Skip to main content

IPA: ‘’WAALIMU ENDELEENI KUJIPAMBA KWA TABIA NJEMA’’

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

CHUO cha Utawala wa Umma Zanzibar ‘IPA’ tawi la Pemba, kimewakumbusha waalimu, wa skuli za wilaya ya Chake chake, kuendelea kuwa kioo, kwa kuwa na maadili mema ndani ya jamii.

Ushauri huo umetolewa Disemba 18, 2023  na Mkuu wa chuo hicho tawi la Pemba, Juma Haji Juma, wakati akiwasilisha mada ya maadili kwa watumishi wa umma, kwenye mafunzo ya uthibitisho wa kazi, kwa waalimu hao, mafunzo yaliyofanyika skuli ya sekondari Madungu wilayani humo.

Alisema, jamii inategemea na kusoma kila kitu kutoka kwa Mwalimu, hivyo ni wajibu wake, hilo kulijua na kuhakikisha anaendelea kung’ara ndani ya jamii, kwa kujipamba na maadili mema.

Alisema, Mwalimu anaangaliwa kuanzia kivazi, matendo, jinsi anavyokula na mazungumzo yake katika jamii, hivyo anapaswa kuhakikisha anakuwa makini saa 24 kwenye maisha yake.

Alieleza kuwa, miongozo ya sheria na kanunu za kiutumishi, zipo kwa ajili ya kutoa muongozo zaidi, lakini Mwalimu mwenyewe analazimika kuongeza wigo, wa kujipamba na tabia njema.

‘’Mwalimu ndio kila kitu ndani ya jamii, kuanzia kivazi, aina ya maeneo anayokaa kuzungumza, matumizi ya lugha na hata namna anavyoilinda nchi yake, kwa maneno mazuri,’’alieleza.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa tawi la ‘IPA’ Pemba, Juma Haji Juma, alisema eneo jingine kwa waalimu wanatakiwa kuhakikisha wanaishi nalo, ni dhana ya uzalendo kwa taifa lao.

Akifungua mafunzo hayo, Mratibu Idara ya Utumishi na Uendeshaji kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba, Harith Bakar Waziri, alisema wizara haitaki kuona, kuwa kuna mtumishi anatimiza miaka miwili, pasi na kupata mafunzo ya uthibitisho wa kazi.





Alifafanua, ndani ya awamu hii ya serikali ya awamu ya nane, Wizara imepewa kipaumbele cha aina yake, ikiwemo kuwezeshwa kufanya mafunzo hayo.

‘’Mafunzo haya mkimaliza yatawapa haki mbali mbali, ikiwemo ya likizo, safari kikazi kwani ni sehemu ya uthibitisho wa kazi, kwa mujibu wa sheria za utumishi wa umma,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, Mratibu huyo, alisema mafunzo hayo yataendeshwa Pemba nzima, kwa waalimu wote ambao wameajiriwa hivi karibuni, ili kuweka sawa matakwa ya kisheria.

Akiwasilisha mada ya dhana ya muwamko wa kustaafu salama kwa watumishi wa umma, mtendaji kutoka ‘IPA’ Ali Issa Matlubu, alisema mada hiyo ni mpya kwa watumishi wapya.

Alieleza kuwa, IPA iliona iwaletee mada hiyo watumishi hao wapya, ili wafahamu kuwa, mara baada ya kuajiriwa kitendo kinachofuata ni kustaafu, iwe kwa lazima, hiari au sheria.



Hata hivyo amesema, tafiti mbali mbali zinaonesha kuwa 70, kila wastaafu 100 wanakosa matayarisho muhimu ya kuelekea kustaafu, jambo linalosababisha magonjwa na hatimae vifo.

Mafunzo hayo ya siku mbili, mada nane zitafundishwa ikiwemo uzalendo, sheria ya Afya na Usalama kazini, sheria ya Utumishi wa umma, Maadili ya watumishi, sheria ya Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa uchumi ‘ZAECA’ pamoja na dhana ya kustaafu kwa salama.

                                                           Mwisho  

 

 



Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch