujitokeza kutaka kuwatetea kwa kuingia jimboni kugombea,” anasema Zawadi Amour Nassor, mwakilishi wa Jimbo la Konde Pemba.

 


Alikwenda jimboni kuchukua fomu ya kugombea akiwa hana tamaa ya kupata kutokana na baadhi ya watu kumbeza kwa kile walichodai hakuwa na pesa za kuwagaia.

 

"Nilikuwa nasikia lazima uwe na pesa ndipo ufanikiwe, lakini niliamua kutafuta mzee mmoja kupata ushauri, lakini aliniangusha kwa kuniambia niende viti maalumu, lakini sikuridhia," anaeleza Zawadi.

 

Alimtafuta mzee mwengine mwaka 2019 na kumshauri kuchukua fomu ambapo kufanikiwa na sasa anaendelea kutatua changamoto za wananchi.

 

Katika kipindi kifupi cha kuwa mwakilishi ametatua changamoto mbali mbali, ikiwa pamoja na kuchimba visima vinane.

 

Anasema, visima saba kati ya hivyo viligharimu shilingi milioni 14 kila kimoja na kimoja ambacho ni kikubwa kiligharimu shilingi milioni 21.

 

Mwakilishi huyu anahimiza malezi mazuri ya watoto kwa kutoa elimu na kulizungumzia suala hilo katika Baraza la Wawakilishi.

 

Mambo mengine ambayo anajihusisha nayo ni mpambano dhidi ya dawa za kulevya na udhalilishaji wa wanawake na watoto.

 

Vile vile, ameweka gari ya kubebea wagonjwa na huwasaidia sana akinamama na watoto ambao hupelekwa hspitali bila ya malipo.

 

Kwa kutumia fedha za mfuko wa Jimbo alizijengea uzio skuli mbili na kununua eneo la kiwanja katika kijiji cha Kipange ambacho Wizara ya Elimu inawajengea skuli, ili kuwapunguzia watoto masafa marefu ya kwenda skuli. 


Pamoja na hayo yote, mwakilishi huyo ametengeneza uwanja wa michezo na kwa sasa wapo katika hatua ya mwisho. 


"Tumezipatia jezi timu 26 za mpira na nimezisajili kwa kutumia zaidi ya shilingi milioni nne, kwa sasa timu hizi zinashiriki ligi kuu, vile vile nimewapatia mafunzo waendesha bodaboda 43 kwa gharama zangu, ili kuwasaidia kujiepusha na ajali’’, aliongeza. 


Mafanikio yake mengine ni pamoja na kuitengeneza skuli yamaandalizi ya Makangale, ili kutimiza ahadi aliyitoa wakati   akiomba kura. 


Maryam Thani Juma, mwakilishi wa Jimbo la Gando, anasema alichukuwa fomu ya kugombea katika uchaguzi wa mwaka 2015. 


Anaeleza, alishawishiwa na mumewe kugombea uongozi baada ya kuona nafasi nyingi zinachukuliwa na wanaume, huku utetezi ukiwa mdogo katika kushughulikia masuala ya maendeleo katika Jimbo.

 


Wakati akiwa barazani amekuwa akitetea mambo mengi na mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na kujengwa kwa skuli ya ghorofa iliyopo Kizimbani, hospitali ya Wilaya Kinyasini, ujenzi wa tangi la maji Raha, uchimbaji wa visima Junguni na barabara za ndani.

 

Alizitumia fedha za mfuko wa jimbo kukarabati madarasa na vyoo vya skuli mbali mbali, kujenga mabanda mawili ya skuli ya maandalizi Kwale Mpona.

 

Vile vile alichimba visima vinne katika Jimbo lake, ambapo vitatu ni kupitia fedha za wahisani na kimoja kwa kutumia fedha zake mwenyewe.

 

Alivipatia vikundi nane vya wanawake wajasiriamali zana za kufanyia kazi na fedha kwa kila kikundi laki mbili, ambapo wengine aliwadhamini kuchukua mkopo benki ya CRDB na mwisho wa siku kulipa yeye.

 

Alifanya kombe kwa wanamichezo na kutumia zaidi ya shilingi milioni nne katika kuziendeleza timu za mpira na pia alichezesha ligi ya mbuzi kwa gharama zake mwenyewe.


Baadhi ya mambo aliyoyafanya Mwakilishi wa Jimbo la Chambani Bahati Khamis Kombo katika kuling’arisha jimbo lake ni, kujenga skuli za maandalizi Chumbageni, Pujini na Chambani.


‘’Pia nimejenga madarasa na kuezeka skuli za msingi Wambaa, Ukutini na Dodo ambapo katika skuli ya Dodo pia nimekarabati vyumba vyengine vinne na stoo kwa kutia saruji na plasta,’’ anasema.


Mwakilishi huyo aliweka kifusi kwenye barabara za Wambaa- Kwaazani sokoni, alichimba kisima kwa ajili ya wananchi na wanafunzi wa skuli ya Ukutini, kulaza mipira ya kusambazia huduma ya maji safi na salama, pamoja na kufikisha huduma ya umeme kijiji cha Kwaazani.


Alijenga barabara ya kijiji cha Kumvini- Kibaridi kwa kiwango cha lami, kusimamia ujenzi wa barabara kuu ya Ole –Kengeja na vituo vya mama na mtoto, ambapo hutumia fedha za mfuko wa jimbo na fedha zake kuhakikisha maendeleo yanapatikana.

 

CHANGAMOTO WALIZOKUMBANA NAZO WAKATI WA KUGOMBEA.

 

Ni baadhi ya watu kuwatia hofu na woga kwani wao walichukulia kuwa ni kitu kikubwa na hakiwezekani kufanywa na wanawake.

 

Kuvunjwa moyo na kuambiwa kuwa hawawezi kufanya chochote kutokana na maumbile yao ya kike, jambo ambalo sio sahihi kwani wameweza na wanaendelea kuwatumikia wananchi wao.

 

Mwakilishi wa Jimbo la Konde yeye alikerwa na baadhi ya marafiki na vipenzi vyake walivyobadilika nyoyo zao na kuwa zaidi ya nyoka, kutokana na tamaa ya pesa zaidi kuliko utu na ihsan. 


Mwakilishi wa Jimbo la Gando anahadithia wanaume walitumia kigezo cha dini kuwakataza wanawake kuwa viongozi, ingawa yeye alikuwa anawatolea mifano hai ya wanawake wa kiislamu walioongoza enzi za manabii.

 

NINI KIFANYIKE

 

Wanawashirikisha wananchi katika kuibua na kutatua changamoto mbali mbali zinazowakabili na ndio maana wanafanikiwa katika kutekeleza yale waliyojipangia kuyafanya. 

"Unaposikiliza kero za wananchi na kuzitatua basi unapungukiwa kubezwa na kuonekana huna thamani, hivyo tunajivunia kuaminiwa katika majimbo yetu," anasema mwakilishi Zawadi Amour Nassor.

 Ili kuondosha migogoro kwa wananchi ni vyema wachukue juhudi ya kuwasikiliza na kuwaondolea matatizo katika vijiji vyao, watumie fedha za mfuko wa Jimbo kupeleka maendeleo kwani uwezo wa kusaidia wanao.

 

ASASI ZA KIRAIA

 

Mratibu wa TAMWA Pemba Fat-hiya Mussa Said anasema, wana mpango mkubwa wa kuwajengea uwezo wanawake na jamii, ili wawe na muelekeo chanya kushiriki kwenye vyombo vya maamuzi. 


“Na tumeona kwamba wanawake wengi waligombea katika chaguzi zilizopita, ingawa hawakushinda wote lakini walionesha moyo mzuri na walioshinda wanaendelea kufanya vizuri katika majimbo yao,” anaeleza.

 

Kwa Pemba, TAMWA imeshawapatia mafunzo wanawake 70 wenye nia ya kugombea na wamewaunganisha na wanawake mashujaa ambao tayari wameshagombea nafasi mbali mbali, ili kuwajengea uzoefu na kuwatoa hofu.

 

Hafidh Abdi Said ambae ni Mkurugenzi wa PEGAO anaeleza, wanawake wachache wanaokaa katika nafasi za uongozi, wanaonekana juhudi kubwa wanazozifanya katika kutekeleza majukumu yao. 


 ‘’Tulipofanya utafiti kwenye vyama, tulituambia kwamba wanapochaguliwa viongozi wanawake hata chama kinaimarika zaidi kwani wanachangia kwa kiasi kikubwa,’’, anasema.

 

WANANCHI

 

Wanasema kuwa, wapo tayari majimbo yote yachukuliwe na wanawake kutokana na utendaji wao wa kazi pamoja na kuwatatulia shida zao.

 

"Kwa vyovyote vile mwanamke ana huruma, hivyo wanajitahidi kutekeleza zile ahadi walizozichukua kwa vitendo, hilo limetufanya tuwapende," wanaeleza wananchi hao.

 

Hassan Salim Ali mkaazi wa Kizimbani Wete anasema, wawakilishi wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika kuisaidia jamii kuwa na maendeleo, hivyo ni muhimu kuwepo hata katika majimbo yote.

 

"Mimi naona tulichelewa sana kutambua hili, lakini tungejua mapema naona majimbo yote tungechukua sisi, mwakilishi wetu anajitutumua kwa kweli kutatua matatizo yetu, anahitaji pongezi," Asha Suleiman mkaazi wa Kiuyu kwa Manda.

 

Wingi wa wanawake waliopo nchini haujawawezesha usawa wa jinsia katika nafasi za uongozi zinazotokana na uchaguzi ili kufikia 50 kwa 50.

 

Kwani mwaka 2020 wanawake walioingia katika Baraza la Wawakilishi ni 29 kati ya 75 ya wawakilishi wote huku wanaume wakiwa 46. 


Ambapo wanawake waliogombea ni 61 na walioshinda ni nane (8), huku wanaume waliogombea wakiwa 190 na walioshinda ni 42.

 Kwa mujibu wa tume ya uchaguzi Zanzibar, wanawake walioingia Baraza la Wawakilishi mwaka 2015 ni 28 sawa na asilimia 36, kati ya wawakilishi wote 84.

 

Kutokana na idadi hiyo inaonesha dhahiri kwamba elimu imewafikia ipasavyo wanajamii na wanawake katika ushiriki wa wanawake kwenye uongozi na ndio maana idadi inaongezeka. 

Kwa kutambua umuhimu wa mwanamke, sera na sheria mbali mbali za Zanzibar zimeeleza kuhusu haki ya wanawake kushiriki katika demokrasia na uongozi.

Kifungu cha 21 (2) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 64 kimeeleza kwamba, kila mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki kikamilifu katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomuhusu mwanamke na taifa lake.

Katiba ya Zanzibar mwaka 1964 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2010 imeeleza wazi katika kifungu nambari 67 (1) kuwa, kutakuwa na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wanawake kwa idadi ya asilimia 40 ya wajumbe wote wa kuchaguliwa katika majimbo.

                                     MWISHO.

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch