Skip to main content

WANAWAKE MLETENI WAKUMBUSHIA AHADI UJENZI KITUO CHA AFYA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAWAKE wa kijiji cha Mleteni shehia ya Kisiwani wilaya ya Wete, wameikumbusha serikali kuwajengea kituo chao cha Afya, kama ahadi ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, alivyoitoa wakati alipowatembelea.

Walisema, tayari wameshakuwa na eneo ambalo walitakiwa kulitoa kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho cha afya, ingawa hadi sasa ni miezi zaidi ya mitano tokea Rais atowe ahadi, ingawa hakujaanza ujenzi.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kijijini hapo, walisema wanahamu kubwa na kujengewa kituo hicho, ili sasa kwao iwe rahisi, kupata huduma mbali mbali zikiwemo za uzazi na mtoto.

Walieleza kuwa, wamekuwa wakiifuata huduma hiyo eneo la Kisiwani ambapo pana umbali wa zaidi ya meli mbili, jambalo linalowapa ugumu, hasa kutokana na uchakavu wa barabara yao.

Mmoja kati ya wanawake hao Aisha Nassir Sheha, alisema kutokana na umbali wa kituo cha afya hasa huduma za mama na mtoto, wengi wao wamekuwa hawamalizi mtiririko wa kuhudhuria kliniki.

‘’Zipo baadhi ya siku hutakiwa kufika kliniki kwa ajili ya uchunguuzi, lakini kutokana na umbali na uchakavu wa barabara yetu, hukatisha,’’alisema.

Alieleza kuwa, inakuwa vigumu kwa mjamzito kuanzia miezi sita kutembea umbali mrefu, kufuata huduma Kisiwani, na hasa kutokana na uchakavu wa barabara yao.

Kwa upande wake Husuna Mohamed Kombo, alisema hakuna hata mjamzito mmoja anaemaliza siku kamili za kuhudhuria kliniki eneo la Kisiwani, kutokana na umbali uliopo hadi hospitalini.

‘’Ni vyema kwa serikali kutimiza ahadi yake ya ujenzi wa kituo cha afya kijiji cha Mleteni, ili wananchi sasa tuwe na uhakika wa huduma,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, mwananchi huyo alisema, kama huduma nyingine ikiwemo umeme, maji na skuli imeshajengwa, ni wakati sasa na kituo cha afya kujengwa.

Kwa upande wake Mkubwa Abdalla Yussuf, alisema kutokana na uchakavu wa barabara yao, hata gari inakuwa ni usumbufu kuwafuata wagonjwa au wajawazito.




Hivyo ameikumbusha serikali, kutekeleza ahadi yake ya ujenzi wa kituo cha afya, hasa kwa vile tayari wameshapata eneo karibu na skuli yao ya maandalizi.

Kaimu Sheha wa shehia ya Kisiwani wilaya ya Wete Bahati Juma Mtwana, alisema ni kweli eneo kwa sasa wameshalipata na wananchi waliwashi kuliondolea vichaka hivi karibuni.

Mkuu wa wilaya ya Wete Dk. Hamad Omar Bakar, alisema ujenzi wa kituo cha afya bado uko pale pale, ingawa umechelewa kutokana na kukamilisha miradi walioiomba mwanzo wananchi hao.

Alieleza kuwa, baada ya kufika Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi kijijini hapo, wananchi hao kwanza waliomba skuli ya maandalizi ambayo tayari imeshajengwa.

‘’Kisha waliomba huduma ya maji safi na salama na huduma ya umeme, na tayari huduma hizo zimeshafikishwa kijijini hapo kwa muda mfupi,’’alieleza.

Hata hivyo Afisa Mdhamini wizara ya Afya Pemba Khamis Bilali Ali, amewataka wananchi na hasa akina mama kuendelea kukitumia kituo cha afya cha Kisiwani.

‘’Wajawazito wanatakiwa kuhakikisha wanahudhuria kliniki, kwa ajili ya kupata maendeleo ya mama na mtoto, kwani kinyume chake kunaweza kukajitokeza matatizo,’’alieleza.



Wakati rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi alipowatembelea wananchi hao, aliwaahidi kuwafikisha huduma kadhaa za kijamii ikiwemo umeme, afya, elimu, maji na barabara.

                          Mwisho      

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch