Skip to main content

SHAMATA AZINDUA SOKO LA KISASA MTAMBILE

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar Shamata Shaame Khamis, amewaagiza wakulima wa ndizi wilaya ya Mkoani, kuepukana na vishoka wa biashara hiyo, na badala yake walitumie soko jipya la Mtambile, ili kupata bei kubwa.



Waziri Shamata aliyasema hayo jana, mara baada ya ufunguzi wa soko la mboga na matunda la Mtambile wilaya ya Mkoani, ikiwa ni sehemu za shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar ya mwaka 1964.

Alisema, kuanzia sasa waachane na wanunuzi wa ndizi wanaowalalia kibei, na badala yake sasa walitumie soko hilo, ili kuzipandisha thamani ndizi zao.




Alieleza kuwa, ndani ya soko hilo mtakuwa na mnada maalum wa mazao mbali mbali, ikiwemo ndizi, muhogo, matikti, nyanya, chungwa na ndimu, hivyo ni wajibu kwa wakulima hao, kulitumia soko hilo.

Waziri Shamata, alisema kwa muda mrefu, wakulima walikuwa wanalaliwa kibei na wachuuzi wanaosafirisha bidhaa hiyo nje ya kisiwa cha Pemba, kwa kueleza kuwa kunaanguko la bei.

‘’Niwatake wakulima wa ndizi, sasa iwe basi kulaliwa bei na njooni hapa ndani ya soko jipya, na muuze bidhaa hiyo na mtapata bei, maana patakuwa na ushindani wa bei,’’alieleza.

Hata hivyo Waziri huyo, aliliagiza baraza la mji wa Mkoani, kutenga bajeti maalum, kwa ajili ya matengenezo madogo madogo ya soko hilo hapo baadae.

‘’Leo (jana) tumelifungua soko hili, linang’ara na linapendeza, sasa ni wajibu kwa Baraza la mji Mkoani, kuanzia sasa kujiwekea bajeti maalum, kwa ajili ya matengenezo,’’alifafanua.

Aidha amewataka wafanyabiashara wote na hasa wale waliokuwa wakianyabiashara zao pembezoni mwa barabara, sasa kuhamia ndani ya soko hilo.

Katika hatua nyingine, Waziri huyo wa Umwagiliaji, Maliasili, na Mifugo, alisema kufanyika kwa Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, yamewakomboa wananchi kiuchumi.

Alisema kuwa, kabla ya kufanyika kwa Mapinduzi hayo, wananchi wa Zanzibar, hawakuwa na nafasi ya kulima na kuuza kwa bidhaa zao kwa thamani, jambo lililowazidishia unyonge.

‘’Tukiwa ndani ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, lazima tuwakumbuke waasisiwa wa taifa hili, akiwemo rais wa kwanza wa Zanzibar, marehemu Abied Amani Karume na mwenzake kwa kujitolea,’’alisema.

Hivyo amewataka wananchi, kuendelea kuiunga mkono serikali ya awamu ya nane, ambayo inaendelea kutekeleza dhana ya mapinduzi daima kwa vitendo, kwa kujenga miradi mikubwa ya maendeleo.

Kwa upande wake, Katibu mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Issa Mahafudhi, alisema ujenzi wa soko hilo, ni utekeleza wa ahadi ya Rais wa Zanzibar, wakati alipokutana na wajasiriamali.

Hata hivyo alisema, mji wa Mtambile umekuwa na ongezeko la watu kila mwaka, na sasa kuchukua nafasi ya tatu kwa idadi ya watu, baada ya Chambani yenye wakaazi 7,460, Kengeja 7,202 na Mtambile 7,000.


‘’Hivyo uwepo wa soko hili, limeandana na mahitaji ya wananchi kwa muda mrefu na hasa suala la changamoto, iliyopo ya wafanyabiashara kuendesha shughuli zao pembezoni mwa barabara,’’alifafanua.

 Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud, alisema serikali inampango wa kujenga soko jingine kama hilo, katika eneo shehia ya Kengeja, ili kukidhi mahitaji ya wajasiriamali.

Akizungumzia Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, alisema yalifanyika kwa lengo la kuwapa heshima wazalendo wa taifa hili, ikiwemo kujitambua kiutu na kiuchumi.





‘’Leo tukiadhimisha miaka 60, kila mmoja ni shuhuda kuwa, ameyapata matunda ya mapinduzi, iwe kwenye sekta ya elimu, afya, barabara, maji safi na salama,’’alifafanua.

Soko hilo la matunda na mboga la Mtambile inavyo vikuta 40, milango 13 ya maduka, ambapo ujenzi wake ulianza mwishoni mwa mwaka 2022, na kumalizika mwezi Julai mwaka huu.

Ujenzi huo umepitia hatua tatu, ikiwemo ukataji mlima, ujenzi wa soko lenyewe na uweka saruji chini nje ya soko hilo, lenye vyoo vinane, kikiwemo cha watu wenye ulemavu.

Aidha ujenzi huo, umegharimu zaidi ya shilingi milioni 5.88 ambapo ni fedha zinazotokana na makusanyo ya baraza la mji Mkoani, kupitia serikali kuu.

Shamra shamra hizo za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar zitaendelea tena kesho, eneo la Makangale ambapo Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar Omar Said Shaaban atalifungua tangi la maji safi na salama.

                           Mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch