Skip to main content

HAKI YA AFYA YA UZAZI JUKUMU LA WOTE: TAMWA-ZANZIBAR

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

JAMII imekumbushwa kuwa, suala la afya ya uzazi, sio jukumu la mwanamke pekee, kama wengine wanavyofikiria, bali linahusu jamii yote, ili kuwa na afya bora iwe ya kimwili au kiakili.  

Kauli hiyo imetolewa leo Julai 29, 2023 na Afisa Mradi wa haki ya afya ya uzazi kutoka Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA- Zanzibar Zaina Abdalla Mzee, wakati akiutambulisha mradi huo, kwenye mafunzo ya siku tatu kwa waandishi wa habari, kisiwani Pemba.

Alisema, imegundulika na tafiti zinaonesha kuwa, linapozungumza suala la haki ya afya ya uzazi, huangaliwa zaidi mwanamke, bila ya kumuhusisha mwanamme.

Alieleza kuwa, hakuna suala la uzazi linalomgusa mwanamke pekee, na hasa likihusisha afya, kwani mwanamme asipowajibika, anaweza kusababisha madhara kwa mjamzito na mtoto wake.




‘’Hii ndio maana, TAMWA-Zanzibar imeibua mradi huu ambao sasa utawawezesha waandishi wa habari, kuieleza jamii, madhara ya kutozingatia haki ya afya ya uzazi na faida zake,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Afisa huyo mradi wa haki ya afya ya uzazi, alisema anaviamini mno vyombo vya habari, katika kuieleza jamii, maana ya afya ya uzazi kwa ufasaha.

Akifungua mafunzo hayo, Afisa ufuatiliaji na tathmini kutoka TAMWA- Zanzibar Mohamed Khatib Mohamed, alisema utafiti unaonesha kuwa, vyombo vya habari viko chini katika kielimisha jamii kwa ufasaha, juu ya haki ya afya ya uzazi.

Alifahamisha kuwa, kupitia mradi huo, anatarajia kuona mafanikio kadhaa, moja wapo ni kupunguzika kwa vifo vya mama na mtoto na ushiriki wa wanaume, katika afya ya uzazi.



Hata hiyo Afisa huyo, alieleza kuwa, bado katika jamii zipo dhana potofu kadhaa, ikiwemo uleaji mimba, mtoto na majukumu ya ndani, kuendelea kuachiwa mwanamke pekee.

‘’Waliowengi hawaoni athari ya mwanamke kukosa kwenda kilini kwa wakati, kukosa lishe bora wakati wa ujauzito na hata kutosindikizwa anapokwenda kliniki, haya yanaweza kumpoteza mtoto yasipozingatiwa,’’anasema.

Akiwasilisha mada ya mtazamo wa dini ya kiislamu, juu ya afya uzazi, Sheikh Abdalla Nassor Abdalla ‘Mauli’ kutoka Jumuiya ya Maimamu Zanzibar ‘JUMAZA’ alisema hilo linazia tokea uchaguaji wa mwenza, katika ndoa.

‘’Uislam umeelekeza hata namna ya kumuendea mwenza wako, namna ya kuilea mimba, ushiriki wa mwanamme kabla na baada hata ya kuzaliwa mtoto,’’alieleza.




Hata hivyo sheikh huyo, alisema uislamu ndio muanzilishi wa uzazi wa mpango, pamoja na uimarishaji wa afya ya mjamzito pamoja na uleaji na makuzi ya mtoto.

Kwa upande wake, Mratibu Tume ya Ukimwi Zanzibar ofisi ya Pemba Ali Mbarouk Omar, alisema waandishi wa habari wazuri, ni wale wanaozijua istilahi za haki ya afya uzazi, ili iwe rahisi, wakati wa kuwaelimisha wananchi.

‘’Kwa mfano ujue nini maana ya umri baleghe, utoaji mimba ulioruhusiwa, mimba zisizotarajiwa, umuhimu wa haki ya afya ya uzazi pamoja na athari za kuzaa kila mwaka,’’alifafanua.

Wakichangia kwenye mafunzo hayo, waandishi hao wa habari walisema, elimu hiyo kwao ilikuwa mpya na hawakua na uwelewa wa kutosha.



Mwandishi wa blog ya Pemba ya leo, Fatma Hamad Faki, alisema hakuwa akijua kuwa, anaweza kupata maeneo mengi ya kuwaelimisha wananchi, juu ya afya uzazi.

Meneja wa redio Jamii Micheweni Ali Massoud Kombo, alisema wamekuwa wakifanya vipindi vya aina hiyo kwa muda mtefu, ingawa hakuwa na uwelewa kwa baadhi ya mambo.

Mwandishi wa kujitegemea Hassan Msellem, alisema sasa amejua kuwa, dini haikatazi kufanya vipimo na mtarajiwa, ili kuelewa uwezo baina yao.

Maradi huo wa majaribio wa mwaka mmoja, unaendeshwa katika wilaya za Magharibi B, Kati kwa Unguja na wilaya ya Chake chake kwa Pemba.

Ambapo mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya TAMWA-Zanzibar na wenzao wa Tanzania bara, unafadhiliwa na Shirika la Wellspring Philonthropic fund la Marekani.




Ambapo shabaha kuu ya mradi huo ni kuwajengea uwezo waandishi wa habari, ili kuripoti kwa ufanisi, juu ya haki ya afya ya uzazi kwa wanawake na wasichana walioko mjini na vijijini.

                  Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch