Skip to main content

SORAGA AWEKA JIWE LA MSINGI KITUO CHA POLISI MKOANI, AACHA UJUMBE WA MAPINDUZI

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAZIRI wa Nchi, Ofis ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar,  Mudrik Ramadhan Soroga, amesema miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar, imemletea heshima mzanzibari, kwa kupata haki zake bila ya ubaguzi, ikilinganishwa na kabla ya mwaka 1964.

Alisema, kwa sasa kila mmoja anapata haki ya kuwasilisha lalamiko lake, katika vyombo vya sheria na kupokelewa kwa heshima na kisha kusikilizwa na uamuzi kutolewa kwa haki.

Waziri Soraga, aliyasema hayo leo Disemba 22, 2023  mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la kituo cha Polisi cha wilaya ya Mkoani cha daraja ‘B’ ikiwa ni sehemu za shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar ya mwaka 1964.

Alisema, sasa mzanzibari anatembea kifua mbele, akijua kuwa inapotokezea kubinywa kwa haki zake, anapopakukimbilia na kufungua mashauri, ambayo yanaendeshwa kwa haki kuanzia mwanzo hadi mwisho.



Alieleza kuwa, waasisi wa taifa hili walipigania haki za wazalendo na mwendo huo unaendelezwa hadi leo ndani ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiwemo ujenzi wa vituo vya kisasa vya Polisi.

‘’Niwaambie kuwa, ujenzi huu wa kituo cha Polisi Mkoani, ni sehemu ya matunda ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ambayo msingi wake mkuu ni Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964,’’alifafanua.

Akizungumzia Mapinduzi hayo, Waziri Soroga, alisema yameleta tija kwa wananchi wa Zanzibar, kwani kabla ya hapo utu, heshima, hadhi ya mzalendo haikuwa ikitambulika.

Alieleza kuwa, kilichokuwa kikijitokeza kwa wazazi wa wakati huo, ni madhila, kufanyishwa kazi ngumu zenye malipo duni na ambayo hayakujali utu wao.

Alifahamisha kuwa, suala la kukosa haki, elimu, matibabu na huduma nyingine muhimu kwa wakati huo, lilikuwa jambo la kawaida, hali ambayo wapinga dhulma iliwauma.

‘’Leo tunafuraha kubwa mno, baada ya waasisi wa taifa hili, kufanya mbinu za kimapinduzi, mkoloni ameshaondoka na sasa kila mmoja ananeemeka na matunda ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964,’’alieleza.

Akizungumzia uwepo wa kituo hicho cha Polisi daraja ‘B’ Waziri huyo, ameliomba Jeshi la Polisi iwe chachu ya kufanyakazi kwa bidii na kutoa huduma bora bila ya upendeleo kwa wananchi.

Alieleza kuwa, kituo hicho kikazae matunda ya kutokomeza majanga yaliomo ndani jamii, ikiwa ni pamoja na vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa wanawake na watoto, dawa za kulevya na ulevi.

Aidha amewakumbusha kuendelea kukitunza, kukilinda na kukienzi, ili kiwafae kizazi cha sasa na kijacho, kwani gharama za ujenzi wa kituo hicho ni kodi za wananchi.

Mapema Kamanda wa Polisi mkoa wa kusini Pemba, Abdalla Hussein Mussa, alisema kituo hicho kimewapa ari na kasi zaidi ya utendaji kazi, hasa kwa vile kinahuduma zote muhimu.

Alieleza kuwa, kituo cha kisasa chenye vyumba 31, ikijumuisha chumba kwa ajili ya mkuu wa kituo, mkuu wa Polisi wilaya, mkuu wa upelelzi wa makosa ya jinai, vyamba saba kwa ajili ya mahabusu wakiwemo watu mashuhuri, watoto wa kike na kiume, watu wazima.

Aidha alieleza kuwa mradi wa ujenzi huo umegharimu shilingi milioni 700, ambapo kati ya fedha hizo, shilingi milioni 580 ni gharama ya ujenzi na shilingi milioni 120 ni malipo ya fundi.





Alifahamisha kuwa, mradi huo ambao umejengwa na fundi wa ndani ya jamii, ulianza Mei 11, mwaka huu na kumalizika, Disemba 5 mwaka huu na tayari kwa ajili ya kuhamiwa.

‘’Ujenzi wa kituo hichi kipya cha Polisi hapa wilaya ya Mkoani, ni hatua kubwa ya serikali, katika kuwandoshea wananchi na Polisi changamoto za eneo la kazi, kwani sasa huduma zitatolewa kwa ufanisi,’’alifafanua.

Mapema Katibu mkuu ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Sera, Uratibu na Barazala la Wawakilishi Zanzibar Dk. Islam Seif, alisema kwa sasa kila mmoja ni shuhuda, jinsi Zanzibar ilivyopiga hatua ya maendeleo.




Alieleza kuwa, viongozi wa kitaifa wa Zanzibar, waliosimamia kufanyika kwa Mapinduzi haya, wamefanyakazi kubwa ya kuwakomboa wananchi mbali mbali, na kwa sasa kila mmoja anatembea kifua mbele.

Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud, alisema serikali bado inayonia ya kujenga vituo vyingine vipya vya Polisi, ili wananchi wapate huduma bora katika mazingira bora.

Hata hivyo, amewakumbusha Jeshi la Polisi, kuendelea kufanyakazi kwa bidii na kwa dhana ile ya ile, ya kuwalinda wananchi na mali zao tena bila ya ubaguzi.




Alisema huu sio wakati tena kwa wananchi, kuendelea kulilalamikia Jeshi la Polisi kiutendaji, kwani waelewe kuwa, ujenzi wa kituo hicho kipya ni kodi za wananchi.

Shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, zitaendelea tena asubuhi hii, kwa Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Omar Said Shaaban kulifungua tangi la kuhifadhi maji Makaangale, ambapo kesho Waziri huyo, pia ataweka jiwe la msingi la mradi wa utotoleshaji vifaranga vya matango bahari, shehia ya Pujini wilaya ya Chake chake.

                            Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch