Skip to main content

MAUZO YA MADINI YAPAA ZANZIBAR

 

 
 NA  HAJI MTUMWA, ZANZIBAR :::

SERIKALI ya Mapinduzi  Zanzibar  (SMZ) kupitia Wizara ya Maji, Nishati na Madini imeingiza mapato ya sh. bilioni tatu na milioni hamsini na sita kwa kipindi cha miezi mitatu ikiwa ni mauzo ya maliasili zisizorejesheka ikiwemo kifusi, mchanga  mawe, kokoto na vumbi.

Hayo yameelezwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizaya hiyo ambaye amehamishiwa katika Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi, Dkt Mngereza Mzee Miraji wakati akimkabidhi ofisi Katibu Mkuu mpya wa wizara  hiyo  Joseph John Kilangi aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi.

Dkt. Mngereza amesema kutokana na changamoto za upotevu wa maliasili kwa kushirikiana na watendaji wake waliamua kuchukua hatua za makusudi kuazisha mfumo wa kuombea maliasili zisizorejesheka ili kuzuia upotevu mali hizo. Hivyo April hadi Juni wizara hiyo imeweza kuingiza fedha hizo  ambapo  mwezi wa Juni pekee uliingiza shilingi bilioni moja na nusu.

“Mfumo huu ni mzuri sana kwani unaweza kuona gari inapoingia katika shimo la maliasili, mali iliyobeba, uwezo wa gari, na wapi inaelekea hali ya kuwa nipo ofisini hata usiku. Pia   mtu akilipa malipo benki kupitia mfumo huu unaonesha fedha zilizoingia aina zote za malipo kuanzi kibali shilingi 3000, kutokana na kamera zilizofungwa. Hii ndio ilikuwa kazi ngumu ya kudhibiti upotevu wa maliasili” alisema Dkt.Mngereza

Aidha Dkt. Mngereza aliwashukuru watendaji kazi wa wizara hiyo  kwa mashikiano makubwa waliyompa katika kipindi chote alichotumika wizara hiyo kwani walikuwa wakifanya kazi kwa mashikiano ya karibu hali ambayo imeonesha dhamira ya Serikali katika kuwaletea wananchi  wake maendelo.

Kwa Upande wake Katibu Mkuu wa Wizara Hiyo Joseph J. Kilangi aliyekabidhiwa amesema anaamini yote aliyokabidhiwa atayaendeleza kwa dhati ile ile  hivyo, amewaomba watendaji wa wizara hiyo kumpa mashirikina kama walivyompa Dkt Mngereza kwa sababu wote wanajenga nyumba moja ya kutekeleza ahadi za Serikali ya Awamu ya Nane inayongoza na Rais Dkt Hussein Mwinyi.

Aidha amewataka watendaji wa wizara hiyo kutomchoka mapema kutokana na kuwaita mara kwa mara kwani majukumu hayo ni mapya kwake hivyo anahitaji kujifunza mambo mengi kupitia kwao. Amesema anaamini akipewa mashirikiano hakuna kitakacho mshinda kwani kinachohitajika ni uwazi na uwajibikaji.

Mapema Waziri wa Wizara hiyo, Shaibu  Hassan Kaduara amemshukuru Dkt Mngereza kwa mashirikiano makubwa aliyompa pamoja na juhudi za kuanzisha mfumo huo. Amesema mashirikinao ya  Dkt. Mngereza yameweza kufanikisha bajeti  ya wizara hiyo kupita kwa urahisi hivyo amewataka watendaji wa wizara hiyo, kuendeleza ili ufanisi upatikane.

Makabidhiano hayo yamekuja kufuatia uteuzi aliyoufanya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapiduzi Zanzibar Dkt Hussein siku ya Juni 30,2022 wa kuwateua manaibu katibu mkuu pamoja kuwabadilisha makatibu wakuu wa wizara mbali mbali za SMZ.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch