Skip to main content

ELIMU YA AFYA YA UZAZI NI HAKI KWA KILA BINADAMU

 



 NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR 

VYOMBO vya habari nchini vimetakiwa kuibua matatizo mbalimbali yanayohusiana na afya ya uzazi kwa wanawake na wasichana jambo ambalo husababisha wanawake wengi kutojiunga na huduma ya afya ya uzazi.

 

Akifungua mafunzo ya siku tatu kwa vyombo vya habari kwa niaba ya Mkurugenzi wa chama cha  waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA ZNZ,  mjumbe wa bodi ya Chama hicho Shifaa Said Hassan, alisema ni wajibu kwa waandishi kufatilia na kuandika matatizo yanayowakabili wanawake hususani wanapotaka kujiunga na  huduma hizo ili waweze kujua njia bora na salama.

 

 “Licha ya kuwepo kwa sera na seheria zinazosisitiza umuhimu wa mwanamke kupata huduma hizo lakini inaonekana asilimiia kubwa ya kundi hilo hawana uelewa wa kutosha juu ya matumizi sahihi ya huduma hiyo hivyo kupitia vyombo vya habari itakuwa chachu ya kuwaelekeza na kufikia malengo ya kuimarisha afya zao,”Shifaa Said, amesma.

 

Aidha aliwaomba  waandishi wahabari kuwa kusikiliza kwa makini mafunzo wanayopata kwa lengo la kuyafanyia kazi ipasavyo ili yalete tija kwa jamii na taifa kwa ujumla.

 

Kwa upande wake mkufunzi na Mwandishi Mkongwe  wa mafunzo hayo Salim Said Salim alisema wanawake wengi na watoto wanakosa haki zao za msingi ikiwemo kukosa lishe bora malezi ya  pamoja baina ya mke na mume,  hali ambayo husababisha jamii kukosa kizazi kisicho bora.

 

 Amesema waandishi wahabari  lazima wafatilie na kuibua ishu ambazo zinahusiana na haki ya afya ya uzazi na badala yake wasiridhike na kufunguliwa kwa vituo vya afya.

 

 “Nawasisitiza waandishi wahabari kufanya uchunguzi juu ya huduma zinazotolewa kama kuna madaktari wa kutosha, dawa za kutosha ili kwenda sambamba na mahitaji ya wananchi katika kupata huduma bora,”Salim Said Salim,Mkufunzi.

 

Akiwasilisha mada ya afya ya Uzazi na malezi ya watoto katika Uislamu Mjumbe wa Baraza la Maulamaa kutoka Ofisi ya Mufti Zanzibarm Sheikh Khamis Abdulhamid Khamis amesema katika kuwalea watoto ni jukumu la wazazi kuzingatia umri wa mtoto tokea siku anayozaliwa mpaka kufikia baleghe na kuendelea kujenga ukaribu na kuwafatilia katika nyendo zao.




 

‘’Katika malezi ya watoto, ni wajibu wa wazazi kushirikiana kwa pamoja kujuwa tabia za watoto wao. Watu wanaoshirkikana nao kama vile marafiki, ni lazima kuwachagulia marafiki wema, hii itawasaidia hata makuzi yao, na pia husaidia kuimarisha afya ya uzazi na malezi kwa mtoto kwa mujibu wa kitabu kitukufu cha qur ani kupitia aya mbali  mbali za qurani,” Sheikh Khamis Abdulhamid.

 

Nae Mkufunzi wa magonjwa ya Uzazi na wanawake kutoka hospitali ya Rufaa Mnazi mmoja Dk Ummulkulthum O.Hamad amesema waandishi wahabari kutekeleza wajibu wao ipasavyo kwa lengo la kuelimisha jamii kuhusu masuala ya haki ya afya ya uzazi,

“Katika jamii kuna shida bado Elimu ni ndogo kabisa kuhusu afya ya uzazi, ukizungumzia suala hili jamii yetu inadhani ni suala la wanawake pekee bali ni la linamgusa kila binadamu kwa sababu mtoto akizaliwa jambo la kwanza unaulizwa umepata mtoto gani? Badala ya kuuliza hali ya mama mtoto inaendeleaje, hapa ujuwe tayari jinsia imeanza, Dk Ummulkulthum O.Hamad,  Daktari wa magonjwa ya uzazi na wanawake kutoka hospitali ya Rufaa Mnazi Mmoja.

 

Nao waandishi wahabari wamesema watayatumia mafunzo waliyoyapata kwa kuandika habari na kutayarisha vipindi vinavyohusiana na haki ya afya ya uzazi kwa lengo la kutoa Elimu kwa jamii ili kuondokana na dhana potofu kwamba masuala haya yanamuhusu mwanamke pekee.

   

 


 

Washiriki wa mafunzo hayo wakieleza changamoto ziliyopo katika afya ya uzazi walisema ni pamoja na madaktari wanaotowa huduma hiyo kutokuwa na lugha nzuri kwa wagonjwa sambamba na kutokuwa na uelewa juu ya baadhi ya huduma wanazizitoa

 

Mafunzo hayo ya siku tatu yameandaliwa na tamwa zanzibar kwa lengo la kuwajengea uwezo waandishi wa habari ili kuielimisha jamii kuhusiana na afya ya uzazi.


MWISHO


 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch