Skip to main content

TUME YA UTANGAAZAJI, WADAU PEMBA WAJADILI SHERIA YA TUME

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WADAU wa Tume ya Utangaazaji Zanzibar, kisiwani Pemba, wamekutana na watendaji wa Tume hiyo, tayari kwa ajili ya kuanza mchakato, wa kuifanyia mabadiliko sheria yao nambari 7 ya mwaka 1997.

Kwenye kikao hicho, kilichofanyika leo Disemba 19, 2023 ukumbi wa wizara ya Habari Gombani Chake chake, pamoja na mambo mingine, watendaji hao wa Tume, waliwasilisha mapendekezo yao, na kisha kupokea ya wadau wao.

Akizungumza kabla ya upokeaji wa maoni hayo, Katib Mtendaji wa Tume ya Utangaazaji Zanzibar Suleiman Abdalla Salim, alisema, wanakusudia kuwa na sheria rafiki kwa vyombo vya habari vya utangaazaji na vile vya mtandaoni.

Alisema, ndio maana Tume imeanza kuwashirikisha wadau wa Unguja na Pemba, ili nao kupata nafasi ya kutoa maoni yao, kuelekea sheria mpya hapo baadae.



Alieleza kuwa, haikuwa busara kwa Tume kujifungia ndani na wataalamu wake na kisha kuwasilisha rasimu ya sheria ngazi ya Makatibu wakuu, bila ya kukutana na wadau wao.

‘’Tume kwa sasa, imeshaanza mchakato wa kuifanyia Marekebisho sheria yake nambari 7 ya mwaka 1997, pamoja na yale marekebisho yake yaliyofanywa mwaka 2010,’’alifafanua.

Akigusia baadhi ya vifungu ambavyo kwa sasa wanavipitisha kwa wadau na kutaka maoni, ni pamoja na jina la taasisi, mundo na masharti ya kuomba leseni.

Afisa Sheria wa Tume ya Utangaazaji Zanzibar Khadija Mabrouk Hassan, alisema wanatamani kuwa na sheria rafiki kwa utangaazaji na wanaoandikia maudhui mtandaoni.

Alisema sheria hiyo, vipo vifungu wanataka kuvipeleka kwa wadau, ili wavijadili  na kuwa sheria yenye kwenda na wakati uliopo kwa maslahi ya umma.

Alifafanua kuwa, kwa mfano kifungu cha 16 cha kutoa adhabu, kwamba atakayevunja masharti ya leseni, pamoja na kwamba ataonywa au kutakiwa asawazishe vipindi vyake, lakini akishindwa atatozwa faini ya shilingi milioni 1.

‘’Lakini anaweza kusitishiwa leseni yake ya utangaazaji pamoja na kufutiwa kabisa, pindi ikionekana ameshindwa kusawazisha kama sheria inavyotaka kwa sasa,’’alifafanua.

Aidha alieleza kuwa, pia kifungu cha 17 kinachoelezea haki na wajibu wa utangaazaji juu ya utaratibu wa kukanusha habari, iliyotangaazwa ambayo sio ya ukweli.

Akifungua kikao hicho, Afisa Mdhamini wiara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Pemba Mfamau Lali Mfamau, aliwataka wanaoendesha vyombo vya habari pasi na kuvisajili, wafanye hivyo haraka.

Alieleza kuwa, sasa wakati umefika kwa Tume ya Utangaazaji kutowafumbia macho, kwani kufanya hivyo, ni kosa kwa mujibu wa taratibu zilivyo.

‘’Niwatake wale wenye tv, redio na tovuti na blogi, wafike Tume kujisaliji, ili wawe halali na huru kuendesha shughuli zao za kihabari,’’alifafanua.

Akitoa maoni yake, Mkurugenzi wa Jamii tv Ali Massoud Kombo, alipendekeza kuwa, ada ya kila mwaka ya shilingi 500,000 ipunguzwe na iwe shilingi 100,000.

Aidha alipendekeza kuwa, katika Bodi ya Tume, lazima kutengwe nafasi maalum kwa ajili ya wajumbe wanawake, waandishi wa habari wa vyombo binafsi na watu wenye ulemavu.

Nae mwandishi wa redio Jamii Micheweni Time Khamis Mwinyi, alipendekeza kuwa, lazima Tume iwe na kifungu cha sheria kinachotambua muda wa majiribio, kwa waanzilishi wa redio na vyombo vya habari mtandaoni.

Mmiliki wa pwani habari tv, Juma Mussa Juma, alipendekeza kuwa, kama chombo cha habari kimekosea na kuna lazimika kupigwa fani, ianzie shilingi 100,000 na sio shilingi milioni 1 kama ilivyo sasa.

Akifunga kikao hicho, Mrajisi Tume ya Utangaazaji Zanzibar Mohamed Said Mohamed, alisema lazima kila jambo, kuwepo ushirikiano miongoni mwao.

Hata hivyo, amewakumbusha wamiliki wa redio, tv na vyombo vya habari mtandaoni, kuharakisha ada ya malipo ya mwaka pamoja na malipo ya leseni zao.

Tume ya Utangaazaji Zanzibar, imeanzishwa chini ya sheria nambri 7 ya mwaka 1997, ambapo moja ya kazi zake ni kusimamia shughuli za utangaazaji ikiwemo kutoa leseni.

                           Mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch